TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI AFISA WA SHERIA DARAJA LA II - MDA's NA LGA's 13-06-2023


TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya MDAs & LGAs

anapenda kuwataarifu Waombaji kazi wote walioomba kazi kwa nafasi ya Afisa wa 

Sheria Daraja la Pili (Legal Officer II) kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa tarehe 14 -

15/06/2023 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili

huo.Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda na

sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.

ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask)

iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

iv. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha

Mpiga kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria.

v. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha

kuzaliwa,kidato cha IV, VI, Stashahada,Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea

kutegemeana na sifa za Mwombaji.

vi. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results,

hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips)

HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.

vii. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi.

viii. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.

ix. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na

kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)

x. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa

hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa

na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.

xi. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja

na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.

xii. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na

kunakili namba ya usaili kwa kuwa namba hizo hazitatolewa siku ya usaili

xiii. Wasailiwa wote mnajulishwa kuwa hali ya hewa ya Jiji la Dodoma ni baridi hivyo

mnashauriwa kuvaa nguo zinazohimili hali ya hewa ya ubaridi.

xiv. Msailiwa haruhusiwi kuja na simu au kifaa chochote cha kielekroniki kwenye eneo la

usaili

Pakua majina hapa chini

 Call For Interview

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?