Akizungumza na wanabari leo Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo amesema Kamati ya Tuzo ya VPL imekamilisha orodha ya wachezaji 30 watakowania tuzo hiyo na kwamba mchakato wa kumpata mshindi unaanza rasmi.
Nyota waliopo katika orodha hiyo ni Habibu Kiyombo, Hamis Mcha, Yahya Zaid, Kelvin Yondani, Razack Abarola, Aggrey Morris, Himid Mao, Awesu Awesu, Adam Salamba, Mohamed Rashid, Shafiki Batambuze, Mudathir Yahya, Marcel Kaheza na Adam Salamba.
Wengine ni Eliud Ambokile, Shabani Nditi, Tafadzwa Kutinyu, Ibrahim Ajibu, Gadiel Michael, Papy Tshishimbi, Obrey Chirwa, Aishi Manula, Emanuel Okwi, John Bocco, Jonas Mkude, Erasto Nyoni, Shiza Kichuya, Asante Kwasi, Hassan Dilunga na Bruce Kangwa.