Posts

Showing posts from May, 2020

CORONA KUBADILI TARATIBU ZA WANACHUO UDSM :

Image
 Serikali ya wanafunzi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam imewataka wanafunzi wote wa UDSM watakapofungua chuo rasmi Jumatatu, Juni Mosi, kuhakikisha wanavaa barakoa (mask) muda wote wanapokuwa darasani na viunga vya chuo. Mbali na hilo, wanachuo hao pia wametakiwa kuhakikisha wanapowasili chuoni ni lazima watumie vitakasa. "Kila mwanafunzi utakapowasili chuoni utakutana na vitakasa mikono vya aina mbili vya kukanyaga kwa miguu na vya  automatic ukiweka mikono inatoa sabuni na maji. Kila mwanafunzi atatakiwa kunawa mikono kila anapotoka sehemu moja kwenda nyingine,hususani anapoingia darasani na kutoka nje. Kumbuka vitakasa mikono vitawekwa maeneo yote ya kuingilia na kutoka madarasani na sehemu zote za mikusanyiko." ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya kwa wanafunzi. Aidha kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa baada ya kikao kilichoshirikisha uongozi wa serikali ya wanachuo na Wizara ya Elimu, jana Jumanne, Mei 26 kikao hicho kimeafiki pia kupunguza muda wa masomo kutoka wiki...

MAGAZETI YA LEO 25/5/2020

Image
KWA HABARI

Mambo yatakayokusaidia uweze kubeba ujauzito

Image
Kuna sababu mbalimbali zinazoweza kumfanya mtu asishike mimba. Sababu hizo zinaweza zikawa zinamhusu mwanamke, mwanamume au wakati mwingine kutojulikana kabisa hali hiyo imesababishwa na nini. Wataalamu wanasema kwamba kwa miaka 20 iliyopita matatizo yanayohusu kushindwa kuzaa yameongezeka kwa kiwango kikubwa na asilimia 25 ya watu wanaotaka kubeba mimba na kuzaa mtoto wanakabiliwa na tatizo hilo. Ni kweli kuwa kwa kawaida watu wengi hubeba mimba na kujaaliwa mtoto pale tu wanapofanya tendo la ndoa. Lakini jambo hilo halitokeo kwa watu wote na ingawa kwa baadhi ya watu kila kitu huonekana kwenda sawa lakini pia hushindindwa kubeba mimba. Utafiti unaonyesha kwamba katika kila familia au 'couples' 5 zinazojamiiana katika wakati muafaka wa ovulation ni moja tu ndio hufanikiwa kupata mtoto, huku karibu wanawake 9 kati ya 10 wakifanikiwa kushika mimba baada ya kujaribu kutafuta mtoto kwa mwaka mmoja mzima bila kuzuia mimba. Hivyo basi nawaomba wale ambao wamekuwa wakifanya...