Kikosi cha timu ya taifa ya Uganda 'Uganda The Cranes' jana kiliibuka na ushidi wa mabao 3-1 dhidi ya Sao Tome and Principle katika Uwanja wa Namboole Stadium nchini humo.

Katika mchezo huo uliokuwa wa kwanza kwa Kocha, Sebastiane Desabre, aliwaongoza vijana wake kupata ushindi wa kwanza huku mabao yakifungwa na Juuko Murushid anayeicheza klabu ya Simba, Joseph Ochaya, na Abraham Ndugwa.

Bao pekee la kufutia machozi kwa Sao Tome lilifungwa na Jose Varaela.

Wachezaji Emmanuel Okwi na Juuko Murushid walipata nafasi ya kuanza ndani ya kikosi hicho za Cranes.


25Mar2018