Shimo chumbani alimofukiwa marehemu
Mwanamke
aitwaye Salma Maulid mkazi wa Mtaa wa Mbilani Kata ya Kidongo Chekundu
Manispaa ya Tabora, ameuawa na mtu anayedaiwa kuwa ni mumewe kisha mwili
wake kufukiwa chumbani, chini ya uvungu wa kitanda.
Tayari
mwili wa marehemu umefukuliwa na Jeshi la Polisi limetangaza kumsaka
mtuhumiwa wa mauaji hayo, ambaye alitoweka kusikojulikana baada ya
kutekeleza tukio hilo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao chanzo cha mauaji hayo ni wivu wa kimapenzi.
Amesema mtuhumiwa baada yakutekeleza tukio hilo amekimbia.
0 Comments