Posts

Showing posts from February, 2020

Binti fanya haya kumsaidia mpenzi wako kutimiza malengo yake

Image
Unaweza kufanya hivyo kwa kumkumbusha kuweka akiba na hata kwa kumuonyesha vipaji vyake asivyoviona. Kwa kumsaidia yeye, itakupatia amani pale utakapoona amefanikiwa huku ukiwa na mchango kwenye mafanikio yake. Ni kweli unapenda vitu vizuri lakini siyo mbaya ukajinyima kwa muda. Dar es Salaam.  Ni kwanini nimeamua kuandika makala hii? Ni swali nililojihoji hata mimi kabla sijaanza kuandika nilichoandika. Sababu kubwa ni hii "sasa mwanaume huna pesa mimi nakupeleka wapi?"  kauli hiyo imetoka kwa mwanadada mmoja aliyekuwa akiwasimulia wenzake juu ya hali ya mpenzi wake.  Hali hiyo ilinipatia mawazo ya mchango wa mwanamke katia kumsaidia mpenzi wake wanapokuwa kwenye mahusiano. Nimeongea na vijana wengi lakini jibu la Mike Goodwill limenivutia zaidi. Baada ya kumuuliza ni vipi anaweza kumridhisha mpenzi wake kiuchumi, alishika kichwa kana kwamba ameona Israeli anamfuata. "Acha tu kaka, kuna muda mwingine ninakuwa sina pesa alafu shemeji yako naye anakupig...

Masimulizi ya Alfu Lela u lela- Kitabu cha Alfu Lela U Lela au Usiku Elfu na Moja (كتاب ألف ليلة وليلة

Image
Kitabu cha Alfu Lela U Lela  au Usiku Elfu na Moja (كتاب ألف ليلة وليلة kwa  Kiarabu  au هزار و یک شب kwa  Kiajemi ) ni mkusanyiko wa fasihi katika muundo wa visa kutoka Mashariki ya Kati. Alfu Lela u Lela kwa maandishi ya Kiarabu Maandishi na historia yake Visa hivi vinatokana na kitabu cha zamani cha Kiajemi kiitwacho  Hazâr Afsâna  (Visa vya Ngano Elfu Moja). Inaaminika kuwa mtu aliyekusanya visa hivi na kutafsiri kwa  Kiarabu  ni  mtambaji hadithi  maarufu  Abu abd-Allah Muhammed el-Gahshigar  katika  karne  ya 14. Tafsiri ya kwanza ya Kiarabu ya kisasa ilichapwa  Cairo ,  Misri  mwaka  1835 . Inasadikika kuwa visa hivi vilianza kukusanywa wakati  Baghdad  ilipokuwa kitovu cha biashara na siasa  Mashariki ya Kati . Wafanyabiashara toka  Uajemi  ( Persia ),  China ,  India ,  Afrika , na  Ulaya  walikuwa wakitembelea Baghdad...

VIDEO | Diamond Platnumz – Jeje

Image
Diamond Platnumz – Jeje Video Shot & Directed By Director Kenny Under Zoom Extra

VISABABISHI VYA GANZI

Image
Mara nyingi ganzi hutokea endapo kuna michomo au mgandamizo wa mshipa wa fahamu. Magonjwa aina Fulani kama  kisukari  huweza kuharibu mishipa mirefu ya fahamu mwilini kama inayopeleka hisia kwenye mikono na miguu na pia huweza kusababisha miguu kupata ganzi. ​ Mara nyingi ganzi hutokea kwenye maeneo yaliyo mbali kutoka katikati ya mwili, mfano mikono na miguu. Unapopata ganzi mara nyingi haimaanishi kuwa unashida kubwa ndani ya mwili wako kama vile  kiharusi  au  saratani. ​ Mara utakapofika hospitali daktari atachukua historia ya tatizo lako ili kujua kisababishi ni nini pamoja na kufanyiwa vipimo vya utambuzi kulingana na historia yako na shida anayohisi kwa asilimia nyingi kwamba utakuwa nayo. ​ Baadhi ya visababishi vinavyofahamika kuleta tatizo la ganzi ni pamoja na; ​ Magonjwa kwenye ubongo na mishipa ya fahamu yake mfano; Neuroma ya akaustik Anurismu ya ubongo(kuvimba kwa mishipa ya damu ya ubongo) Fistula kati ya mshipa...

Fursa lukuki kwa vijana kilimo cha “stroberi” Tanzania

Image
Vijana wenye changamoto za ajira watakia kuchangamkia ili kupata kipato.  Wataalamu wa kilimo cha matunda hayo wamesema mahitaji na soko ni la uhakika. Mbali na faida za kiuchumi, stroberi zina manufaa mengi kiafya. Dar es Salaam.  “Nyumbani wana shamba ambalo hawalitumii. Niliomba nianze kufanya heka heka zangu kwani nilikua nimechoka kukaa nyumbani bila kusahau uchovu wa kuzunguka maofisini kutafuta kazi pasipo mafanikio,” anaeleza Tekla Buyamba ambaye ameamua kuingia katika kilimo cha matunda ya stroberi kukabiliana na tatizo la kukosa ajira.  Tekla anasema amejiajiri katika kilimo cha zao hilo la fukasidi (strawberry) ili kujipatia kipato kwa ajili ya kuendesha maisha yake. Fukasidi hustawi katika maeneo yenye joto la wastani, na hukua kwa haraka zaidi na uzalishaji kuongezeka linapolimwa kisasa zaidi ambapo hulimwa katika mikoa ya Morogoro, Mbeya, Iringa, Arusha, Kilimanjaro na kwa sehemu mkoani Pwani. Matunda ya  stroberi   yana matumizi m...