Dawa hii kwa jina jingine inajulikana kama sildenafil, imekua ikitumika sana kwa watu wenye matatizo ya nguvu za kiume.Dawa nyingine inayofanya kazi sawa na dawa hii ni Revatio.

*Inafanyaje kazi*
Dawa,hii hufanya kazi kwa kulainisha na kutanua mishipa ya damu hivyo kufanya damu nyingi kufika katika mishipa ya uume na kufanya uume kusimama,

Hupaswi kutumia dawa hii kama una tatzo la presha na unatumia dawa za presha.Kwani kutumia dawa hii wakati unatumia dawa ya presha inaweza kupelekea kushuka sana kwa presha hali inayoweza kupelekea kupoteza maisha.
Dawa hii hupelekea pia kupungua kwa mzunguko wa damu kwenye macho na kupelekea kushindwa kuona.

Pia hupaswi kutumia dawa hii ukiwa na matatizo yafatayo
Matatizo ya moyo
Matatizo ya figo
Matatizo ya Inni
Matatizo ya damu kama Ugonjwa wa seli Mundu( sickle cell) saratani ya damu(leukemia)
Vidonda vya tumbo
Tatizo la kupinda kwa uume(peyronies disease)

Vitu gani unapaswa kuepuka unapokua unameza dawa hii
Pombe,Kunywa pombe wakati umemeza dawa hii inaweza kuleta madhara ikiwemo kifo
Zabibu au bidhaa zilizotengenezwa na zabibu ni za kuepuka unapotumia dawa hii kwani zinaweza kuingiliana(drug interaction na kuleta madhara)

Madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi ya muda mrefu ni pamoja na upofu,kutosikia vizuri,vidonda vya tumbo,matatizo ya kifua.


DAWA HII HAITIBU MOJA KWA MOJA TATZO BALI INALIONDOA KWA MUDA UNAPOIMEZA INAPOISHA MWILINI BASI TATZO LINABAKIA PALE PALE.