Posts

Showing posts from September, 2024

SIFA ZA KONSONANTI, UZIADA KANUNI ZA KIUSILIMISHO NA ZISIZO ZA KIUSILIMISHO

SIFA KUU ZA KONSONANTI Sifa hizi zinazingatia mambo makuu matatu 1.      Jinsi konsonanti zinzvyotamkwa 2.      Mahali ambapo konsonanti hutamkiwa 3.      Hali ya nyuzi sauti SIFA ZA JINSI YA MATAMSHI Katika sifa hii konsonanti hugawika katika makundi sita A.    VIPASUO/VIZUIWA Wakati wa utamkaji wa konsonanti hizi huwa kuna mzuio wa mkondohewa na kuachiwa ghafula. Konsonanti hizi zimepewa jina hilo kutokana na kwamba katioka kuachiwa ghafla kwa mkondohewa sauti itokeayo huwa kidogo kama ina mlio wa kupasua. Kwa mfano konsonanti /p/, /b/, /t/, /d/, /k/ na /g/. /p/  kipasuo sighuna cha midomo /b/ kipasuo ghuna cha midomo /t/ kipasuo sighuna cha ufizi /d/ kipasuo ghuna chaa ufizi /k/ kipasuo sighuna cha kaakaa laini /g/ kipasuo ghuna cha kaakaa laini B.     VIZUIO/VIPASUO KWAMIZA Konsonanti hizi zinapotamkwa hewa husukumwa nje kwa nguvu na kuzuiwa halafu nafasi ndogo huachwa ili hewa ipite ikiwa na mkwa...

MOFOLOJIA YA LUGHA KISWAHILI

Image
mofolojia ya lugha ya kiswahili Mofolojia-ni uwanja mdogo ndani ya isimu. Isimu-Ni taaluma inayochunguza lugha ya binadamu kisayansi. Mwanaisimu-ni mwanasayansi achunguzaye lugha ya binadamu katika nafasi zake zote yaani muundo, matumizi yake na nafasi yake katika jamii. Isimu ina nyanja na matawi yake. MATAWI YA ISIMU -Fonolojia -Sintaksia -Mofolojia -Isimu nadharia Nyanja za Isimu hushughulika na jinsi maneno yanavyoundwa. Mfano; mofolojia, fonolojia -Matawi ya Isimu huhusu mikabala ya kuchanganua taarifa mbalimbali za lugha. Mfano; Isimu nadharia huchunguza vipengele mbalimbali vya lugha. MATAWI YA ISIMU ISIMU NADHARIA -Taratibu zinazobuniwa kuwawezesha wachunguzaji fulani wa lugha kufuata taratibu fulani. ISIMU FAFANUZI -Hutoa uchunguzi wa sarufi za lugha na huhusu uchunguzi wa lugha na familia ya lugha fulani na historia ya lugha hiyo katika mazingira yaliyopo ISIMU HISTORIA -Huangalia jinsi lugha ilivyokua hapo awali. Hutumika kulinganisha lugha kulingana na jamii zake ukajua kam...