Kuna mti mmoja (jina lake linahifadhiwa ) unapatikana porini, mti huo ukikomaa, urefu wake hauzidi wa mtoto wa miaka saba, una magamba kwa mbali na rangi yake ni nyeupe

Mti huu ukikauka ukausaga unga wake huwa mweupe kama mti wenyewe.

Ukichukua unga wa mti huu halafu ukajipaka usoni unakuwa na uwezo wa kuwaona wachawi  na  misukule.

Ukijipaka unga wa mti huu usoni halafu ukatembea mtaani wakati wa mchana, unaweza kuona mambo yote yanayofanyika katika siri kubwa kama vile wachawi wakiwa wanawanga au wanafanya shughuli zao wakiwa uchi.

Mti huu unakufanya  pia  kuwa  na  uwezo  wa  kuwaona  misukule  na  kama  wewe  ni  mfanyabiashara ya  duka  basi  mti  huu  utakupa  uwezo  wa  kuwaona  watu  wanao  kuja  dukani kwako  na  hela  za  chuma  ulete.

Vilevile mti huu una uwezo wa kukimbiza nyoka mfano ukiwa na kipande cha mti huu mfukoni halafu ukawa unatembea, kama mbele yako kuna nyoka atakimbia kabla hujafika.

Pia  mti  huu hutumiwa  na  watu  wanao  fanya  shughuli ya  kutafuta  mali  zenye  asili  ya  kukaliwa, kushikiliwa,kulindwa  na  kufichwa  na  majini  wa  kisheitwani  kama  vile  madini  na  mali  mbalimbali.

Kwa ufupi  mti  huu  unakaliwa  na  majini ambao  kazi  yao  kuu  ni kufunua  mambo  yaliyowekwa  sirini  na  kufichua  mambo  yote  yaliyofichwa.

Kwa  hiyo  mtu  akichanjiwa  ama  kupakwa  uchawi  huu  anakuwa  na  uwezo  wa  kuona  mambo  yaliyo  fichwa na  kuwekwa  sirini.

MTI  MWEUPE  WA  KUONA  WACHAWI NA  ULOZI  KATIKA MAPENZI.
Mti mweupe  una  matumizi mengi  sana. Moja  kati  ya  matumizi  hayo  ni  pamoja  na  kutumika  katika  ulozi  wa  mapenzi.

Katika  ulozi  wa  mapenzi, mti  mweupe  hutumika  Zaidi  katika  uchawi  wa  mapenzi  ambao  hutupwa  kwa  njia  ya  kumtegea  mtu  kwenye  njia  anayo  itumia  kupita.

Kama  unataka  kumtega  mtu  ulozi  wa  mapenzi, basi  usiku  utachukua  huu  mti  mweupe  kiasi  utajipaka usoni, kiasi  utaufunga  kwenye  kitambaa  chekundu  na  kuweka  chini  ya  mto  ambao utaulalia  na  kiasi  utachoma  kwenye  koroboi  au  chetezo  huku  ukimnuizia  mtu  ulie  mkusudia  na  kuwaomba  majini  wanao husiana  na  mti  huu mweupe  wakufunulie  na  kukuonyesha  njia  ambayo  mtu  ulie  mkusudia  atapita kesho  yake  au  katika  siku  maalumu  ya  kinyota  ambayo  umepanga  kumtega  mtu  huyo  uchawi  huo  wa  mapenzi.

Usiku  wa  siku  hiyo utamuona  katika  ndoto  mtu  ulie mkusudia  akipita  katika  njia  ambayo  wewe unaifahamu.

Ikifika  kesho  yake  asubuhi  utatakiwa  kwenda  katika  njia  hiyo  na  kutega  dawa  nyingine  ya  ulozi  wa  mapenzi  ambayo  hutumika  kwa  kumtega  mtu  aruke ili  imnase. 

Na  mtu  huyo  akisharuka  katika  njia  hiyo  basi  dawa itamnasa  na  jinni wa  mapenzi  aliekusudiwa  atamuingia  mtu  huyo  na  kuamuru  kufanya  mambo  yote  ambayo mlogaji  alikusudia  kuyafanya.

Hivyo  ndivyo  mti  mweupe  wa  kuona  wachawi  unavyo  tumika  katika  ulozi  wa  mapenzi.

Mbali  na  kutumika  katika  ulozi  wa  mapenzi  mti  huu  unatumika  katika  mambo  mengine  mengi  sana  mazuri  kwa  mabaya.

Mambo  yote  hayo  utayapata  kuyafahamu  kupitia  kitabu  changu  ambacho  kitatoka  mwezi  wa  saba  kati  kati. Kitabu  hicho  kinaitwa : MAMBO  TISA  YANAYO  UNDA  NYOTA YA  MWANADAMU NA  UHUSIANO  KATI  YA  NYOTA  YA  MTU  NA  MAFANIKIO YAKE  KATIKA  MAISHA  ambacho  kimeandikwa  nami  DOKTA. MUNGWA  KABILI.

Ndani  ya  kitabu  hiki  utapata  kufahamu  kila  kitu kuhusu  mti mweupe, kuanzia  taratibu  za  kuuchukua  porini, siku  na  muda  unao  takiwa  kuuchukua  porini, maneno  unayo  takiwa  kuyatamka wakati  unauchukua  mti  huu  porini, masharti  ya  kutumia  mti  huu, jinsi  unavyo  weza  kujiepusha  na  shari  za  wachawi  na  walozi  zitokanazo  na  kuutumia  mti  huu  pamoja  na  matumizi  yote  ya  mti  huu  kuanzia  kujipaka, kuchanjiwa,kuchoma, kufukiza, kupuliza  pamoja  na  mambo  yoote  yanayo  husiana  na  mti  huu.


MAKALA  HAYA  YAMEANDALIWA  NA  DOKTA. MUNGWA  KABILI.  ANAPATIKANA KWA  SIMU  NAMBA  0744  000 473.