AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
Akaingia kwenye moja ya chumba na mimi nikaingia pasipo kubisha hodi, gafla macho yangu yakakutana na Regina akiwa mtupu kama alivyo zaliwa huku mwili wake ukiwa umejaa maji, akionekana kutoka kuoga, nikatazama kila kona ya chumba na sikumuona binti ambaye nilikuwa ninamfatilia, Regina hakuonekana kushangaa wala hukuficha sehemu zake za siri, zaidi akabaki akiwa ametabamu na kuanza kupiga hatua za kunifwata, gafla nikastukia mlango ukifunguliwa nyuma yangu na nilipo geuka nikakutana na Rahma akiwa anatushangaa

ENDELEA
*Eddy ndio unafanya nini hapo?”
Rahma alizungumza huku akinitazama kwa hasira,
“Kwani wifi wewe, unatuona tunafanya nini?”
Regna alimuuliza swali Rahma, ambalo likazidi kumkasirisha Rahma
“Koma wewe, sijazungumza na wewe, nimemuuliza mume wangu”
“Ndio unijibu sasa, umetukuta tumesimama unababaika, ungenikuta nimemuweka kifuani mwangu si ndio ungekufa”
Regna alizungumza kwa dharau wala sikujua ujasiri kama huu ameutolea wapi, Rahma akanipiga kikumbo, nikastukia akimvaa Regna na kumuangusha chini, na kuanza kupigana, nikabaki nikiwa ninashangaa, sikujua hata nifanye kitu gani, Regna akamgeuza Rahma na kumkalia tumboni mwake, na kuanza kumtandika vibao vya mashavu, Rahma naye hakubaki nyuma, akajikakamua hadi akafanikiwa kumuweka Regna chini ambaye yupo uchi, na kuanza kunzaba makofi ya hasira.Nikamkimbilia Rahma na kumuwahi mikono yake, na kumchomoa mikononi mwa Regna

“Rahma, tulia mke wangu, mbona unataka kuleta aibu kwa wageni waliofika hapa”
Nilizungumza huku nikiendelea kumshikilia Rahma kwa nguvu
“Niache nimkomeshe huyo malaya wako”
Rahma alizungumza huku akijikakamua kutoka mikononi mwangu
“Malaya mwenyewe, hivi unadhani utaweza kuwa peke yako, na ninakuambia ni lazima nimchukue huyo mume wako, kwanza mwanamke mwenyewe huna kizazi, unadhani mume wako ataendelea kukaa na mwanamke tasa kama wewe? Uyooooo”
Maneno ya Regna yalizidi kunishangaza kwa maana si kawaida ya mtu anaye jitambua kuzungumza mambo kama hayo

“Eddy niachie, nimfundishe adabu huyu malaya, hawezi kunvunjia adabu ndani ya nyumba yangu”
“Rahma tulia, ninakuomba utulie mke wangu”
“Unamtetea huyo malaya wako eheee, niache sasa”
Nikastukia Rahma akinipiga kisukusuku cha tumbo na kujikuta nikimuachia, akamvamia Regna na kumuangusha chini, kwa haraka nikafunga mlango, kuepuka watu wa nje kusikia kitu kinacho endelea ndani ya chumba.Rahma akazishika nywele nyingi za Regna na kuanza kukibamiza kichwe chake kwenye kwenye sakavu yetu ya kisasa, Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kumuona damu zikiwa zinasambaa chini, zikitoea kwenye kichwa cha Regna.Kwa haraka nikavuta Rahma kwa nguvu zangu zote na kumzuia kuendelea kumpigiza Regna kichwa chake chini