Mwanaume
mmoja nchini Nigeria mwenye umri wa miaka 42 anapambania kuokoa maisha
yake baada ya kuzikata sehemu zake za siri na kisu ndotoni, baada ya
kuota anachinja mbuzi kwa ajili ya kumsaidia mke wake kuandaa chakula
cha jioni.
Tukio
hilo limetokea Agosti 12, 2022, na kusema kwamba baadaye alikuja
kushtuka na kugundua kwamba alikuwa akizikata sehemu zake za siri badala
ya mbuzi kama alivyokuwa anaota.
Imeelezwa
kwamba mke wa mwanaume huyo hakuwepo nyumbani na ndipo alipopigiwa simu
na majirani zake kumuarifu kwamba mume wake amejeruhiwa na ndipo
alipowahi kurudi nyumbani na kumkuta amezishikilia sehemu zake za siri
na kisha kumpeleka hospitali.
0 Comments