Nahodha wa Simba, John Bocco atafanyiwa vipimo leo asubuhi mjini Shinyanga ili kujua amepata maumivu kwa kiasi gani.

Hali hiyo inatokana na Bocco kuumia jana ikiwa ni dakika chache baada ya kuifungia Simba bao dhidi ya Mwadui FC kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Bocco alitolewa nje baada ya kushindwa kuendelea na kitengo cha tiba cha Simba, kimeeleza kwamba atafanyiwa vipimo hivyo ili kujua tatizo hilo kwa undani zaidi.


Baada ya ya vipimo hivyo, suala litakalofuatia ni matibabu ili kuhakikisha anarejea katika hali yake

                             TANGAZO