Afariki kwa Kudaiwa kulishwa saruji na askari wa JWTZ


Mkazi wa Kijiji cha Gumba, Kata ya Gwata wilayani Kibaha mkoani Pwani, Bakari Mbagara (63) amefariki dunia kwa kile kinachodaiwa kuwa alipigwa na waya wa umeme na kulazimishwa kula saruji na Askari wa JWTZ, Koplo Cibumba Lugola wa Kikosi cha 21 FIR Ngerengere.

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema wanaendelea kumshikilia mtuhumiwa wa mauaji hayo.

 

Uchunguzi wa polisi umeonesha kwamba Mbagara ambaye alifariki dunia Januari 2 na kuzikwa Januari 3 alifuatwa kwenye kilabu cha pombe na askari huyo akamchukua kwenda nae eneo analofanyia biashara, akimtuhumu kumuibia kuku wake.

 

Sahau Bakari ambaye ni mtoto wa marehemu amesema mtuhumiwa baada ya kumpiga baba yake, alimwachia na kumwamuru aondoke, na wakati akirudi nyumbani alianguka njiani.

Comments

Popular posts from this blog

HIZI HAPA SMS TAMU ZA KUMTAKIA USIKU MWEMA MPENZI WAKO

SMS na MESEJI 900+ za mapenzi

MIAKA 22 SASA TANGU KUZAMA KWA MELI KUBWA YA MV BUKOBA, TANZANI TUMEJIFUNZA NINI?