KWA WALIMU WOTE
Sikilizeni wimbo huu:
Nilipokuwa mtoto niliitwa Chacha
Kwa matamshi yangu ya sasa
Nilipokuwa kijana niliitwa Chaupele
Nilipokuwa mtu mzima niliitwa Manywele Nilipokuwa mwalimu nikaitwa Bure.
Huu utakuwa wimbo wako
Utakapostaafu urudipo nyumbani Umelewa kangara na nyayo zako
Zikishidwa kulenga njia nyembamba vijijini
Utakuwa kichekesho kwa watoto watakao kuita Ticha popote upitapo
Kumbuka mwalimu utakapostaafu.
Mijusi watataga mayai ndani ya viatu Vyako vilivyokwisha visigino
Na ndani ya sidiria chakavu Zilizoshikizwa kamba kwa pini. Mende watazaliana ndani ya chupa tupu
Za marashi na za bia
Na manyigu yatajenga ndani ya kofia Zilizosahaulika kutani.
Utakapokufa nge watazaliana
Chini ya jiwe juu ya kaburi lako, Na mlevi fulani akipita atapenga
Na kupangusa vidole kwenye jiwe pweke. Mwanzo na mwisho wako ndio huo
0 Comments