Posts

Kuendelea siasa za kupenda vita za Marekani katika Peninsula ya Korea

Image
Katika hali ambayo baadhi ya duru za habari zimearifu kupungua misimamo ya pande mbili kuhusiana na mgogoro wa Peninsula ya Korea, yaani Marekani na Korea Kaskazini, Washington imetuma meli yake ya kivita aina ya USS Ronald Reagan katika maji ya karibu na Korea Kaskazini. Kabla ya hapo pia Marekani ilituma meli ya USS Carl Vinson kwenda katika maji ya Peninsula ya Korea suala ambalo lilisababisha kuongezeka mvutano katika eneo hilo. Korea Kaskazini iliitaja hatua ya kutumwa meli hiyo katika maji ya eneo hilo kuwa ni sawa na kutangaza vita huku ikiionya vikali Washington kutokana na madhara makubwa yanayoweza kutokea kufuatia hatua hiyo ya kichokozi. Mbali na Pyongyang, Uchina pia ilikutaja kupenda vita kwa Washington katika eneo hilo kuwa kunatokana na siasa za kiuhasama za baharini ambapo ilimtaka Rais Donald Trump wa Marekani kuachana na mwenendo huo. Kiongozi wa Korea Kaskazini akikagua marubani wa kike Kwa kuzingatia indhari za mara kwa mara za Korea Kaskazin...

Kufanana kwa mofolojia na fonolojia

Image
                                                                                                                       Katika kujadili swali hili tutaanza kufasili dhana kuu zilizojitokeza ambazo ni fonolojia na mofolojia. Ambapo wataalamu mbalimbali wamefasili dhana hizi huku kila mmoja akitoa fasili yake. Pia tutatalii kwa kina juu ya kuhitilafiana na kufanana kwa fonolojia na mofolojia na mwisho n...

KUSIGANA NA KULANDANA KWA MSAMIATI

Tangaza biashara yako na masshele Blog +255766605392 KUFANANA NA KUTOFAUTIANA KWA LEKSIKOGRAFIA, LEKSIKOLOJIA NA LEKSIKONI. Katika kujadili mada hii tutaanza kufasili maana ya leksikografia, leksikolojia na leksikoni kisha tutajadili zaidi kuhusu tofauti zilizopo baina ya leksikografia, leksikolojia na leksikoni na mwishowe tutaweka hitimisho la mada yetu pamoja na marejeo. Wataalamu mbalimbali wametoa fasili ya Leksikografia kama vile Mdee (1985) anaeleza leksikografia ni usawiri wa kamusi, Huu ni utaalamu au utaratibu wa kukusanya msamiati pamoja na tafsiri yake na kuupanga katika kitabu cha maneno ambacho huitwa Kamusi. Fasili hii ya Mdee ina udhaifu kwani Kamusi siyo lazima iwe imeandikwa katika kitabu pekee, bali kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia siku hizi kamusi zimeweza kuandikwa katika elektroniki mfano kompyuta na simu za mkononi. Hali kadhalika Oxford dictionary (2001) Leksikografia ni kitendo cha kuunda kamusi. Hivyo basi...

CHIMBUKO - USHAIRI

Tangaza nasi au ikiwa una kazi yoyote ya kitaaluma na ungependa iwe hewani kupitia blog hii.         0766605392 CHIMBUKO LA USHAIRI Dhana ya ushairi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali huku kila mmoja akitoa fasili yake. Baadhi ya wataalam hao ni kama ifuatavyo: Mssamba, (2003) akimnukuu Shaban Robert, anasema; “ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi zaidi ya kuwa na sanaa ya vina ushairi unaufasaha wa maneno machache au muhtasari.” Mnyampala (1970) anasema kuwa “ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho kitu kilichobora sana maongozo ya Dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina maalum.” Amri Abeid (1954:1) anasema kuwa “ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki halina maana.” Encyclopedia American (EA) inaeleza kuwa ushairi ni kauli zenye hisia na ubunifu, mpangilio fulani wenye urari, uwasilishaji wa tajiriba au mawazo...