Posts

Showing posts from August, 2018

AINA ZA BAHARI YA USHAIRI WA KISWAHILI

Image
Na E. MASHELE  +255766605392 BAHARI ZA MASHAIRI Utenzi  Utendi Ndiyo mashairi marefu katika shairi, huwa na kina aghalabu huzungumzia maswala ya kihistoria , mashujaa ,mapenzi na mengineyo. Huwa na kipande kimoja tu. Idadi ya mizani katika kila mshororo huwa kati ya mizani nne na kumi na mbili .kina cha mshororo wa mwisho aghalabu huwa kilele katika beti zote nacho huitwa   kina bahari        Mfano Nakuita hima janabi, Njoo katika ukumbi, Unipeyo rambi rambi, Ya hiki changu kili o , Kilio changu muhubiri, Nataka kukukatibu, Kiwe katika vitabu, Pamo na msaada o , Mifano ya utenzi Utenzi wa fumo liyongo           utenzi wa uhuru wa Kenya  Msuko Ni shairi lenye kibwagizo kifupi. Mfano  i Mwajiona asumini, nanyi mmebahatika, Na waridi vitaruni,mwahisi hamna shaka, Pia viluwanmitini, nanyi mmeburudika, Mtahizika! Mf...

HIZI NDIZO FAIDA ZA VIAMBATA VYA OMEGA 3 NA OMEGA 6 VILIVYOMO KWENYE BLUE BAND MPYA

Image
Wengi wetu tumefanikiwa kuliona Tangazo jipya la Kampuni ya siagi inayofahamika kama BLUE BAND kwenye chanel mbali mbali za TV.Katika Tangazo hilo linaelezea kua BLUE BAND mpya ina Viambata vya OMEGA 3 NA OMEGA 6.Bila shaka watu wengi wamekuwa wakijiuliza Omega 3 ni nini na Omega 6 ni nini,Bila shaka na wewe unayeisoma makala hii ni mmojawapo wa watu wanaojiuliza viambata hivi ni nini. Basi leo nitakuelezea kwa undan nini maana ya viambata hivi na vina umuhimu gani katika afya yako. OMEGA 3 NA OMEGA 6 NI NINI? Omega 3 Hizi ni aina ya Fats(Mafuta) ambazo mwili hauwezi kujitengenezea bali mwili unategemea aina hii ya virutubisho kutoka katika vyakula. Virutubisho hivi vinasaidia utendaji kazi wa Cells zote za mwili,Virutubisho hivi vinasaidia kutengeneza Hormones ambazo zinasaidia kuganda kwa damu pindi unapopata majeraha,Zinasaidia kutanuka na kusinyaa kwa mishipa ya damu hivyo kusaidia kuimarisha mzunguko wa damu. Omega 3 pia inasaidia kuukinga mwili na matatizo ya moyo(heart ...

Wanawake Wanne Wauawa Na Kunyofolewa Nyeti Jijini Mwanza

Image
SIKU moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela, kuwaagiza wakuu wa wilaya za Kwimba na Misungwi kupambana na vitendo vya ubakaji na mauaji, wanawake wanne wamekutwa wameuawa kikatili kisha miili yao kunyofolewa nyeti. Miili ya wanawake hao ilipatikana jana ndani ya Shamba la Mifugo la Mabuki, huku ikiwa na dalili za kunyongwa. Mbali ya kupatikana kwa maiti hizo, pia kwenye eneo la tukio kulikutwa mafuvu mawili ya binadamu. Kupatikana kwa maiti hizo kunafanya idadi ya wanawake waliouawa wilayani Misungwi kufikia wanane. Juni 11, mwaka huu, wanawake wengine wanne waliuawa kikatili na watu wasiojulikana ndani ya pori hilo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema miili ya wanawake hao imeshatambuliwa, hivyo akawataka wananchi kutoingia porini kukata kuni wakati Jeshi hilo likiendelea na uchunguzi wa mauaji hayo. Alitoa mwongozo kwamba, katika hatua ya dharura wawepo askari ndani ya shamba hilo kwa ajili ya kufanya doria za kila mara, ikiw...

AJIRA MPYA ZA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI, JULAI, 2018

Image
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AJIRA YA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI JULAI, 2018 Ofisi ya Rais – TAMISEMI inapenda kuutarifu Umma kuwa, jumla ya Walimu 4,840 wamepangiwa vituo vya kazi kwenye Shule mbalimbali za Msingi na baadhi kwenye Shule za Sekondari nchini. Walimu hao waliopangiwa vituo vya kazi wanatakiwa kuripoti katika Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri zilipo shule walizopangiwa na baadaye kuripoti kwenye Shule walizopangiwa. Walimu wote wanatakiwa kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi kuanzia tarehe  23 Julai, 2018  hadi tarehe  7 Agosti, 2018  wakiwa na mahitaji yafuatayo: Vyeti halisi vya taaluma vya Kidato cha Nne na/au Kidato cha Sita; Vyeti halisi vya kitaaluma vya mafunzo ya Ualimu katika ngazi husika; na Cheti halisi cha kuzaliwa. Walimu wote waliopangiwa vituo vya kazi wanaelekezwa kuwa: Vituo vyao vya kazi ni Shule ya Msingi au Sekondari alizopangiwa na sio Makao Makuu ya Halmashauri; Mwajiriwa atakayeripoti na kuchukua posho ya ...