Msanii wa muziki wa kizazi kipya ambaye alipata umaarufu kwa kupiga picha za utupu na kuweka mitandaoni, Amber Lulu, amesimulia historia ya maisha yake ambayo imemfanya abadilike na kuwa alivyo sasa.

Akizungumza kwenye Backstage ya Bongo Fleva Top 20 ya East Africa Radio, Amber Lulu amesema maisha yake ya nyuma yalikuwa yenye mahangaiko ya maisha akiwa na umri mdogo, huku akilazimika kujitafutia hadi pesa ya shule.

Amber Lulu amesema wakati yupo mdogo akisoma mama yake alikuwa na tatizo na lililomfanya ashindwe kutimiza majukumu mengi ya kifamilia, hivyo akaamua kujiingiza kwenye masuala mbali mbali ya kujitafutia riziki ili aweze gharama za kumudu maisha.