Posts

Showing posts from August, 2020

MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2020

Necta examination result s form six 2020 Bofya HAPA kuona majina yote

Wanachokiwaza wanaume juu ya mitindo ya nywele za wanawake

Image
Baadhi wamesema wanawake waachwe wafanye wanachokitaka licha ya kuona kuwa ni kiashiria cha kutokujiamini. Kwa wanaume, kuwa na nywele asilia ni kuukubali uzuri wako na kujiamini. Hata hivyo, hayo ni maoni binafsi kutoka kwa wadau. Dar es Salaam.  “Tangu niwe na mpenzi wangu, niseme ukweli tu kuwa sijawahi kuona nywele zake. Karibia kila wiki anakua na nywele mpya, leo rasta, kesho wigi, sijawahi kushika kichwa chake nikakutana na nywele zake, ” anasema Kennedy Bundala mkazi wa Morogoro. Katika mfululizo wa makala  zilizopita tulielezea mambo mbalimbali yanayohusu nywele asilia ikiwemo namna ya kuzitunza na madhara kwa wanaotengeneza nywele za dawa. Hata hivyo, ni mara chache sana kusikia hisia au kuwaona wanaume wakijadili masuala ya nywele za wanawake kwa kina. Je, wanaume wanawaza nini juu ya nywele za Wanawake ambao ni wake, wapenzi, mama na hata dada zao? Bundala, ambaye amekuwa na mpenzi wake kwa mwaka mmoja na nusu sasa bila mafanikio ya kuwahi kuziona ...

Msichana mwenye sifa hizi huwa hakiwii kuolewa

Image
     Kuolewa ni heshima kwa mwanamke. Heshima hiyo inaenda mbali zaidi hadi kuwagusa wazazi wa binti ambaye ataolewa. Wazazi wanatembea kifua mbele pindi binti yao anapoolewa, tena wanafurahia zaidi binti huyo anapoolewa akiwa angali bado hajazaa. Wanamshukuru Mungu kwa binti yao kujitunza. Wanamshukuru binti kwa kuwapa heshima katika familia yao na ndiyo maana siku ya sherehe ya kuagwa (send off) wazazi wanafurahi sana kuagana na binti yao kwa heshima. Hali hiyo huwa inaleta shauku kubwa kwa warembo wengi kutamani kuingia kwenye ndoa. Wengi wanaguswa na rekodi za wanawake wenzao ambao wamejitunza na hatimaye kuwaletea heshima wazazi wao. Kinyume chake, wengi wamejikuta wakijilaumu kwa kushindwa kuleta heshima katika familia zao. Binti umri unaenda, anatamani kuingia kwenye ndoa lakini hapati wa kumuoa. Au mwingine inatokea, anatamani kuolewa lakini anaishia kupigwa mimba na kuachwa. Badala ya kuleta heshima, analeta aibu katika familia yake kutokana na mila na desturi ze...

Matumizi ya lugha ya kiswahili

Matumizi ya lugha ya Kiswahili  ni kama ifuatavyo. 1. Kiswahili hutumika katika kufundishia shule za msingi isipokuwa lugha ya Kiingereza hufundishwa kama somo. 2. Kiswahili hutumika katika vyombo vya habari, mfano redio na runinga. 3. Kiswahili hutumika katika nyanja mbalimbali za kiserikali, mfano Mahakama ya mwanzo na ya kati. 4. Pia Kiswahili hutumika kama somo katika shule za sekondari hadi chuo kikuu. 5. Kiswahili hutumika katika shughuli za michezo mbalimbali. 6. Kiswahili hutumika katika nyumba za ibada kutolea mawaidha na mahubiri, mfano kanisani na msikitini. 7. Pia Kiswahili hutumika katika shughuli za kibiashara kama lugha ya mawasiliano miongoni mwa watu. 8. Kiswahili hutumika katika shughuli za kiofisi.

Ngeli za nomino katika lugha ya kiswahili

NGELI ZA NOMINO Ni namna ya kuweka majina katika makundi yanayofanana. Majina ya Kiswahili yanaweza kuwekwa katika makundi mbalimbali. Makundi hayo yamegawanywa na wanaisimu ya Kiswahili kwa kuzingatia maumbo ya alomofu za umoja na uwingi wa majina (kimofolojia) na kwa kuzingatia namna majina yanavyopatana na viambishi awali vya vitenzi (upatanisho wa kisarufi / kisintaksia). 1.      Kimofolojia: Katika kigezo hiki wanaisimu wameyapanga majina kulingana na alomofu za umoja na uwingi za majina hayo. Huu ni mtazamo mkongwe ambao uliofuatwa na wanasarufi wa kimapokeo wakiongozwa na Meinholf, Broomfield na Ashton mnamo miaka ya 1920 – 50. Uchambuzi ulikua kama ifuatavyo:- 1.      M- 2.      WA- i). Majina ya viumbe vyenye uhai ispokuwa mimea. Mfano; Mtoto – Watoto, Mzee – Wazee, Mkurya - Wakurya ii) Majina yanayotokana na vitenzi vinavyotaja watu. Mfano; Msomi – Wasomi, Mkulima – Wakulima, Mfanyakazi – Wafanyakazi. 3.     M- 4. ...

Dalili hatari kipindi cha ujauzito ambazo si za kupuuzia

Image
Hata kama umesoma sana na kuongea na wazazi mbalimbali kuhusu dalili mbali mbali kipindi cha ujauzito, bado itatokea baadhi ya wakati ambapo utakuwa huna uhakika kama unavyojisikia ni kawaida au la. Dalili zifuatazo ni muhimu kuzipa uzito wake na kuzifuatilia kwa makini. Kama ukizipata dalili hizi ni vyema kuwasiliana na mkunga, daktari wako au kituo cha kliniki ya wajawazito haraka iwezekanavyo. Nina maumivu tumbo la kati Maumivu makali au vichomi katikati au juu kidogo ya tumbo, ikiambatana na kchefuchefu na kutapika, inaweza kumaanisha kitu kimoja kati ya vifuatavyo. Unaweza ukawa na: Kuvimbiwa kulikopitiliza Kiungulia Tumbo kuchafuka Kama upo kwenye miezi mitatu hadi sita ya ujauzitowako, hii inawezza kumaanisha presha mimba ya awali. Hii ni dalili hatari na itahitaji matibabu ya haraka. Nina maumivu ya tumbo la chini Maumivu makali upande mmoja au pande zote kwenye tumbo lako la chini yanahitaji uchunguzi kugundua kama sio kitu cha kushtua. Kwa kiwan...