AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Regina alizungumza huku akilisogelea friji moja na kulivuta nje, na kwakusaidiana na wezake, wakautoa mwili ambao hadi wanauweka chini nikabaki nikiwa ninashangaa kwani ni mwili wangu wote.
“Huyu ni wewe,  halisi baada ya kufa wakakuleta huku ila wamejisahau na kujua wewe upo hai”
Regina alizungumza huku akiugeuza mwili wangu, ambao hauna nguo hata moja, nikaliona jeraha la kisiki kilichokuwa kimenichoma mgongoni, kipindi mkia wa joka kubwa ulivyokuwa limenipiga na kunirusha juu na kukiangukia kisiki hicho
“Jile mwenyewe, sasa au unataka tukuwekee rost kama la wengine ulio wala?”

ENDELEA

Nikashusha pumzi nyingi huku nikimtazama, Regina na wezake anao fanana nao.
“Moja, mbili, ta…..”
“Ngoja kwanza Regina”
“Ehee unsemaje?”
“Ninakuomba umsaidie mke wangu, hapa nilipo sijielewi kabisa, tafadhali ninakuomba ndugu yangu”
Regina wote watatu wakaanza kucheka kwa dharau huku wakianza kunizunguka kwa kasi sehemu ambayo nimechuchumaa na mwili wangu, ninaoa ambiwa niule.Wakasimama gafla huku macho yao na sura zao zikianza kubadilika, macho yao yamejaa miale ya moto iliyo ambatana na machozi ya damu, huku sura zao zikianza kusinyaa na kuwa nyeusi tii kama mkaa.

“KULAAAA”
Regina mmoja alizungumza na kunifanya niitazame maiti ya mwili wangu, nikajikuta nikisimama kiujasiri huku nikiwatazama Regina wote watatu, nikamtazama aliye shika kichupa chenye dawa, wakendelea kunitazama kisha nikachuchumaa chuni, na kuishika miguu ya maiti yangu, nikaibana vizuri kwa viganja vyangu, kwa kutumia nguvu zangu zote nikainyanyua haraka na kuizungusha, ikawapiga kwenye miguu yao na wote wakaanguka chini, aliye shika kichupa chenye dawa akakiangushia karibu yangu.

Nikajirusha kwa haraka na kukiokota kichupa, na kuanza kukimbia kuelekea nje, kabla sijafika mlangoni nikastukia kumuona Regina mmoja akiwa amesimama mbele yangu.Huku sura yake ikiwa imekasirika sana, akajaribu kunirukia ila nikamkwepa na kunipa nafasi ya kutoka nikiwa ninakimbia kuelekea kwenye jingo alipo mke wangu Rahma.