MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI AJIRA MPYA 2023

 


 

Serikali imetengaza majina ya WALIOITWA KWENYE USAILI wa AJIRA mpya 2023 katika nafasi mbalimbali za AJIRA zilizotolewa mapema mwaka huu 2023.

SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

JA.9/259/01/A/312

04/06/2023

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Kituo cha Kimataifa 

cha Mikutano Arusha (AICC), Local Government Training Institute ( LGTI), Shirika la Elimu 

Kibaha (KEC), National Institute of Transport (NIT), OFISI YA WAZIRI, Tanzania Library 

Services Board ( TLSB), Tengeru Institute of Community Development (TICD), Taasisi ya 

Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI),, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (NAOT), Shirika la Reli Tanzania 

( TRC), Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania(TAA), Water Institute, Bodi ya Filamu 

Tanzania, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), MDAs & LGAs anapenda kuwataarifu 

Waombaji Kazi wote walioomba kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia tarehe 

2023-05-12 hadi 2023-06-19 na hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi 

watakaofaulu usaili huo.Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia 

maelekezo yafuatayo:-

i.

Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda 

na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.

ii.

Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa 

(Mask) iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

iv.

Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho 

cha Mpiga kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria.

v.

Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha 

kuzaliwa,kidato cha IV, VI, Stashahada,Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea 

kutegemeana na sifa za Mwombaji.

vi.

Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of 

results, hatiza matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) 

HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.

vii.

Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi. 

viii. 

Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.

ix.

Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na 

kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)

x.

Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue 

kuwa hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi 

zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.

xi.

Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa 

kuja na vyeti vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.

xii.

Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao 

na kunakili namba ya usaili kwa kuwa namba hizo hazitatolewa siku ya usaili

xiii.

Wasailiwa wote mnajulishwa kuwa hali ya hewa ya Jiji la Dodoma ni baridi hivyo 

mnashauriwa kuvaa nguo zinazohimili hali ya hewa ya ubaridi.

xiv.

Msailiwa haruhusiwi kuja na simu au kifaa chochote cha kielekroniki kwenye eneo 

la usaili.


Download full advertisement in PDF bellow

Call For Interview

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?