Posts

Showing posts from November, 2017

Viongozi wakubaliana Wahamiaji kuondolewa kwa dharura Libya

Image
Viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya na wa nchi za Umoja wa Afrika wanaokutana katika mkutano wa kilele nchini Ivory Coast wamekubaliana kuhusu mpango wa kuondoa nchini Libya wahamiaji wanaokabiliwa na mateso. Uamuzi huo ulichukuliwa baada ya Rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara katika mkutano wa tano wa kilele wa viongozi wa nchi za Umoja wa Ulaya na wa nchi za Umoja wa Afrika kutoa wito wa hatua za dharura kuchukuliwa kukomesha biashara ya utumwa na mateso mengine dhidi ya wahamiaji yanayoendela Libya. Rais Ouattara amesema jumuiya ya kimataifa inapaswa kufanya kila liwezekanalo kukomesha madhila wanayopitia wahamiaji. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliyeongoza kikao cha dharura pembezoni mwa mkutano huo kujadili suala hilo la biashara ya utumwa Libya, amesema viongozi wa Libya, Ujerumani, Chad, Niger, Ufaransa pamoja na nchi nyingine nne na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika wameamua kuanzisha operesheni ya dharura kuwaondoa wahamiaji ha...

UTANDO MWEUPE KINYWANI MWA MTOTO(THRUSH IN BABIES)

Image
Utandu mweupe(oral thrush) unakuwa kama maziwa kwenye kinywa cha mtoto ni infection inasababishwa na fungus wanaoitwa candida albicans. Utandu(thrush) huo unamwadhiri mtoto sehemu ya ulimi ,kuta za mashavu kwa ndani na ufizi  linawapata haswa watoto wachanga waliotoka kuzaliwa mpaka miezi 2-4,pia inawapata watoto wakubwa na watu wazima pia. Sababu ya mtoto kupata utandu kinywani ni nini? Candida fungus wanapoongeka kuwa wengi mwilini ndio wanasababisha mtoto kupata utandu kinywaji.candida fungus nao wanasababisha na haya matatizo ndio wanakuja kuzalishwa wengi kwenye mwili wa mtoto Hana kinga ya kutosha mwilini na bado inajitengeneza ndio hapo inakuwa rahisi kwake kupata infection. Mama alivyokuwa mjamzito  au mtoto anapotumia dawa za antibiotic anapunguza kinga ya mwili ndio mana inakuwa rahisi kushambuliwa. Mtoto akitumia antibiotic inasababisha kupunguza kinga wa bacteria Mama anaenyonyesha nae akitumia antibiotic inachangia mtoto kupata utando...

TATIZO LA MWANAMKE KUKOSA HAMU YA KUFANYA MAPENZI

Image
Tatizo la kukosa hamu ya kufanya mapenzi au kukosa nyege kwa lugha ya mitaani huwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume lakini ni wanaume wanaokerwa zaidi na tatizo hili kulio wanawake. Wakati ambapo ni asilimia 15 hadi 16 ya wanaume wenye tatizo hili, idadi ya wanawake ni mara mbili ya hii ya wanaume. Lakini wakati ni asilimia 23 ya wanaume wanaonyesha kuridhika kuishi na tatizo hili, asilimia 46 ya wanawake wapo radhi kabisa kuendelea kuishi na tatizo hili. Si lazima kuendelea kuishi na tatizo la kukosa hamu ya kufanya tendo la ndoa kwa sababu kuna mambo mengi unayoweza kuyafanya ili kuondokana na hili tatizo. Hali ya kupenda kufanya mapenzi au tendo la ndoa kwa mwanamke inabadilikabadilika sana ikipanda na kushuka kulingana na matukio mbalibali yanayomtokea katika maisha yake. Baadhi ya matukio yanayoathiri hamu ya mwanamke kufanya mapenzi ni pamoja na kuanza na kwisha kwa mahusiano ya kimapenzi na mwanamme, kupata ujauzito, na magonjwa. Kama...

BUHARI: RAIA WANIGERIA WANAUZWA KAMA MBUZI LIBYA

Image
Haki miliki ya picha REUTERS Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari amesema raia wote wa Nigeria ambao wamekwama Libya watarejeshwa nyumbani na kusaidiwa kurejelea maisha ya kawaida. Akizungumzia video za karibuni ambazo zimekuwa zikiwaonesha Waafrika wakiuzwa kwenye mnada wa watumwa nchini Libya, Rais Buhari amesema inasikitisha sana kwamba "baadhi ya raia wa Nigeria wanauzwa kama mbuzi - dola kadha Libya". Ameonekana pia kushangaa iwapo raia wa Libya walijifunza lolote la maana tangu kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011. ''Walichojifunza pekee ni kuwapiga watu risasi na kuua. Hawakujifunza kuwa mafundi wa umeme, mafundi wa mabomba au ufundi wowote ule," amesema. Kwenye video iliyotolewa na CNN mapema mwezi huu, vijana kutoka mataifa ya Afrika kusini mwa jangwa la Sahara walionekana wakiuzwa kama wafanyakazi wa mashambani kwa wanunuzi. Walikuwa wanauzwa $400 (£300) katika eneo ambalo halikufichuliwa Libya. Haki miliki ya picha AF...

NADHARIA MBALIMBALI KUHUSU HISTORIA YA KISWAHILI

               Kiswahili Asili Yake ni Kongo Baadhi ya wataalamu hudai kuwa asili ya lugha ya Kiswahili ni huko Kongo ambayo baadaye iliitwa Zaire na sasa inaitwa Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo. Dai hili linaimarishwa na wazo lingine linalodai kwamba katika vipindi kongwe vilivyopata kuwako, sehemu za Pwani ya Afrika mashariki hazikuwa zimekaliwa na watu. Kutokana na hali ya vita, uchungaji na biashara, inadaiwa kuwa Wabantu walitoka sehemu za Kongo walisambaa na kuja pwani ya Afrika mashariki kupitia Kigoma. Baadhi ya wabantu hawa walipitia sehemu za Uganda. Wakati wa kusambaa kwao, walieneza pia lugha zao ikiwemo hii ya Kiswahili. Udhaifu wa nadharia hii ni kwamba, madai ya kuwa asili ya Kiswahili ni Kongo hayana msingi kwani mpaka sasa wataalamu wanaodai hivi hawajaweza kueleza na kuthibitisha kisayansi ama Kihistoria juu ya lini hasa watu walianza kuishi pwani ya Afrika mashariki.    K...