Muigizaji nguli nchini Tanzania, Amri Athuman maarufu kama Mzee Majuto amewasili nchini na kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Ny.0erere jijini Dar es Salaam akitokea nchini India alikokuwa amekwenda kwa ajili ya matibabu.

Mzee Majuto amewasili Airport leo Juni 22, 2018 majira saa 10 jioni na kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambapo atakua hapo kwa muda ili kukutana na wataalam kwa ajili ya uangalizi kukamilisha matibabu yake.