Posts

MUSTAKABALI WA MAENDELEO YA KISWAHILI KATIKA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Image
  Bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Picha/ HISANI   P. KIMANI wa Masshele blog  Kwa Mukhtasari WAKATI wa kipindi cha kupigania uhuru nchini Tanganyika na kwa kiasi kikubwa Kenya, Kiswahili ndiyo lugha iliyotumiwa kuwaunganisha wakazi wa mataifa hayo. Harakati za siasa zilipoanza kupamba moto nchini Tanganyika, lugha ya Kiswahili ilikuwa 'silaha’ madhubuti iliyotegemewa na chama cha Tanganyika African Association (TAA) kupigania ukombozi. Isitoshe, Chama cha Tanganyika African National Union (TANU) kilipoanzishwa rasmi 1954, viongozi wake walilazimika kutumia Kiswahili mikoani na wilayani kuwashawishi wananchi kujiunga na harakati za ukombozi. Ni sehemu chache sana ambapo lugha za kikabila zilitumiwa na kuhitaji mkalimani wa Kiswahili.   Kwa maana hiyo, Kiswahili kilikuwa ni alama ya umoja, uzalendo na uhuru. Hapa Kenya wakati wa utawala wa Uingereza, Kiswahili kilitumika katika baadhi ya shule za msingi hasa ma...

Paul Makonda Aamua Kufunguka Kuhusu Diamond na Alikiba, Adai Anapenda Ugomvi wao..Lakini....

Image
Mkuu wa Mkoa wa Dar ss Salaam Paul Makonda ameamua kuandika maoni yake kutokana na kile anachokiona kuhusu wasanii wa Bongofleva wanaoshindanishwa kimuziki ambao ni Alikiba na Diamond. RC Makonda ameaandika maneno 17 kwenye Instagram ambayo yanawahusu mastaa hao wanaotajwa kuwa wana ushindindani kimuziki akionesha kufuraishwa na kazi za mastaa hao lakini akiwaonya tofauti zao kutovuka mipaka na kuvunja sheria au tamaduni za kitanzania. “Tofauti zenu mimi nazipenda, kwani zinaleta ushindani mzuri kwenye mziki. Ila naomba mzingatie sheria na Utamaduni wetu..” – RC Makonda Tupe Maoni Yako Chini

Ukweli Mchungu...Kisheria Matonya Hana Haki yoyote ya Kusema Ameibiwa Nyimbo ya Zilipendwa na Diamond....

Image
Na Zawadi B Lupelo Tulipokuwa tukisoma kiswahili mwalimu wetu wa fasihi (kiswahili 2) alipenda sana kutoa tafsiri ya neno mojamoja. Alituambia SANAA ni UFUNDI wa kueleza mawazo yaliyo katika fikra za mwanadamu. Ni kweli mwanadamu ana mawazo mengi sana lakini kuna namna ya kueleza hayo mawazo hivyo basi wanachokifanya wasanii ni ule ufundi wao wa kueleza yale yaliyomo akilini mwao. Kilichomo kwenye akili ya Diamond (mawazo yake) yanaweza yakawemo pia kwenye akili ya mtu mwingine yeyote lakini mtu huyo asiwe na ufundi wa kueleza mawazo hayo kama anavyofanya Diamond Platnumz. Anaweza asiwe na sauti kama yake, anaweza asiwe na uwezo wa kuandika mashairi kama yake, uwezo wa kunata na beat kucheza nk. Maneno ya mwalimu wetu wa kiswahili 2 hayakuwa mbali na sheria zetu hasa inapokuja kwenye sanaa. Sheria za hati miliki zinatambua uwepo wa ufundi binafsi kwa msanii wa kuwasilisha mawazo aliyonayo ndiyo maana sheria inalinda ule ufundi wa msanii na si vinginevyo. Ili nieleweke vyema...

Papa asisitiza kusitishwa mashambulizi dhidi ya Waislamu wa Rohingya

Image
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesisitiza kusitishwa mashambulizi na utumiaji mabavu dhidi ya Waislamu wa kabila la Rohingya huko Myanmar. Papa Francis ameeleza kusikitishwa na mashambulizi hayo dhidi ya Waislamu wa Rohingya wa nchini Mynamar na kusema kuwa: Watu wote wanapaswa kusaidia ili kufanikisha kukomeshwa mashambulizi na hatua za ukandamizaji dhidi ya Waislamu wa Myanmar.  Kiongozi wa Kanisa Katoliki ameongeza kuwa haki za jamii hiyo ya Waislamu zinapasa kuheshimiwa. Waislamu wapatao 92 wa kabila wa Rohingya wameuawa katika kipindi cha siku kadhaa zilizopita wanaoishi katika mkoa wa Rakhine huko Myanmar kufuatia kushadidi mashambulizi na ukandamizaji wa jeshi la nchi hiyo. Waislamu wa Rohingya wa nchini Myanmar   Mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa na Mabudha wenye misimamo mikali na wanajeshi wa Myanmar dhidi ya Waislamu wa Rohingya katika mkoa wa Rakhine magharibi mwa nchi hiyo tangu miaka kadhaa iliyopita hadi sasa yamesababi...

Rasmi: Msako wa Wanafunzi wajawazito kuanza

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Fadhil Nkurlu amesema kamati ya ulinzi na usalama imekamilisha utaratibu wa kuwasaka wanafunzi wenye mimba ili kuchukua hatua inayostahili. Kiongozi huyo ametoa kauli hiyo akiwa katika Kata ya Ntobo, kwenye  Halmashauri ya Msalala wakati wa makabidhiano ya mradi wa maendeleo ya jamii wa ADP Busangi uliotolewa na Shirika la World Vision Tanzania kwa ushirikiano na wananchi. Nkurlu alisema pamoja na mafanikio ya mradi huo, kwa sasa tayari utaratibu wote kupitia kamati za ulinzi na usalama za mji, Msalala na Ushetu zimekaa na kukubaliana kufanya msako shuleni ili kuwabaini wasichana watakao kuwa na mimba. “Baada ya kukubaliana kitakaochofuata ni kuwakamata na wale watakaobainika hatua kali zitachukuliwa, Serikali haiwezi kutumia fedha nyingi kwa ajili ya watoto kwenda shule lakini yanafanyika mambo kinyume na malengo,” alisema.

33 Ways to Monetize a Website (or a Blog) Affiliate marketing? Amazon? Google AdSense?

Image
Contact +255766605392.    Making money from your   website   isn’t a myth. It’s doable by everyone. In fact, turning a part-time, hobby blog into an income generating asset is fairly common with a bit of luck and some hard work. At the very least, you should be able to make enough to cover your basic  expenses for a domain  and  hosting . You might even be able to replace your income (and then some). Keep in mind that the strategies listed below range from easy and passive, to ones that require a TON of on-going work (so make sure you pick something that suits your site and lifestyle preferences). There are 33 total tips in this guide, but let’s start with the ten most popular (and predictable) site monetization tips. P.S.  It doesn’t matter whether you’ve started a blog  or  created a website . Those methods work for both. 10 Most Common Ways to Make Money with Your Website Making money from your website...

Second selection 2017/18

Image
Ingia hapa kuona majina yote share na wengine click majina