Posts

UHAKIKI RIWAYA YA TAKADINI PDF

Image
RIWAYA: TAKADINI MWANDISHI: BEN J HANSON WACHAPISHAJI: METHEWS BOOKSTORE AND STATIONERS MWAKA: 2004 MHAKIKI: DAUD MAKOBA MUHTASARI WA RIWAYA Takadini ni riwaya inayojaribu kuzungumzia matatizo ya mila na desturi yaliyopo katika jamii za Kiafrika hasa sehemu za vijijini. Mwandishi anamuonyesha mhusika mkuu Takadini aliyezaliwa na ulemavu wa ngozi jinsi anavyotengwa na watoto, watu wazima na jamii yote kwa ujumla. Mwisho tunamuona Takadini akipendwa na msichana Shingai. Pamoja na vikwazo vingi, penzi la Shingai na Takadini halikufa. Baadae Shingai anapata mimba ya Takadini, kisha anajifungua mtoto asiye mlemavu. Hapo wana jamii wanashangazwa na kujikuta wakiamini kuwa hata mlemavu anaweza kuzaa mtoto asiyemlemavu. UCHAMBUZI WA FANI NA MAUDHUI MAUDHUI KATIKA RIWAYA YA TAKADINI DHAMIRA UKOMBOZI WA KIUTAMADUNI Utamaduni ni jumla ya maisha ya jamii. Katika jamii ya  Zimbabwe watu wenye ulemavu hawakuruhusiwa kuishi, waliuawa kikatili. Ni katika jamii hii pia, ...

UHAKIKI WA RIWAYA YA WATOTO WA MAMAN’TILIE

Image
MWANDISHI: EMMANUEL MBOGO WACHAPISHAJI: HEKO PUBLISHERS MWAKA: 2002 MHAKIKI: MWALIMU MAKOBA WASIFU WA MWANDISHI Emmanuel Mbogo ni Profesa wa drama na fasihi na amehudumu katika vyuo vikuu mbalimbali ikiwemo, Chuo Kikuu cha Kenyatta Kenya na Chuo Kikuu Huria. Mbogo ni mwanafasihi mahiri sana katika Afrika ya Mashariki. MUHTASARI WA RIWAYA Maman’tilie, mama mwenye watoto wawili lakini wote wamefukuzwa shule kwa kukosa ada na sare. Anajitahidi hapa na pale ili apate, lakini wapi? fedha imegeuka nyoka inateleza kwenye nyasi. Mumewe Mzee Lomolomo hana muda, yeye kila kukuchapo huelekea bunge la walevi kunywa pombe tani yake. Akiwa huko hunywa na kurudi nyumbani akiwa mbwii! Mwisho mwandishi anauliza swali gumu, ‘Nani anajali?’ UCHAMBUZI WA FANI NA MAUDHUI MAUDHUI KATIKA RIWAYA YA WATOTO WA MAMAN’TILIE Maudhui hujumuisha mawazo na pengine mafunzo mbalimbali yaliyomsukuma mtunzi ama mwandishi wa kazi ya fasihi akaandika kazi yake. DHAMIRA Dhamira ni...