Posts

Showing posts from April, 2019

Silaha za ushindi zinazoweza kuwasaidia wanafunzi kidato cha sita 2019

Image
Mwanafunzi ajiandae kiisaikolojia kwa kujenga fikra za kujiamini na kuhakikisha afya ya akili na mwili iko sawa kuukabili mtihani.  Walimu wana wajibu wa kuwaandaa vema wanafunzi kwa kuwafundisha mbinu za kufaulu mtihani. Tathmini ya muda uliobaki kabla ya kufanya mtihani ifanyike ili kutoa kipaumbele kusoma notsi chache na masomo unayoyaelewa zaidi.  Dar es Salaam. Kufeli sio jambo la kufurahisha kwa mtu yeyote iwe kimasomo au maisha. Hata kwa wanafunzi waliopo shuleni ambao wanategemea kutimiza ndoto zao kuelimika na kupata taaluma watakazozitumia kuendeleza maisha, kufeli ni moja ya masuala hawaombei wakumbane nayo.  Lakini kufeli kunaweza kuepukwa ikiwa mwanafunzi amejiandaa vizuri kuukabili mtihani. Kufaulu mtihani kunategemea pia mbinu mbalimbali ambazo zikitumika vizuri zinaweza kumtoa mwanafunzi kimasomo. Wadau wa elimu wakiwemo wanasaikolojia na wahadhiri wa vyuo vikuu wameweka wazi mbinu wanazoweza kutumia watahiniwa wa kidato cha sita ambao wan...

KUNA WAKATI MAPENZI YANAFIKA MWISHO , USILAZIMISHE!

Image
NIANZE kwa kumshukuru Mungu kwa kunijalia kuiona siku hii ya leo nikiwa mzima wa afya. Ni matumaini yangu kwamba na wewe msomaji wangu uko poa kabisa, karibu kwenye ukurasa huu tubadilishane mawazo na kujadili mambo mbalimbali yanayohusu uhusiano wa kimapenzi.   Leo nataka kuzungumza na watu ambao wamefikia mwisho wa safari yao ya kimapenzi lakini hawataki kukubaliana na ukweli. Hakuna mtu anayemshauri mtu kuachana na mwenzi wake wala hakuna anayependa kuachana na mwenzi wake waliyeishi pamoja kwa muda mrefu lakini kuna hatua inafika, unakosa njia nyingine zaidi ya kumuacha aende. Imewahi kukutokea kwamba licha ya kuwahi kumpenda au kupendana na mtu fulani, imefika hatua mambo yote hayawezi kuendelea tena, moyo umekinai, hisia zimekufa na jambo pekee unalotaka litokee ni wewe na mwenzi wako kuachana? Kwamba huamini kama kuna jambo lolote linaloweza kuwafanya mkaendelea kukaa pamoja tena, dunia yenu ya mapenzi imefika mwisho na hakuna tena cha ziada! Mnapofikia hatua hi...

Ajira zaidi ya milioni 2 zinawasubiri wasichana wanaosoma masomo ya sayansi

Image
Inakadiria kuwa katika kipindi cha miaka 10 ijayo kutakuwa na ajira zaidi ya milioni 2 za teknolojia ambazo hazitajazwa kwa sababu ya ukosefu wa wataalam wa digitali. Changamoto hiyo inafungua mlango kwa wasichana duniani kufaidika na fursa hiyo kwa kuongeza kasi ya kusoma masomo ya sayansi. Baadhi ya wasichana wa Tanzania wameanza kuchangamkia fursa hizo kwa kubuni mifumo ya utatuzi ya kidijitali. Dar es Salaam.  Huenda wanafunzi wa kike wanaosoma masomo ya sayansi katika shule za sekondari na vyuo vikuu wakaboresha maisha yao, baada ya kubainika kuwepo kwa pengo la wataalam wa dijitali duniani.  Kwa mujibu wa Muungano wa Kimataifa wa Mawasiliano (ITU) unakadiria kuwa katika kipindi cha miaka 10 ijayo kutakuwa na  ajira zaidi ya 2 milioni za teknolojia  ambazo hazitajazwa kwa sababu ya ukosefu wa wataalam wa digitali. ITU inasema changamoto za ajira zinafungua mlango kwa wasichana duniani kufaidika na fursa hiyo kwa kuongeza kasi ya kusoma masomo ya...

UDSM yatakiwa kuongeza kasi utoaji haki miliki kwa wavumbuzi

Image
Sera ya umiliki wa Mali-Akili ya mwaka 2008 inataka Chuo Kikuu kupata kinga ya kisheria katika kutangaza na kuuza kibiashara bidhaa zinazohusiana na Mali-Akili kadri itakavyokuwa inafaa kwa maslahi ya Chuo, mtafiti na umma kwa jumla. Picha|Mtandao. Hatua hiyo inakuja baada ya CAG kubaini kuwa kuna usimamizi na utangazaji duni wa Mali-Akili chuoni hapo. Tangu mwaka 1981 hadi Januari 2018 Chuo kiliweza kutengeneza mashine 66, lakini uvumbuzi mmoja tu ndiyo ulikuwa na haki miliki. Imeshauriwa kutengeneza mifumo imara ya kuchunguza vumbuzi zinazokidhi kupata haki miliki na kufikiria kutoa motisha kwa wavumbuzi bora. Dar es Salaam.  Wakati watanzania wakiungana na wenzao duniani kuadhimisha Siku ya Mali-Akili Duniani ( World Intellectual Property Day ), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kimetakiwa kutengeneza mfumo mzuri wa usimamizi na kuendeleza vumbuzi mbalimbali zenye sifa ya kupata haki miliki.  Siku ya Mali-Akili Duniani huadhimisha Aprili 26 ya kila mwaka...

Advance your career with the Google Africa Certifications Scholarships

Image
Posted by William Florance, Global Head, Developer Training Programs Building upon our pledge to provide mobile developer training to 100,000 Africans to develop world class apps, today we are pleased to announce the next round of Google Africa Certification Scholarships aimed at helping developers become certified on Google’s Android, Web, and Cloud technologies. This year, we are offering 30,000 additional scholarship opportunities and 1,000 grants for the Google  Associate Android Developer ,  Mobile Web Specialist , and  Associate Cloud Engineer  certifications. The scholarship program will be delivered by our partners,  Pluralsight  and  Andela , through an intensive learning curriculum designed to prepare motivated learners for entry-level and intermediate roles as software developers. Interested students in Africa can learn more about the Google Africa Certifications Scholarships and apply  here According to...

TFF KUAMUA TIMU ITAKAYOCHEZA NA SEVILLA KATI YA SIMBA NA YANGA

Image
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), ndilo litakaloamua nani akipige na moja ya timu vigogo kutoka nchini Hispania. Sevilla moja ya timu inayojulikana kwa bora wa soka barani Ulaya na ubebaji wa kombe la Europa League, itakuja nchini mwezi ujao kucheza mchezo mmoja wa kirafiki. Awali, Kampuni ya Michezo ya Kubeti ya SportPesa inayoileta timu hiyo, iliamua Yanga na Simba zicheze mechi na mshindi acheze dhidi ya Sevilla. Hata hivyo, ilielezwa ratiba ya Ligi Kuu Bara inayokwenda ukingoni inaonekana kuwa imebana sana. “Kutokana na hali hiyo, tumeambiwa SportPesa wameamua kuwaachia TFF waamue kuhusiana na suala la timu ipi itacheza na Sevilla. “SportPesa walitaka Yanga na Simba washindane, mshindi basi angepata nafasi hiyo ambayo ni sehemu ya bahati kubwa kucheza na moja ya timu bora duniani. “Lakini sasa TFF nao wamekubaliana na SportPesa kwamba ratiba imebana, hivyo wameachiwa wao ndio wataamua kama nilivyokudokeza,” kilieleza chanzo. Sevilla mi moja ya timu zinazotoa ushindani kwenye La...

UHAKIKI TAMTHILIYA YA ORODHA pdf

Image
Jina la kitabu: ORODHA Mwandishi: Steve Reynolds Mwaka: 2006 Mhakiki: Mwalimu Makoba Tamthiliya hii ya Orodha inahusu suala zima la UKIMWI na athari zake katika jamii. Mhusika mkuu Furaha na wahusika wengine, wametumiwa kuonesha athari za gonjwa hili lakini pia mbinu za kupamban na UKIMWI, zimechorwa vyema. JINA LA KITABU Jina hili (ORODHA) linasadifu yaliyomo. Mhusika Furaha anaandika orodha ya kusomwa kwa sauti wakati wa mazishi yake ambayo jamii ya kijiji inaamini inafichua majina ya watu waliomwambukiza virusi vya UKIMWI. Orodha inayotolewa na mhusika furaha ambayo aliomba isomwe katika mazishi yake ni, uwazi, ukweli, uadilifu, uelewa, upendo, elimu, uwajibikaji na msamaha. MAUDHUI Maudhui ni jumla ya mawazo yote yanayozungumzwa katika kazi za fasihi, pamoja na mtazamo wa mwandishi juu ya mawazo hayo. Vipengele vya maudhui ni pamoja na , dhamira, migogoro, falsafa, ujumbe na msimamo. DHAMIRA i.  Athari na mapambano dhidi ya gonjwa la UKIMWI...