massheleemanuel@gmail.com

By Glory mushy


FASIHI SIMULIZI YA KIAFRIKA
Fasihi Simulizi ni nini?
Wataalamu mbalimbali wametoa maoni yao kuhusu maana ya FS. Miongoni mwao ni Finnegan (1970), Matteru 1979), Balisidya (1983), Okpewho (1992) na wengineo wengi. Ili kuweza kubaini maana ya FS ni vema kudurusu fasili zilizotolewa na wataalamu hawa. Lengo hasa ni kutaka kufahamu ubora na udhaifu wa fasili zao, hatimaye tuweze kuunda fasili muafaka zaidi kuhusu maana ya FS.
F.S yaweza kuelezwa kwamba, hutegemea msanii ambaye huiumba kwa maneno katika tukio maalum (Finnegan, 1970)
Ni fasihi inayotegemea mdomo ktk kutolewa na kuenezwa kwake… (M.L.Matteru, 1979)
Ni aina ya fasihi ambayo hutumia mdomo katika kuumbwa, kuwasilishwa na kusambazwa kwa waasikilizaji na watumiaji waake (Balisidya, 1983)
F.S humaanisha fasihi itolewayo kwa neno la mdomo… (Okpewho, 1992)
F.S ni kazi ya sanaa inayotumia lugha kazi hii ya sanaa huhifadhiwa kwa kichwa na kusambazwa kwa njia ya masimulizi ya mdomo… (M.Msokile, 1992)
Ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia mdomo na vitendo bila kutumia maandishi (Mulokozi, 1996)
Neno F.S linamaanisha hadithi za jadi, nyimbo, mashairi, vitendawili na methali ambavyo hutolewa kwa neno la mdomo (Bukenya na Wenzake, 1997)
Sanaa hii iitwayo Fasihi, inaweza kuhifadhiwa kwa njia kuu mbili: kwa njia ya mdomo na kimaandishi. Aina ya kwanza, ambayo tunajihusisha nayo katika sehemu ya kwanza inajulikana kama F.S (Wamitila, 2003)
Ø Fasili hizi hazigusii lolote kuhusu matumizi ya nyenzo za sayansi na teknolojia katika kubuni, kutongoa na kuhifadhi sanaa husika. Nyenzo kama vile, Radio, Video, DVD, VCD, Televisheni, Kompyuta na Wavuti….. kwa sasa zinatumika katika kutolea na kurekodia tanzu za F.S kama vile hadithi……
Ø Katika F.S fanani na hadhira huwapo ana kwa ana: dhana ya kuwapo ana kwa ana pia inahitaji mjadala (uwezekano wa kuwa na aina mbalimbali za hadhira)
UAINISHAJI WA TANZU ZA FASIHI SIMULIZI
Utata umekuwa ukijitokeza katika uanishaji na ugawaji wa tanzu na vipera vya FS. Utata huu unatokea kutokana na kutofautiana kwa vigezo vinavyotumiwa na wataalamu mbalimbali katika ugawaji huu, kwani kila mtaalamu hutumia vigezo vyake kulingana na matakwa ama mtazamo wake. Hebu sasa tuwatazame baadhi ya wataalamu ambao wameainisha tanzu za FS, tukiangalia pia udhaifu na ubora wa vigezo walivyotumia
A M .L. BALISIDYA (MATTERU) (1987)
Anagawanya FS katika tanzu tatu ambazo ni NATHARI, USHAIRI na SEMI. Katika kila utanzu kuna vipera vyake mbavyo navyo vina vijipera pia. Uainishaji wake ni kama ifuatavyo:
(1)NATHARI
A. Ngano
· Istiara
· Hekaya
· Kwanini na kwa namna gani
· kharafa
B. Tarihi
· Kumbukumbu
· Shajara
· Hadithi za historia
· epiki
C. Visasili
· Kumbukumbu
· Tenzi
· Kwanini na kwa namna gani
(2)USHAIRI
A. Nyimbo
v Tahlili
v Bembea
v Tumbuizo
v Ngoma
v Mwiga
v Watoto
v kwaya
B. Maghani
v Majigambo
v Vijighani
v Shajara
v tenzi
(3)SEMI
A. Vitendawili
Ø Kitendawili
Ø Mizimu
Ø mafumbo
B. Methali
Ø Msemo
Ø nahau
C. Misimu
Ø Utani
Ø Masaguo
Ø soga
Upungufu wa uainishaji huu
Katika uainishaji wake, baadhi ya tanzu hazionekani ama tunaweza kusema zimeachwa kabisa. Mfano visakale, ngomezi,
Balisidya anauweka utenzi kuwa ni kipera cha visasili katika kundi la nathari. Hapa anaibua mjadala kwani kama tujuavyo kuwa utenzi katika FS huhusisha uimbaji pia. Hivyo swali la kujiuliza ni je utenzi ni nathari?
Vilevile kuna kuingiliana kwa tanzu. Mfano kumbukumbu na kwanini na kwa namna gani ni tanzu ambazo zinajitokeza katika kundi zaidi ya moja.
M. M MULOKOZI (1989)
Kwa upande wake Mulokozi anaainisha tanzu za FS katika makundi sita ambayo ni MAZUNGUMZO, MASIMULIZI, MAIGIZO, USHAIRI, SEMI, na NGOMEZI.
(1)MAZUNGUMZO
§ Hotuba
§ Malumbano ya watani
§ Ulumbi
§ Soga
§ mawaidha
(2)MASIMULIZI
a) Hadithi - Ngano (Istiara, Mbazi, Kisa)
b) Salua – kisakale, mapisi, tarihi, kumbukumbu, kisasili
(3) MAIGIZO (tanzu zake hutegemea na shabaha na miktadha)
(4)USHAIRI
a) Nyimbo
· Tumbuizo
· Bembea
· Za dini
· Wawe
· Tenzi
· Tendi
· Mbolezi
· Kimai
· Nyiso
· Za vita
· Za taifa
· Za watoto
· Za kazi
(b) Maghani (ya kawaida, ya sifo- kivugo na tondozi)
Ghani masimulizi – rara, ngano, sifo, tendi
(5)SEMI
§ methali
§ vitendawili
§ misimu
§ mafumbo
§ lakabu
(6)NGOMEZI
- Za taarifa
- Za tahadhali
- Za mahusiano k.m mapenzi
Kwa upande wake Okpewho anaeleza kuwa uainishaji wa hadithi/ngano ni tatizo la muda mrefu. Hata hivyo anaeleza kuwa kuna vigezo/njia nne mpaka sasa ambazo zimetumiwa kuainisha hadithi/ngano.
Kwanza, kigezo cha unguli (protagonist of the tale), katika kigezo hiki kunajitokeza ngano zihusuzo wanadamu, ngano za wanyama, ngano za vichimbakazi, na ngano za miungu. Hata hivyo kigezo hiki kinaonyesha kuwa na matatizo.
· Matatizo hayo ni pamoja na kufanana kitabia kati ya jamii moja na nyingine. Kwa mfano katika ngano za wanyama, wanyama hupewa uwezo wa kuzungumza, kufikiri, na kutenda kama wanadamu.
· Pia kigezo hiki kinapuuza namna mbalimbali katika ngano ambazo vichimbakazi, wanadamu na wanyama huhusiana.
Pili, kigezo cha lengo la ngano husika (purpose of the tale), katika kigezo hiki ngano zinaainishwa kwa kuzingatia lengo la simulizi husika. Hapa panajitokeza ngano za kimaadili, ngano za kuhimiza kazi n.k. Okpewho anaeleza kuwa katika kigezo hiki kundi kubwa la ngano ni zile za kimaadili.
Tatu, kigezo cha sifa ya ubora wa ngano (characteristic quality of the tale), kigezo ambacho ndicho kinaonekana kubeba kundi kubwa la ngano. Katika kigezo hiki kuna ngano ayari (trickster tales)-hizi huambatana na uelevu au ulaghai wa wahusika; ngano za mtanziko (dilemma tales) na ngano za kihistoria ambazo huhusu vita, vizazi, mashujaa, usuli wa kitu/jambo fulani n.k.
Nne ni Kigezo cha muktadha wa utendaji wa ngano husika. Katika kigezo hiki kinachoangaliwa ni ngano inatendwa wakati gani na katika mazingira gani. Kwa mfano, kwa kutumia kigezo hiki tunaweza kupata ngano zinazotendwa wakati wa mbalamwezi (moonlight tales), ngano zinazotendwa wakati wa ibada (divination tales), ngano zinazotendwa wakati wa mapumziko ya wawindaji (hunters’ tales) na nyinginezo.
Kwa ujumla vigezo hivyo vina matatizo kwa sababu kuna uwezakano wa aina moja ya ngano kujitokeza katika vigezo vyote. Kutokana na utata huo, Okpewho anazianisha ngano katika makundi yafuatayo:
Kundi la kwanza ni hekaya (legends). Kundi hili linaelezwa kuwa ndio kundi kubwa kabisa la hadithi na hujumuisha tarihi, ngano za mashujaa, ngano za mapenzi n.k.
Kundi la pili ni ngano fafanuzi (explanatory tales). Hizi hufafanua asili ya kitu au wazo kwa kuzingatia mazingira na tajiriba za jamii. Kundi hili linajumuisha aina mbili kubwa: (1) Ngano zinazoelezea asili ya kuumbwa kwa ulimwengu, (2) Ngano zinazosawiri sifa na tabia za viumbe mbalimbali katika mazingira yao. Aina hii ya pili hujumuisha visasili na visaviini.
Kundi la tatu ni ngano zisizo fafanuzi (fables). Kundi hili hujumuisha hadithi zinazohusu tajiriba zihusuzo wanyama, viongozi wa dini iwe katika ulimwengu au vinginevyo. Katika hadithi hizi msimulizi hatoi maelezo maalumu ni namna gani hadhira iifasili hadithi hiyo.
UFAFANUZI WA TANZU ZA FS NA VIPERA VYAKE
1. SIMULIZI/ HADITHI
Masimulizi ni fasihi yenye kusimulia habari fulani (narrate). Ni masimulizi ambayo yanatumia lugha ya mjazo au nathari na mtiririko wake huwa mwepesi au sahili. Urefu wa hadithi hutofautiana kutoka kitanzu/kipera kimoja hadi kingine. Kwa jumla zipo hadithi ambazo ni za kubuni na zingine za kihistoria. Baadhi ya vipera vya utanzu huu ni;
i. Ngano
Hizi ni hadithi za kimapokeo zitumiazo wahusika kama wanyama, miti na watu katika kuelezea au kuonya kuhusu maisha. Utanzu huu unajumuisha fani kadhaa kwa mfano:
Istiara – hadithi ambayo maana yake ya wazi inawakilisha maana nyingine iliyofichika. Yaani hadithi nzima ni kama sitiari.
Mbazi- hadithi fupi yenye mafunzo itolewayo kama kielelezo wakati wa maongezi au wa kumkanya mtu
Kisa- hadithi fupi ya kufurahisha kuhusu tukio la kweli.
ii. Visakale
Masimulizi ya mapokeo juu ya wahenga au mashujaa wa kabila au taifa yenye kuchanganya chuku na historia. Kwa mfano hadithi za Liyongo
iii. Mapisi
Maelezo ya historia bila kutia mambo ya kubuni.
iv. Soga
Ni hadithi ndogo ndogo zinazohusisha utani na ucheshi kwa kiasi fulani. Hizi ni hadithi ambazo hutambwa katika mtiririko wa matukio ambao huzua kicheko. Soga hudhamiria kuchekesha kwa kukejeli pia. (wamitila: 2010)
v. Tarihi
Hizi ni hadithi ambazo husimulia au zimejengwa kwenye matukio ya kihistoria. Inawezekana matukio yanayosimuliwa yakawa ya kweli, yaani yalipata kutokea kihistoria. Hadithi hizi hutokea zaidi katika maandishi, mfano ni tarihi ya Kilwa, tarihi ya Pate n.k.
vi. Visasili
Ni utanzu unaofungamana na imani za dini na mizungu (rituals) ya jamii. Hizi ni hadithi za kale zenye kuwakilisha imani na mtazamo wa jamii inayohusika kuhusu asili ya ulimwengu na mwenendo wake, kuhusu asili yao wenyewe, na maana na shabaha ya maisha yao. Mara nyingi hadithi hizi huaminiwa kuwa ni kweli tupu, na hutumika kuelezea au kuhalalisha baadhi ya mila na madhehebu ya jamii inayohusika.
2. SEMI
Semi ni tungo au kauli fupifupi za kisanaa zenye kubeba maana au mafunzo muhimu ya kijamii. Baadhi ya tanzu katika kundi hili ni;
I. Methali
Methali ni semi fupi fupi zenye kueleza kwa muhtasari fikra au mafunzo mazito yaliyotokana na uzoefu wa kijamii. Mara nyingi mawazo hayo huelezwa kwa kutumia tamathali hasa sitiari na mafumbo. Methali nyingi huwa na muundo wenye sehemu mbili. Sehemu ya kwanza huanzisha wazo Fulani, na sehemu ya pili hulikanusha au kulikaamilsha wazo hilo. Kwa mfano; haraka haraka haina Baraka, tama mbele mauti nyuma.
II. Vitendawili
Ni usemi uliofumbwa ambao hutolewa kwa hadhira ili iufumbue. Fumbo hilo kwa kawaida huwa linafahamika katika jamii hiyo, na mara nyingi lina mafunzo muhimu kwa washiriki, mbali na kuwachemsha bongo zao. Vitendawili ni sanaa inayotegemea uwezo wa mtu kutambua, kuhusisha na kulinganisha vitu vya aina mbalimbali vilivyomo katika maumbile.
III. Misimu
Ni semi za muda na mahali maalum ambazo huzuka na kutoweka kutegemea mazingira maalum. Msimu ukipataa mashiko ya kutosha katika jamii huweza hatimaye kuingia katika kundi la methali za jamii hiyo.
IV. Mafumbo
Ni semi za maonyo au mawaidha ambazo maana zake za ndani zimefichika. Fumbo hubuniwa na msemaji kwa shabaha na hadhira maalum, hivyo ni tofauti na methali au vitendawili ambavyo ni semi za kimapokeo.
V. Lakabu
Haya ni majina ya kupanga ambayo baadhi ya watu hupewa au hujipatia kutokana na sifa zao za kimwili, kinasaba, kitabia au kimatendo. Majina haya huwa ni maneno au mafungu yaa maneno yenye maana iliyofumbwa. Mara nyingi majna haya huwa ni sitiari. Baadhi ya majina haya humsifia mhusika, lakini mengine humkosoa au hata kumdhalilisha. Mifano ya lakabu;
Mukwavinyika – mtekaji wa nyika
Baba wa taifa – mwl Nyerere
Simba wa Yuda – Hile Selassie
Mkuki uwakao – Jomo Kenyatta.
UTENDAJI SIMULIZI
Usimulizi wa Hadithi katika Afrika
Okpewho anajadili usimulizi wa hadithi katika Afrika. Anaeleza kuwa msimulizi wa kijadi ni tofauti na msimulizi anayepatikana katika maandishi. Usimulizi katika Afrika unafanyika wakati maalumu hasa wakati wa jioni au usiku watu wanapokuwa katika mapumziko baada ya vipindi maalumu vya kazi.
Usimulizi wa hadithi katika Afrika hufuata fomula maalumu. Usimulizi wa hadithi hizi huwa na mianzo na miisho ya kifomula ingawa mianzo na miisho hiyo hutofautiana toka jamii moja hadi nyingine. Kwa mfano matumizi ya paukwa pakawa, hadithi hadithi n k kutegemeana na utanzu husika.
Pia usimulizi wa hadithi unaambatana na ushiriki wa hadhira ambaye huonyesha kuwa anafuatilia simulizi hiyo.
Kwa jumla, utambaji wa hadithi jukwaani huwa na sifa kadhaa zinazoutambulisha. Sifa hizi huzitenga hadithi za mapokeo na zile tunazozisoma vitabuni. Utendaji huu unaandamana na sifa zifuatazo;
Usemi halisi. msemaji anasema moja kwa moja
Michepuko: msimuliaji hutoa kauli za pembeni au maoni yake. Anaiacha hadithi na kusema mambo ya pembeni au kando kabla ya kuendelea tena kuisimulia. Michepuko hii inaweza kuwa na jukumu la viliwazo hasa katika hadithi za kusikitisha au za kitanzia.
Urudiaji
Matumizi ya wakati uliopo kihistoria/ au uliopita kisimulizi. Utambaji au usimulizi huwa katika wakati uliopita lakini huchanganya pia na sifa zinazohusishwa na wakati uliopo ili kuhakikisha kuwa umbali uliopo kati ya hadhira na hadithi yenyewe umepunguzwa.
Kubadilisha muundo wa hadithi: mtambaji anauwezo wa kuubadilisha muundo wa hadithi kwa kuongeza vitushi fulani, kurudia visa fulani, kubadilisha msamiati, kurahisisha kisa, kutia ucheshi n.k. Kwa hakika kila utambaji hadithi moja huwa ni tofauti na utambaji wa hadithi hiyo wa mwanzoni yaani inafaraguliwa.

NADHARIA ZA FASIHI SIMULIZI
Nadharia huchukuliwa kuwa dira ya kumwongoza mtafiti au mchambuzi kulikabili na kulielezea vyema jambo fulani kwa tazamao unaotazamiwa kuwa imara zaidi kuliko ule wa nadharia nyingine. Nadharia hutoa mwongozo katika utatuzi wa jambo fulani ambalo halijaweza kuhakikishwa ukweli wake. Ni mawazo, maelezo au mwongozo uliopangwa ili kusaidia kutatua au kutekeleza jambo fulani, kwa upande wetu jambo la kifasihi simulizi.
HISTORIA YA NADHARIA YA FASIHI SIMULIZI
Historia ya nadharia ya fasihi simulizi ilianza katika elimu ya ushairi, balagha n.k. ya Wagiriki toka karne ya 18. Katika karne ya 20 nadharia hii imekuwa ni mkabala mkubwa katika usomaji wa matini. Kuna nadharia mbalimbali za kifasihi kama vile Umuundo, Umarksi, Ufeministi nk.
Hivyo, tunaweza kujumuisha kuwa nadharia ya fasihi simulizi ni chombo kinachotoa mwongozo kuhusu mwelekeo wa jamii fulani. Hii ina maana kwamba ni mwangaza unaoimulika jamii juu ya mazingira na fikra zake. Kwa hali hiyo basi, nadharia hii haina budi kuzibainisha sifa na ushirikiano wa jamii husika.
Kuingia kwa ukoloni mamboleo kumefanya fikra na maarifa kutoka nje zitukuzwe na kuabudiwa huku fikra za ndani zikidumazwa kila kukicha. Kwa kufanya hivyo nadharia hizi zimeweza kuleta mabadiliko katika nadharia asilia zilizokuwepo. Kwa mfano; utamaduni wetu wa asili kama vile ususi, ufinyanzi, jando na unyago, nk zimebadilika baada ya kuingia kwa ukoloni mamboleo.
Hata hivyo, wahakiki wa Magharibi na Kiafrika wameangalia mambo mengi yaliyoikabili fasihi simulizi ya Kiafrika kama tutavyoona katika nadharia za fasihi simulizi tutakazopitia.
Nadharia za Fasihi simulizi tutakazojadili katika kozi hii ni hizi zifuatazo:
1: Nadharia za kitandawazi
Nadharia ya Ubadilikaji Taratibu (Evolutionalism Theory)
Nadharia ya Msambao (Diffusionism Theory)
Nadharia ya Kisosholojia (Sociological Theory)
2: Nadharia za kitaifa
3: Nadharia Hulutishi
1. Nadharia za Kitandawazi
Ubadilikaji Taratibu “Evolutionalism”
Mfuasi wa nadharia hii ni Charles Darwin (1809-1882) ambapo hoja zake zilikuwa na ushawishi mkubwa kwa wanafunzi waliokuwa wakijifunza kuhusu utamaduni kama vile Edward Burnet Tylor (1832-1917) na James George Frazer (1854-1941). Wote hawa waliamini juu ya misingi anuwai kuhusu kanuni zinazoongoza asili na maendeleo ya utamaduni wa mwanadamu.
Kundi hili liliona kuwa dhana ya ubadilikaji taratibu misingi yake mikuu ni viumbe hai. Wanaona kwamba viumbe hai vyote vinakuwa katika mchakato wa mabadiliko mbalimbali hadi kufikia maumbo vilivyonayo sasa.
Wanaedelea kusema kuwa kuna kanuni ambazo ni muhimu sana zinazochangia makuzi ya kanuni za binadamu. Wakaona kuwa kuna ukoo, akili au asili au jamii moja ambayo imezagaa ulimwenguni kote, na kama uchunguzi utafanywa wa kuchunguza jamii mbili kiutamaduni katika kipindi kilekile cha mabadiliko, itabainika kuwa elimu zao zina tabia zinazofanana.
Wanaendelea kusema kwamba, ili kuelewa jamii moja kwa ujumla ni vyema kulinganisha na jamii nyingine ya aina hiyo kwa kipindi kilekile cha ukuaji. Kwa mfano kuchunguza ngano za kijadi katika makabila mbalimbali ya Kusini kama vile uchawi na miviga na kulinganisha na jamii za Kiafrika.
Kwa ujumla katika nadharia hii tunabaini kuwa nadharia hii ilitawaliwa na mbinu linganishi (comparative methods).
Kwa mfano Frazer (kazi yake ni The Golden Bough ambayo ilikuwa katika majuzuu 13), alitafiti sanaa jadi ya Waitalia. Katika utafiti wake yeye alijihusisha na kutafiti chimbuko la matambiko ya uchawi na dini huko Italia. Alichokuwa anataka kuthibitisha kuhusu jamii ya Waitalia ni kwamba asili ya dini inapatikana katika magical rites za mtu wa kale.
Pamoja na watafiti wenzake, walikuja kama watawala na kuchunguza mila na desturi za Kiafrika ili kuzilinganisha na utafiti kama huo aliokuwa akiufanya huko kwao. Walitafiti na kuchunguza jamii ndogo ndogo za Kiafrika na kisha kufanya ulinganishi. Kwa ujumla wataalamu hao walikusanya, walitathimni fani mbalimbali za Kiafrika kama vile ngano, nyimbo, vitendawili, methali na aina nyingine, za FS katika jamii mbalimbali za Kiafrika. Baadhi ya watawala wataaluma wa kikoloni walitafiti kuhusu fasihi simulizi ya Kiafrika chini ya usimamizi wa Frazer ni pamoja na;
John Roscoe ambaye alitafiti jamii ya Baganda- Uganda.
Edwin Smith & Andrew Dale ambao walitafiti jamii ya Ila- Zambia.
Reverend Henri Junod- Tonga, Afrika Kusini
Robert Rattray- Akan-Ghana, pia Hausa- Nigeria
P. Amaury Talbot- Ekoi- Nigeria (Southeastern Nigeria)
H. Chatelain- Angola. Chatelain akichunguza kuhusu ngano za Angola na za Afrika kwa jumla, aligundua kuwa ngano za Kiafrika ni tawi toka mti mmoja wa ulimwengu.
Mwisho, wote kwa pamoja walihitimisha kuwa watu wa Afrika ni sawa na watu wengine popote pale ulimwenguni.
CHANGAMOTO
Dhana hii ya ubadilikaji taratibu iliathiri mbinu na matokeo ya utafiti wao kwa njia tofautitofauti kama vile:
Ø Kila kilichokusanywa katika fasihi simulizi kilihesabika kama masalia ya zamani au mabaki ya fasihi zilizotangulia.
Ø Kadri fani hizo zilivyorithishwa kwa njia ya mdomo toka kizazi kimoja hadi kingine ndivyo zilivyozidi kupoteza sifa mahsusi za ubora, zilichuja na kuchujuka
Ø Chochote kilichosalia lazima kitakuwa na dosari fulani tofauti na kitu halisi cha zamani
Ø Walijihusisha mno na maudhui na kamwe hawakujihusisha na sifa za kifani kama vile miundo na mitindo ya fani husika. Hii ni kutokana na ukweli kwamba lengo lao lilikuwa ni kufahamu hali halisi ya utamaduni wa jamii za watu wasiostaarabika na historia yao. Ili kuyafahamu haya waliona kuwa ni bora kupata muhtasari tu wa maudhui yanayojadiliwa ndani ya fasihi simulizi ya jamii husika na sio kujihusisha na fani ya fs hiyo
Ø Hawakuoa umuhimu wa fanani na mtambaji: “no creator, no author of such tales,…….as a product of joint or communal authorship.”
Ø Pia waliziona kazi za fasihi simulizi za Kiafrika kwamba hazina mwenyewe kwa kuwa ni mali ya jamii nzima. Walisema kwamba, ijapokuwa fasihi simulizi ni mali ya jamii, lakini sio kwa kiwango hicho walichokisema wao. Walisisitiza kuwa si kila mzungumzaji anaweza kuwa fanani wa fasihi simulizi. Wao walilipuuza suala la upekee wa muktadha.
HITIMISHO
Kimsingi, ilikuwa vigumu sana kupata matokeo sahihi katika uchunguzi ulioongozwa na misingi ya kiuibukaji. Hii ni kutokana na mbinu batili zilizotumika pamoja na kuongozwa na malengo muflisi na finyu kuhusu umbile la jamii za Kiafrika kwa jumla. Leo hii nadharia hii haitumiki tena katika mijadala ya fasihi simulizi. Wakoloni waliitumia kama njia ya kuhalalisha suala la uvamizi na ukoloni barani Afrika.
Nadharia ya Msambao “Diffusionism Theory”
Iliongozwa na mawazo na ushawishi wa Grimms na Thompson
Ni nadharia iliyopingana na nadharia ya ubadilikaji taratibu tuliyoona hapo juu. Wana ubadilikaji taratibu waliamini kuwa;
Ikiwa ngano mbili kutoka katika jamii mbili tofauti zimeonyesha kufanana kwa namna fulani za kimuundo au kimaudui ni kwa sababu wanadamu ulimwenguni kote wanamkondo mmoja wa mawazo na kufikiri kwao ni kwa namna moja, na kwamba ngano hiyo inasawiri hatua sawa za maendeleo ya kiutamaduni katika jamii husika.
Tofauti na wanaubadilikaji, wanamsambao wangeamini kuwa;
Pale ambapo kufanana kwa namna hiyo kutatokea, sababu ya msingi ya kuwapo kwa mfanano huo ni kuwa katika kipindi fulani hapo zamani sana jamii hizo mbili ziliwahi kukutana kwa namna fulani, makutano baina ya jamii hizo yalisababisha hali ya kuazimana kwa baadhi ya mila na tamaduni (mawazo) mojawapo ya jamii husika.
Watafiti hawa waliangalia mila na desturi za jamii zilivyokuwa zikikua na kusema kuwa zilikua kutokana na msukumo wa asili na lugha za Ulaya. Walikubaliana kwa sehemu kubwa kuwa asili ya mila, desturi na aina nyingine za utamaduni zinapatikana India, na walitaka kutafiti ni kwa kiasi gani utamaduni huu wa Indo-European ulikuwa umesambaa duniani.
Wana msambao nao walitumia mbinu ya ulinganishi kama walivyofanya wanaubadilikaji taratibu. Kazi ya utafiti ilihimizwa na wajerumani ambao ni Jacob na Wilhelm Grimm ambao walikusanya ngano nyingi kutoka India na kutoka katika nchi yao.
Jacob na Wilhelm Grimm: Walitafiti ngano kutoka India na Afrika, na walihitimisha kwamba, kuna kufanana kwa ngano za India na Ulaya. Wakatoa maamuzi ya kwamba, hadithi za Kiafrika ni chimbuko kutoka kwa wazazi wenye asili na utamaduni wa India na Ulaya. Hivyo, dhana yao hiyo waliifikia kutokana na kuifanyia kazi dhana potofu, kwani kila bara lina utamaduni, mila na desturi zake. Aidha waliliona bara la Afrika kama bara ambalo halijastaarabika.
Stith Thompson: Yeye aliwaunga mkono akina Jacob na Wilhelm. Katika kitabu chake cha The Folktale (1946:438) anapendekeza kuwa panapotokea kufanana kati ya ngano/hadithi za Ulaya na za Afrika, zinaweza kuelezewa kuwa huenda hadithi/ngano hizo zililetwa na Wazungu wakati wa utumwa.
Mawazo yao kwa ujumla ni kuwa;
Ø Utamaduni unaweza kusambaa tu kutoka katika jamii imara na maarufu tena yenye nguvu kuelekea kwenye utamaduni wa jamii iliyo kinyume chake “from superior to an inferior people)
Ø Ikiwa kulikuwa na kufanana kwa namna yoyote katika ngano zilizopatikana Afrika na Ulaya kwa mfano, lazima moja kati ya jamii hizo ni dhaifu kuliko nyingine, na jamii dhaifu….Afrika, ilihali jamii imara… ulaya
Ø Yote haya yangeweza kuelezwa tu kwa misingi ya ukweli kuwa jamii za Ulaya zilileta mambo hayo Afrika kutokea Ulaya kipindi cha biashara ya Watumwa (Thompson 1946:438)
Tafiti ziliendelea kufanyika baada ya Jacob, Grimm na Thompson ambapo bara la Afrika lilionekana kuwa bara lenye giza na hivyo kukaonekana haja ya kuanzisha dini ya Kikristo na teknolojia ya Ulaya barani Afrika ili Afrika iondokane na giza hilo.
Kwahiyo tunaweza kuona namna kila kitu cha Afrika ikiwemo fasihi simulizi yake vilivyodidimizwa na watawala hawa wa kikoloni.
Mapungufu
Tunaweza kusema kwamba, ingawa walijitahidi kuipa hadhi fasihi simulizi kwa kusisitiza upekee wa muktadha, hawakuchunguza kwa undani sifa za kisanaa za fasihi simulizi. Pia walijishughulisha na muhtasari tu wa simulizi walizochunguza, na hivyo ni dhahiri kwamba kuna vipengele vingine muhimu vya Fasihi Simulizi ya Kiafrika ambavyo havikutiliwa maanani..
Hitimisho
Ø Bado tafiti za namna hii hapa Afrika zinaendelea lkn mkabala na malengo ni tofauti
Ø Ule upendeleo uliokuwepo hapo zamani sasa umeondoka
Ø Sasa wanajihusisha na kutafiti msambao wa ngano na vipengele (units) vyake ndani ya tamaduni mbalimbali, katika bara la Afrika. Kama vile asili ya ngano za Kiafrika zinazosimuliwa katika Marekani ya Kusini na Kaskazini
Nadhari ya Sosholojia ‘Sociological Theory’
Mihimili ya Nadharia hii
(a) Umahsusi na sio umajumui
· Ilikuwa mahususi zaidi kuliko nadharia zilizotangulia: badala ya kujikita katika taaluma ya sanaa jadi kwa ujumla (maumbile ya mwanadamu na utamaduni wa mwanadamu) kama walivyofanya wanadharia wa zamani, nadharia ya usosholojia ilijikita katika jamii peke yake.
· Hii ilikuwa baada ya kugundua dosari zilizofanywa hapo kabla; dosari za kutoa matamko ya juu juu na ya kijumla zaidi
Ø Kauli hizo mara nyingi zilitupilia mbali vipengele fulani vya maisha kmv lugha na mienendo mingine….. hakika viliitofautisha jamii moja dhidi ya nyingine
Ø Kwao, tofauti zilizokuwepo baina ya jamii moja na nyingine zilikuwa na maana zaidi kuliko kufanana kulikokuwepo
· Kwa hiyo wanasosholojia waliazimia kuchunguza kila jamii kwa wakati na nafasi yake, kwa kurekodi kila kilichopatikana katika jamii husika (sanaa jadi yao).
· Wataalamu mbalimbali walioongoza jitihada hizi ni pamoja na hawa wafuatao
Ø Bronislaw Malinowski na A.R. Radcliffe-Brown (Uingereza)
Hawa walichunguza jamii mbalimbali katika Pasifiki, na waliandika mengi kuhusu jamii hizo. Jamii hizo ni pamoja na visiwa vya Trobriand na Andaman mutawalia
Ø Franz Boas (Marekani)
Huyu alichunguza jamii za wenyeji wa Marekani
· Wapo pia wataalamu wengi waliofanya utafiti wao, na kuandikia kuhusu jamii za Kiafrika ambao ni pamoja na hawa wafuatao
i. E.E. Evans-Pritchard………Nuer (Sudani)
ii. Geoffrey Lienhardt……..Dinka (Sudani)
iii. William Boscom…….Yoruba (Nigeria)
iv. S.F. Nadel………..Nupe (Nigeria)
v. Marcel Griaule……….Dogon (Burkina Faso)
Ingawa hata kabla ya wataalamu hawa, kulikwishakuwepo wataalamu wengine waliotafiti na kuandika kuhusu FS ya kiafrika lakini wataalamu hao waliongozwa na mawazo ya kiubadilikaji taratibu zaidi
(b) Mkazo katika Utendaji
-Tofauti na ilivyokuwa kwa wananadharia wa nadharia zilizotangulia ambao hawaku.... “They were not interested in studying the performers of oral tradition” wanasosholojia waliweka msisitizo katika kuchunguza PERFORMERS/watendaji wa fani mbalimbali za FS. Kutokana na msisitizo wao huu imebainika kuwa
*Fanani wa FS wana ujuzi na ustadi wa kiutendaji katika sanaa husika (ubunifu wao ni mkubwa sana). Jambo hili… limetusogeza mbele kidogo ktk kuielewa FS
*Wanasosholojia walidiriki na kuthubutu kudokeza kuhusu sifa za ndani za kimtindo katika FS ya kiafrika
(c) Msisitizo juu ya dhima ya Fasihi Simulizi katika jamii
Ø Tofauti na ilivyokuwa imedhaniwa hapo mwanzo kuwa FS ni mabaki tu ya zamani na kwamba hayakuwa na umuhimu wowote katika maisha ya jamii katika zama za kisasa, wanasosholojia waliamini kuwa uamilifu wa FS uko hai na haufi na kwamba unabadilika kulingana na maendeleo ya jamii husika. Dhima hizo ni pamoja na “DHIMA ZA KIJAMII ZA FS…KWA MUJIBU WA WANASOSHOLOJIA”
- FS ni kama Encyclopedia ya hekima za jamii husika
Hii ni kwa mujibu wa Bascom 1959 ambaye alifanya utafiti katika Poetry of Divination katika jamii za Wayoruba wa Nigeria
- FS ni nyenzo muafaka ya kurekodia hatua mbalimbali za maendeleo ya jamii husika. Aylward Shorter 1969…..the tales of origin katika jamii ya Wakimbu Tanzania
- FS inasaidia na imeendelea kusaidia kuimarisha ‘authority of statement or a custom in situation kama vile katika mahakama au contests for Chieftaincy. J.C. Massenger…..Anang of Nigeria 1958, J.B. Christenseu……Fante of Ghana 1958. Hawa walichunguza Methali katika jamii zilizotajwa
· CHANGAMOTO ZAKE…….Pamoja na uzuri uliotajwa bado kuna changamoto kadhaa
Ø Given far less time to illuminating and analyzing the artistic properties of African OL
Ø They have published tale, in flat, unimpressive prose, eliminating features of oral style (repetition and exclamation)
Ø They have done few carefully analyses of techniques of the original language that appealed to the audience of the tale in the first place
Ø The circumstances surrounding the performance of the tale (ushiriki wa hadhira, matumizi ya ala za muziki, nk) not reported
Ø Hata pale ambapo wamejaribu kuuleza vyema muktadha huu, umuhimu na nafasi yake katika kufanikisha au kukwamisha ngano husika haujaelezwa
Ø Ilikuwa vigumu sana kwa kutumia mbinu zao kuona ni kwa vipi ngano kwa mfano inaweza kuwa fasihi
Ø Pia kutokana na mbinu yao ya kusisitiza umuhimu wa FOLKLORE katika utamaduni wa watu, wataalamu kmv BOSCOM NA BEN-AMOS walisisitiza kuwa “Any judgement of a folk text must be based on the views of the society from which the text come” Wazo hili ni zuri sana lkn, ikiwa kazi za fs ya kiafrika zitaeleza mawazo ya wageni na si ya wenyeji, kmv boscom na amos, ni kwa sababu sanaa hizo zina sifa fulani fulani ambazo zinaenda na kueleza mambo fulani yaliyo mbali na dhana ya uzuri kwa waafrika. Mazingira km haya yakitokea, ni jukumu la mwandishi, ikiwa kweli wanaelewa vyema lugha husika, kufafanua sanaa husika na sifa za sanaa hiyo ilimuradi wageni waikubali sanaa husika na waipokee. Kwa hiyo mkabala wa MUKTADHA WA KIJAMII waliokuwa nao wanasosholijia ulikuwa FINYU SANA….. changamoto ya kiuhakiki ktk kazi za kifasihi
· HITIMISHO………..Hata kabla ya wataalamu hawa kufanya uchunguzi wa kisosholojia, walishakuwepo wataalamu wa mwanzo kama vile…………………….. ambao walifanya uchunguzi wa kisosholojia.
Ø Tofauti kubwa ni kuwa wale wa mwanzo waliongozwa na mawazo ya kiuibukaji
Ø Waliongozwa na kuhamasishwa na ….kizazi cha Franzer.
Ø Hawa wa baadaye walijihusisha na kuhamasika zaidi na “ HISTORIES OF THE CULTURES THEY STUDIED
Ø PIA waliongozwa na kuhamasishwa na mawazo ya Malinowski
Ø Pia hawa wa baadaye walitilia mkazo matumizi na uamilifu wa sanaa jadi za kiafrika katika jamii “SOCIETAL FUNCTIONS OF OL
Ø Hata hivyo, bado wataalamu hawa hawakufanikiwa au hitimisho lao halikuendana na tathimini ya karibu na kina kuhusu material walizozikusanya. Hii ni kwa sababu hawakuwa na ujuzi wa kutosha katika lugha za jamii za kiafrika

TOFAUTI KATI YA WANASOSHOLOJIA NA WANAUIBUKAJI AU WATAALAMU WENGINE WA MWANZO
· WATAALAMU WA MWANZO They were not interested in studying the performers of oral tradition
Ø Kwa sababu waliamini kuwa watendaji hawa walikariri tu mambo waliyoyapata kutoka kwa mababu zao siku za nyuma na kwamba wao wenyewe hawakuyaelewa mambo hayo, mengi yao. Hawakuyaelewa
Ø Pia waliamini kwamba, watambaji hawa walikuwa wajinga na washamba kabisa kiasi kwamba hawakuwa na uwezo w kuongeza ubunifu wowote katika sanaa hizo
Ø KWA UPANDE WAO wataalamu hawa waliweka msisitizo katika kuchunguza PERFORMERS wa fani mbalimbali za FS
Ø Kutokana na msisitizo wao huu tumebaini mambo murua yaendanayo na FS
i. Wamebainisha ujuzi na ustadi wa watendaji katika sanaa husika (ubunifu wao ni mkubwa sana)
jambo hili… limetusogeza mbele kidogo ktk kuielewa FS
Nadharia za Kitaifa
Utangulizi
· Je tunakumbuka changamoto za Nadhariaa zilizotangulia? Kwa mfano wanasosholojia?
Ø Hawakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu lugha za Kiafrika.
Ø Kwa kiwango kikubwa waliathiriwa na dhana za kikoloni na upendeleo wa kibeberu: Afrika ni bara la giza na la washenzi wasiokuwa na aina yoyote ya ustaarabu, na walistahili kustaarabishwa na Wazungu kupitia mlango wa ukoloni.
· Dosari hizi ziliathiri pia uwezo wao katika kuchunguza FS ya Kiafrika
Ø Mara baada ya kutafiti, hawakuwa tayari kuchapisha matokeo halisi ya utafiti wao: waliyahariri
Ø Kwa kutumia msaada wa wenyeji (viongozi na wasomi wa mwanzo) walitafsiri tafiti hizo katika lugha za kigeni
Ø Kila ambacho hawakukielewa, walikifuta kutoka katika data zao
Ø HATIMAYE, sifa na ujumi wa fasihi simulizi ya kiafrika haukudhihirishwa (LITERARY QUALITIES OF AOL WAS NOT APPRECIATED)
· Kutokana na dosari hizo, palihitajika kundi la wanazuoni wenye ujuzi na mtazamo mwingine, tofauti na ule wa kikoloni.
Ø Ndipo walipojitokeza wanazuoni wa Kiafrika kmv. S.Adeboye Babalola wa Nigeria, Daniel Kunene wa Basotho, Kofi Awoonor wa Ghana na J.P. Clark wa Nigeria
Ø Lengo na azma yao ilikuwa ni kukosoa mawazo ya wanazuoni wa Kimagharibi. Kwa kweli walifanya hivyo, tena bila kuyatathmini vilivyo.
Ø Ilifikiriwa kuwa wataalamu hawa walikuwa na sifa maridhawa za kuimarisha uchunguzi katika FS ya Kiafrika. Kwa mfano, mtazamo chanya kuhusu Bara la Afrika, uzoefu wao kuhusu FS ya Kiafrika na ujuzi wao katika lugha za Kiafrika.
Ø Kwa kutumia nyenzo hizi, walijaribu kuboresha tafiti za zamani za kikoloni katika FS ya Kiafrika. Je waliboreshaje?
Waasisi
S. Adeboye Babalola
- Nigeria, aliandika The Content and Form of Yoruba Ijala (1966)
- Ijala ni Ushairi wa Wawindaji katika jamii ya Wayoruba
· Yaliyomo kwenye kitabu hiki ni yapi
Ø Usuli wa kitamaduni wa utendwaji wa Ijala
Ø Sherehe na matukio mengine ambapo aina hii ya ushairi inatambwa
Ø Maudhui ya Ijala
Ø Mafunzo ya Washairi wa Ijala
Ø Utendaji wa Ijala
Ø Mbinu za kimtindo katika Ijala (ladha ya Kishairi)
- Complex structure of imagery and allusion
- The manipulation of sounds and the voice
- Linguistic devices.. (poetic diction)
Ø Matini ya Mashairi ya Ijala katika lugha ya Kiyoruba
Ø Tafsiri ya Mashairi katika lugha ya Kingeraza
Ø Tanbihi (Footnote) inayofafanua mambo muhimu katika tafsiri
Daniel P. Kunene
- Basotho (1971) Heroic Poetry of the Basotho
Yaliyomo kwenye kitabu cha Kunene
Ø Uchambuzi wa kina kuhusu muundo wa sarufi ya Kisotho
Ø Dhana ya Ushujaa kwa Wasotho
Ø Mbinu zitumikazo kuchagua majina muafaka ya mashujaa
Ø Uchambuzi wa majina ya Sifo… praise Names
Ø Kutathmini ruwaza ya Takriri…..(fomula simulizi)
Kutathmini
Ø njia ambazo mshairi anajenga ishara…
- Vitu mbalimbali katika utamaduni unaozunguka
- Mazingira
- Vitu mbalimbali vinavyosifiwa
Ø Uhusiano kati ya Mtindo wa Kishujaa katika FS na athari yake kwa washairi wa Kisotho katika zama za kisasa
Wanazuoni wa Kimarekani: Milman Parry na Albert Lord
- Harakati za kudai uhuru barani Afrika
Ø Ushairi simulizi wa Kishujaa: mashujaa wa tendi Simulizi
J.P. Clark wa Nigeria
Ø Mhariri wa Ozidi Saga (1977)
· Katika Ozidi Saga tunasimuliwa kuwa
Ø Ozidi ni hadithi ya Kijadi inayosimuliwa kwa muda wa siku saba
Ø Inasimulia kuhusu mbinu za kivita za kitamaduni za Shujaa Ozidi
Ø Mambo au vitu vinavyoambatana na hadithi kmv
- muziki,
- nyimbo,
- dansi na
- uigizaji wa matuko au vitushi muhimu
Ø alirekodi kila kitu kilichowezekana kunaswa na tape recoda
- tendo au kauli kutoka kwa mtambaji lililosababisha hadhira kuangua vicheko. Katika hali km hii, fanani alilazimika kufanya uradidi wa kauli au matendo hayo. Hali hii inaonyesha athari ushiriki wa hadhira katika utendaji
- matendo au kauli zenye kuibua hali ya mshangao na mshituko kwa hadhira
- kauli zilizotolewa na watazamaji ktk hadhira kmv maswali na maoni kuhusu utendaji husika
- majibu ya msimuliaji kuhusu kauli hizo
- hali ya utendaji ambapo mziki unachezwa na kisha ladha au midundo Fulani ya kimuziki huimbwa na kikundi cha wanamuziki wa fanani
Hitimisho;
Kutokana na yaliyosemmwa na kutendwa na Wananadharia ya Kitaifa, mambo kadhaa tunaweza kuyasisitiza
Ø Wanazuoni wenyeji walifanikiwa kueleza na kufafanua ufanisi wa mbinu mbalimbali za kimtindo katika FS
Ø Wanazuoni wa kiafrika hawakuwa wa mwanzo kufanya uchunguzi wa namna hii, badala yake hata wazungu walikwishajaribu kufanya hivyo, tatizo lilikuwa kwenye mtazamo (wa kikoloni na wa kitaifa)
Ø Walirekodi hali na muktadha wote wa utendwaji wa FS
Ø Wazungu walikosea kutathmini FS ya kiafrika kwa sababu walitumia vigezo vya FA … yenye misingi na utamaduni wa kimagharibi. Kimsingi, hizi ni Fasihi mbili tofauti, zenye kutoka katika jamii mbili tofauti, na hivyo zinahitaji vigezo tofauti vya utathmini. Zina michakato tofauti ya kiubunifu.
Nadharia hulutishi / HYBRIDITY THEORY
Iliasisiwa na Wanazuoni wa Kiafrika wenye mtazamo kuwa hata wageni wamechangia sana katika kukuza taaluma ya FS ya Kiafrika. Miongoni mwa waasisi na wafuasi hawa ni pamoja na M.M.Mulokozi, Johson na Ngungi wa Thiong
· Katika nadharia zote zilizotangulia, wakiwemo wana nadharia za Kitaifa kulikuwa na changamoto mbalimbali. Hata hivyo, changamoto hizo zilitofautiana kutoka kundi moja la wananadharia hadi lingine. Kwa kuwa changamoto za nadharia nyingine zilikwisha jadiliwa, hapa tutajadili na kugusia tu zinazohusiana na nadharia za kitaifa
Ø Walipinga kabisa mawazo ya wanazuoni wa Kimagharibi
Ø Walidai kuwa Wananadharia wa Kimagharibi hawakutoa jambo lolote la msingi kuhusu Afrika.
· Kimsingi, wazo kuwa Wanazuoni wote na tena mawazo yote yaliyotolewa na Wageni hayafai katika taaluma ya FS ya kiafrika ni batili.
· Huu ndio msingi wa kuibuka kwa Nadharia Hulutishi
· Nadharia hulutishi zinaleta uwiano wa kitaaluma na kuibua mjadala kuwa
Ø Ingawa kwa kiwango kikubwa mawazo ya Wanazuoni wa Kigeni yalitawaliwa na dosari kadhaa, si kila walichokinena kuhusu Afrika, hususani utamaduni na Fasihi ya Kiafrika ni kibaya.
Ø Kwa mujibu wa Mawazo ya Wananazuoni wa Nadharia Hulutishi, yaliyosemwa na Wageni yanahitaji kuchambuliwa na kufanyiwa ufafanuzi wa kina. Ndani mwake mna dosari na pia mna uzuri wa namna fulani. hayapaswi kupuuzwa kabisa.
· Katika utafiti na uchunguzi wa masuala yanayohusu FS ya kiafrika ni vema kuchanganya
- Mbinu bora kutoka kwa kigeni (F ya kigeni na mbinu zao)
- Mbinu bora kutoka kwa wenyeji (F ya Kiafrika kwa kutumia mbinu za kiafrika)
· Matokeo yake, ilipatikana aina fulani ya fasihi yenye sifa Mchanganyiko, ndio maana iliitwa nadharia Hulutishi

Mchango wa Wageni ktk FS ya Kiafrika
1. RUTH FINNEGAN
- Alifanya utafiti na kuandika mengi kuhusu Afrika
- Miongoni mwa kazi zake ni pamoja na Limba Stories & Storytelling (1967), Oral literature in Africa (1970)
- Katika kazi zake hizi Finnegan anafanya yafuatayo kuhusu afrika na fasihi yao kwa ujumla
ü Anaukana muelekeo uliokuwepo wa kulitazama Bara la Afrika na Fasihi yao
Kutotilia maanani ubunifu wa fanani wa fs na bara la Afrika kwa ujumla
ü Anathamini sifa za kiubunifu za FS ya kiafrika
- Hata hivyo, naye hakusafika sana, kwani pamoja na mchango wake mzuri anatenda makosa kadhaa ya kiufafanuzi na kinadharia. Makosa haya yalileta athari kubwa kwa wanazuoni wa baadaye kuhusu umbo na sura halisi ya FS ya Kiafrika. Makosa ayatendayo ni yapi/
ü Afrika hakuna tendi
ü Afrika hakuna Visasili
2 . GORDON INNES
- Amechunguza tendi simulizi za jamii ya Wamandinka huko Gambia
- Katika uchunguzi wake alihimiza wasifu wa kila msimuliaji, na Muktadha wa utambaji wao, kmv matumizi ya ala za muziki
- Kutokana na utafiti wake alithibitisha na kuunga mkono wazo la Finnegan kuwa katika jamii za kiafrika kuna uwezekano kuwa, watambaji au wasimuliaji tofauti wenye kusimulia kisa kimoja kwa namna tofauti tofauti, tofauti hiyo inasababishwa na ujuzi wa mtambaji, uzoefu wa mtambaji na muktadha wa utambaji. Kwa maana hiyo basi, tunapata mawazo kuwa
ü Innes ana imani kuwa watambaji wa FS kwa kawaida hawana mtindo mmoja wa utambaji. Hii ni kwa sababu kila mmoja ana ustadi wake, uzoefu wake na muktadha tofauti na mtambaji mwingine.
2.5 Hitimisho na Tathmini
Katika hatua za hivi karibuni kumekuwapo na mapinduzi makubwa kuhusu FS ya Kiafrika na Bara la Afrika kwa Ujumla. Huu tunaweza kuiita mueleko mpya ambao “giving greater recognition to the literary qualities of African Oral Literature’. Swali ni kuwa je, muelekeo huu mpya umesaidia kwa kiasi gani mustakbali wa FS ya Kiafrika?
Ø Kuondolewa na kufutika kwa dhana potofu kuhusu Bara la Afrika
Ø Kukomaa kwa mtazamo chanya kuhusu FS ya kiafrika
- Methali na vitendawili “depth of wisdom
- Kiwango kikubwa cha ubunifu
- Utamaduni ambapo FS hii imechipuka ni changamani sana
Ø Kukua na kukomaa kwa taaluma ya F ya Kisasa ya Kiafrika
- Hapo mwanzo F ilitazamwa kama sehemu ya sanaa au tawi la Anthropolojia
- Sasa hivi, somo la F linasomwa na kufundishwa katika Vyuo na Taasisi mbalimbali kama somo linalojitegemea. Lina malengo yake, na nadharia zake
- Linaonyesha uhusiano mkubwa kati Fs ya kijadi na F ya kisasa ya kiafrika
Ø Uzuri na umaridadi wa utamaduni wa Kiafrika sasa hivi unatangazwa kwa njia ya kukusanya na kutafsiri mbinu na tanzu za FS ili kupata F ya kisasa. Katika utunzi mpya, mbinu za kisasa na za zamani za FS zinachanganywa pamoja
Ø Sasa, maswali mengi ya kiutafiti yamepatiwa ufumbuzi; sisi ni akina nani? Tuko wapi? Tunafanya nini? Kwa nini tuko hapa? Tumefikaje hapa tulipo leo hii? Je, hatua tuliyofikia inakidhi haja na matakwa ya kijamii katika hali zote (hususani haja ya kisanaa au kiubunifu? Kama haikidhi haja hiyo, tufanyeje ili tusonge mbele?


FASIHI LINGANISHI YA KISWAHILI NA TAFSIRI
Lengo la makala hii ni kuangalia kwa ufupi fasihi linganishi ya Kiswahili na tafsiri kwa kuzingatia uchambuzi wa utanzu uliofasiriwa zaidi kulingana na data zilizokusanywa huku msisitizo ukiwa katika mchango wa tafsiri katika fasihi linganishi ya Kiswahili pamoja na changamoto zitokanazo na mchakato wa tafsiri katika kufasiri matini za kifasihi.
Ili makala hii iweze kueleweka zaidi kipengele cha fasili ya dhana za msingi kama vile fasihi linganishi pamoja na tafsiri kimezingatiwa kama ifuatavyo:
Maana ya fasihi linganishi; Miongoni mwa wataalam waliofasili dhana ya fasihi linganishi ni Boldor (2003) akimrejelea Compbell (1926) anaeleza kuwa, fasihi linganishi ni taaluma inayochunguza uhusianao uliopo baina ya fasihi mbili au zaidi nje ya mipaka ya kitaifa kwa njia ya kulinganisha mfanano na msigano (tafsiri yangu).
Dhana nyingine ya msingi ni tafsiri; Kwa mujibu wa Mwansoko na wenzake (2006) tafsiri ni uhawilishaji wa mawazo katika maandishi kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine. Hivyo, tafsiri ni miongoni mwa nyenzo muhimu katika kukuza na kusambaza fasihi kama ifuatavyo:
Tafsiri imesaidia kuingiza utanzu mpya katika fasihi andishi ya Kiswahili, kwani historia ya fasihi barani Afrika inaonesha kwamba, hapo awali jamii za kiafrika hazikuwa na utanzu huu wa fasihi. Hivyo basi, kupitia tafsiri fasihi ya Kiswahili imeweza kujitanua zaidi.
Pia tafsiri imesaidia kukuza na kusambaza fasihi ya Kiswahili ulimwenguni. Kwa mfano kiswahili kwenda lugha nyingine kama vile, Kijerumani “Kasri ya Mwinyi Fuad” (Dei Sklaverei der Gewiirze). iliyotafsiriwa na Manique Lutgens na Karin Boden (1997). Pia riwaya ya “Uhuru wa Watumwa” (The Freeing of the Slaves). iliyotafsiriwa na E.A.L.B. (1967) “Nagona na Mzingile” imetafsiriwa kwa Kifaransa na Xavier Garnier, “Bwana Myombekere na Bibi Bugonoka” imetafsiriwa kwa Kijerumani na Wilhelm J. G. Mohling nk.
Naye Ruhumbika katika makala yake (2003) anaeleza, kupitia tafsiri wasanii hukomaa kwa kusoma maandishi ya wasanii wengine na kujifunza mbinu mbalimbali ambazo zitasaidia katika kukuza na kueneza fasihi ya Kiswahili.
Vilevile mataifa mbalimbali huweza kujifunza utamaduni na historia za mataifa mengine kupitia kazi za kifasihi zilizotafsiriwa, hivyo fasihi ya taifa husika hukua na kuenea zaidi.
Lifuatalo ni jedwali la mapitio ya vitabu mbalimbali vilivyotafsiriwa kwa lugha ya kiswahili.

JINA LA KZI
UTANZU
JINA LA MFASIRI
MWAKA
LUGHA

“The Well of Gining” Kisima cha Giningi
Tamthilia
Muhamed S. Abdalla
1968
Kiingereza-Kiswahili

Maisha Yangu “Moya Zhizn”
Riwaya
Andrei Zhukov
1968
Kiswahili-Kirusi
3
Historia ya Dunia ya Kale

V. Makarenko
1988
Kirusi-Kiingereza
4
Dada Alyonushka na kaka Ivanushka
Hadithi
M. Mbigili.
2002
Kirusi-Kiswahili
5
Postamasta
Riwaya
Bernard Mapalala
2003
Kirusi-Kiswahili
6
Tufani
Tamthilia
Samuel S. Mushi
1969
Kiingereza-Kiswahili
7
“I will marry when I want” Nitaolewa Nikipenda
Tamthilia
E. A. E. P. Ltd
1982
Kiingereza-Kiswahili
8
(The list) Orodha
Tamthilia
Saifu D. Kiango
2006
Kiingereza-Kiswahili
9
(The Beautiful One are Not yet Born) Wema Hawajazaliwa
Riwaya
Abdilatifa Abdallah
1976

Kiingereza-Kiswahili
10
“The Test of Heaven” Aliyeonja Pepo
Tamthilia
M. Mkombo
1980
Kiingereza-Kiswahili
11
“The Government Inspector” Mkaguzi Mkuu wa Serikali
Tamthilia
Christon Mwakasaka

1979

Kiingereza-Kiswahili
12
Uhuru wa Watumwa “The Freeing of The Slaves in East Africa”
Tamthilia
E. A. L. B.
1967
Kiswahili-Kiingereza
13
“Anthology of Swahili Poetry” Kusanyiko la Mashairi
Ushairi
Ally Ahamed Jahadhmy
1975

Kiingereza-Kiswahili
14
“The Black Hermit” Mtawa Mweusi
Tamthilia
E. A. E. P. Ltd
1970
Kiingereza-Kiswahili
15
“Song of Lawino” Wimbo wa Lawino
Ushairi
Paul Sozigwa
1975
Kiingereza-Kiswahili

Baada ya kuangalia mapitio mbalimbali ya kazi za fasihi ya Kiswahili zilizotafsiriwa ifuatayo ni tathmini fupi ya kazi hizo;
Katika kufanya tathmini imebainika kuwa tamthilia ni utanzu unaonekana kufasiriwa sana kutokana na sababu zifuatazo:
Mwansoko (2006:46) tamthilia ni utanzu uliotafsiriwa sana kutoka na malengo makuu mawili; lengo la kuigizwa na lengo la kusomwa. Pia umefasiriwa sana kutokana na kwamba, ulikuwa ni utanzu mpya katika Afrika, hivyo wageni na wenyeji walitafsiri kwa lengo la kuutambulisha katika mazingira ya kiafrika. Vilevile umeonekana kutafsiriwa sana kutokana na urahisi wa lugha yake, kwani tamthilia hutumia maneno machache na yanayoeleweka tena bila hata ya ufafanuzi wa kina kama ilivyo katika riwaya.
Pia umefasiriwa sana kutokana na umuhimu wa maudhui yake ambayo hujibainisha katika masuala mtambuko duniani kote. Kwa mfano; tamthilia ya “Nitaolewa Nikipenda, Mtawa Mweusi” nk. maudhui yake yanahalisika katika jamii mbalimbali. Vilevile umetafsiriwa sana kwa lengo la kukuza na kueneza lugha adhimu ya Kiswahili, ambayo haikuwa na machapisho mengi yahusuyo fasihi andishi.
Kwa upande wa lugha zilizojitokeza zaidi katika kufanikisha suala la tafsiri ya fasihi ya Kiswahili ni lugha ya kiingereza, na Kiswahili; lugha ya Kiingeza imejitokeza sana katika tafsiri kutokana na kwamba, waingereza ni moja kati ya mataifa yaliyotawala sehemu kubwa ya dunia, na ndio taifa lililokuwa na dola yenye nguvu zaidi. Vilevile waingereza walishapiga hatua kubwa katika maendeleo ya fasihi ukilinganisha na mataifa mengine. Pia hata lugha ya kiingereza ni moja kati ya lugha kubwa duniani na inayofahamika na mataifa mengi.
Lugha ya Kiswahili nayo imeonekana kutafsiriwa sana kutokana na hitaji la kuwa na machapisho mengi ya kifasihi ili kukuza na kueneza fasihi ya Kiswahili. Pia ni lugha inayokua kwa kasi na inayoeleweka sana Afrika Mashariki ukilinganisha na lugha nyingine.
Pamoja na hayo yote, bado inaonekana kuwa, ushairi ni utanzu unaokabiliwa na changamoto nyingi zaidi katika kufasiri kutokana na kwamba, kwa kiasi kikubwa ushairi hutumia lugha ya mkato na ya kisanaa zaidi yenye msamiati mgumu uliosheheni taswira, ishara, lahaja, tamathali za semi pamoja na misemo, mafumbo nk. Hivyo basi, kuna uwezekano mkubwa wa kupotosha maana ya kifasihi pamoja na sanaa iliyomo katika utanzu huu.
Licha ya hayo, vilevile ugumu unasababishwa na kanuni za kiarudhi hasa katika mashairi ya kimapokeo kwani, ni vigumu sana kutafsiri ushairi huku ukizingatia urari wa vina na mizani bila kupotosha maana iliyokusudiwa.
Hivyo basi, ili kuepuka changamoto hizo ingefaa sana mfasiri anayefasiri utanzu huu awe mahiri wa lugha zote mbili, pia awe mtu mwenye upeo mkubwa katika uwanja huu na mwenye juzi mkubwa wa kutunga mashairi au naye awe kiasi fulani msanii. Hivyo haitamwia vigumu sana katika kuteua maneno mwafaka.
Baada ya kuangalia tathmini ya mapitio hayo ufuatayo ni uchambuzi wa tamthilia ya “Mkaguzi Mkuu wa Serikali” kwa muongozwa wa nadharia ya usawe wa aina matini.
Newmark (1982) matini yoyote ile ifasiriwe kwa kuzingatia aina yake. Hii ina maana kwamba, kazi itakayotokea itafanana na matini chanzi. Vilevile mbinu ya “Ulinganishaji Matini” itatumika katika kufanya uchambuzi wa kazi teule, kwani katika mbinu hii matini lengwa hulinganishwa na matini chanzi ili kubaini vipengele vya kifani na kimaudhui vilivyoongezwa, vilivyopunguzwa na vilivyopotoshwa.
Kipengele hiki kitajihusisha na uchambuzi wa tamthilia ya “Mkaguzi Mkuu wa Serikali” iliyoandikwa na Nikolai V. Gogol katika lugha ya Kirusi na kutafsiriwa katika lugha zote kuu duniani ikiwemo Kiswahili. Tafsiri ya Kiswahili imefanywa na Christon Mwakasaka kupitia tafsiri ya Kiingereza iliyofanywa na D. J. Campbell kutoka katika lugha ya Kirusi.
“Mkaguzi Mkuu wa Serikali” ni moja kati ya tafsiri za kifasihi ambazo ni bora kwa kiasi fulani katika upande wa maudhui na ni mbovu kwa kiasi kikubwa katika upande wa fani. Ubovu huu unatokana na mfasiri kutozingatia nadharia ya “Usawe wa Aina Matini”. Hali hii imesababishwa na kufasiri tafsiri, yaani kufanya tafsiri kupitia matini iliyotafsiriwa bila kutumia matini chanzi kama ifutavyo:
Mfasiri amepotosha muundo asilia wa tamthilia na kusababisha kutokea kwa tafsiri tenge/mbovu. Kwa mujibu wa Gromova (2004) tafsiri ya Kiswahili ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali iliegemea tafsiri ya Kiingereza, ambayo ilifupisha matini asilia na kuigawa tamthilia ya Gogol katika matendo matatu badala ya matano. Kitendo hiki kinapunguza ubora katika taaluma ya fasihi linganishi ya kiswahili kwa kuifanya fasihi ya kiswahili kuwa na mapungufu.
Vilevile kuna upotoshaji mkubwa katika kufasiri majina ya wahusika. Mchambuzi Gromova katika makala yake anafafanua kwamba, ni vigumu sana kutafsiri katika Kiswahili majina ya Kirusi, kwani yana maana fulani. Katika tamthilia “Mkaguzi Mkuu wa serikali” kuna wahusika wengi ambao majina yao yanasababisha msomaji Mrusi apate taswira ya tabia zao. Kwa mfano, katika tafsiri ya Kiingereza lile jina la Constables ambalo katika Kiswahili ni Askari na katika Kirusi ni “Dyerzhimorda” halina maana ileile iliyokusudiwa kwa msomaji wa Kiswahili au Kiingereza. Kwani kwa Kirusi neno “morda” ni uso wa mnyama, na neno hili linatumika kwa ajili ya mtu ambaye unataka kumdharau. Ama lile jina la jaji “Lyapkin-Tyapkin” linatokana na mwigo “lyap-tyap”, maana yake ni kufanya kazi ovyo, bila nidhamu.
Pia kuna upunguzaji wa matini: Ukilinganisha matini ya Kiingereza na matini ya Kiswahili utaona kuwa katika tafsiri ya Kiswahili mfasiri hakueleza wasifu wa wahusika wakati katika tafsiri ya Kiingereza uk.16 mfasiri ameeleza kwa kirefu wasifu wa baadhi ya wahusika. Mbinu hii kama ingeingizwa katika matini lengwa ingeleta mchango mzuri katika fasihi linganishi ya kiswahili, kwani msomaji wangepata hamasa ya kutaka kujua zaidi kuhusiana na mhusika aliyemvutia. Mbinu hii haipo kwa waandishi wengi wa fasihi ya Kiswahili.
Vilevile kuna upotoshaji mkubwa wa mandhari. Mfasiri Mwakasaka katika tamthilia ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (uk.vi) anakiri kwa kusema kuwa “...nimekata maelezo ya jukwaani kila nilipoona kuwa si ya lazima.” Kitendo hiki hakifai kabisa katika kazi za kifasihi kwani maelezo ya jukwaani ni muhimu sana katika ujengaji wa mandhari, wahusika na dhamira. mfano katika tafsiri ya Kiingereza “ACT” 1 uk.23 kuna maelezo marefu sana yanayofafanua mandhari, wakati katika Kiswahili ONESHO LA KWANZA hakuna maelezo kama hayo.
Upotoshaji wa kipengele cha mtindo: katika matini lengwa neno “ACT” limefasiri mara mbili yaani act kama onesho uk.41 na act kama tendo uk.64, wakati katika matini chanzi “The Government Ispector” limetumika neno “ACT” mwanzo mpaka mwisho. Upotoshaji huu hauna mchango mzuri katika fasihi linganishi ya kiswahili kwani huleta mkanganyiko kwa wasomaji juu ya kipengele cha mtindo.
Upotoshaji wa jalada la kitabu. Katika matini lengwa mfasiri ameweka picha ya mtu anayedhaniwa kuwa ndiye Mkaguzi Mkuu wa Serikali, wakati katika matini chanzi hakuna picha kama hiyo. Hivyo basi, kitendo hiki kinatoa mchango hasi katika taaluma ya fasihi linganishi ya Kiswahili kwani, huifanya hadhira ifikiri kwamba hivi ni vitabu viwili tofauti.
Pamoja na mapungufu hayo mfasiri kwa kiasi kikubwa amefanikiwa sana katika kipengele cha kimaudhui, hasa katika upande wa dhamira na ujumbe. Dhamira zilizojitokeza katika matini chanzi zimejitokeza pia katika matini lengwa. kwa mfano, uongozi mbaya, rushwa, utapeli, uvivu, ukahaba, uaminifu nk. Mfano, (uk.72) Bw. Posta hakuwa mwaminifu katika kazi yake kwani alikuwa akifungua barua za watu. M/WILAYA: “Lakini uliwezaje kufungua barua ya mtu mashuhuri kama yule...” Vivyo hivyo hata katika matini chanzi suala hili linajitokeza. Mfano, (uk.88) Mayor: “But how dared you open the mail of such an important personage?” Kwa ujumla kipengele hiki cha maudhui katika fasihi linganishi ya kiswahili kina mchango mkubwa sana katika fasihi ya kiswahili kwani watunzi wa kazi za kifasihi hujifunza mbinu mbalimbali katika kuelezea masuala ya kijamii. Pia hata wasomaji kupitia kazi za fasihi zilizotafsiriwa huweza kujifunza tamaduni za mataifa mbalimbali.
Hivyo basi, pamoja na yote yaliyojadiliwa katika makala hii bado mchakato wa kufasiri kazi za kifasihi unakabiliwa na changamoto mbalimbali kama ifuatavyo:
Umahiri wa lugha zote mbili au moja kwa wafasiri; yaani lugha chanzi na lunga lengwa. Kwa mfano, Mwakasaka amefasiri kupitia tafsiri ya Kiingereza kutoka na kutomudu lugha ya Kirusi, hivyo anarudia makosa yaliyopo katika tafsiri ya Kiingereza kwenye Kiswahili.
Changamoto nyingine ni tofauti za kiutamaduni. Mambo kama dini, mavazi, mila na desturi. Kwa mfano, majina ya Kirusi huwa na maana yenye ujumbe mahususi, hivyo yanapofasiriwa katika kiswahili hupoteza ile maana halisi na kupotosha ujumbe uliokusudiwa.
Vilevile changamoto ya tofauti za kiisimu baina ya lugha mbili katika muundo wa sentensi na maumbo ya maneno. Kwa mfano muundo wa Kiingereza ni tofauti na muundo wa Kiswahili.
Pia changamoto nyingine ni kutoelewa mbinu mwafaka ya tafsiri husika, hivyo husababisha tafsiri kuwa tenge/mbovu.
Hivyo basi, ni dhahiri kwamba si rahisi kupata tafsiri iliyosahihi kwa asilimia zote, isipokuwa tunaweza kupata tafsiri bora kama tu wafasiri wa kazi za kifasihi watakuwa na sifa stahiki.
Kwa mfano, uwezo wa kumudu lugha, kujua utamaduni wa lugha husika pamoja na mazingira yake, kuwa na ujuzi wa taaluma husika kabla ya kufasiri nk. Kwa misingi hii tunaweza kupata tafsiri za kifasihi zilizobora zaidi

MAREJEO
Boldor, A. (2003). etd.lsu.edu/docs/available/etd-0408103.../Boldor_thesis.pdf “Perspectives on comparative literature”. Babes-Bolyai University, Cluj. May 2003.
Gogol, N. (1836). The Government Inspector. (Translated & adapted by D.J.Campbel 1974). East African Educational Publishers. Nairobi.
Gogol, N. (1836). The Government Inspector. (Mkaguzi Mkuu wa Serikali 1979). Kimetafsiriwa na Christon Mwakasaka. East African Educational Publishers. Nairobi.
Gromova, N.V. (2004). “Tafsiri Mpya za Fasihi ya Kirusi katika Kiswahili”. Swahili forum11 (2004): 121-125.
Newmark, P. (1982). Approaches to Translation. Oxford. Pergamon Press. London.
Ruhumbika, G. (2003). “Tafsiri za Fasihi za Kigeni Katika Ukuzaji wa Fasihi ya Kiswahili.” Makala za Semina ya Kimataifa ya Waandishi wa Kiswahili III (2003). TUKI. Dar es Salaam.
Mwansoko, H.J.M na wenzake. (2006). Kitangulizi cha Tafsiri: Nadharia na Mbinu. TUKI. Dar-es-salaam.
UCHAMBUZI WA VITABU VYA SHAABAN ROBERT ULIOFANYWA NA WANAFUNZI WA SHAHADA YA AWALI YA KISWAHILI MWAKA WA TATU CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.

UHAKIKI WA RIWAYA YA KUFIKIRIKA
MWANDISHI S. ROBERT
Riwaya ya kufikirika ni riwaya iliyotungwa na mwandishi mashughuli Shaabani Robert, katika riwaya hii mwandishi anaeleza juu ya mila na desturi zilizopitwa na wakati kuwa hazina nafasi katika kipindi cha sasa. Mwandishi anaeleza kuwa jamii ya watu wakufikirika ilikuwa inaamini juu ya uganga na mambo ya kijadi. Hivyo kupitia mhusika utu busara ambaye alikuwa anaelimu kubwa ya dunia. Utu Busara alijiingiza katika kundi la utabiri ili aweze kuleta mabadiliko katika nchi ya kufikirika. Kutokana na utabiri wake Mfalme na Malkia wanafanikiwa kupata mtoto na baadae Utu Busara tena anakuwa mwalimu wa mtoto wa mfalme na kuanza kumfundisha elimu ya dunia ambayo ni kinyume na matakwa ya mfalme, baada ya kufukuzwa na mfalme, Utu Busara anaamua kujiingiza katika kilimo ambapo ikapelekea kukamatwa kwa kudhaniwa kuwa ni mjinga. Kutokana na elimu na weledi alionao utu busara anafanikiwa kujiokoa kutoka gerezani na kufanikiwa kumponya mtoto wa mfalme kwa kutoa ushauri kuwa apelekwe hospitali. Mwisho mtoto wa mfalme anapona na kufanya utu busara kufanikiwa katika nia yake ya kuleta mabadiliko katika nchi ya kufikirika.
Katika kuhakiki na kuchambua riwaya hii ya Kufikirika tutazingatia vipengele vya fani na maudhui. Hivyo tutaanza kwa kuchambua vipengele vya maudhui ambavyo hujumuisha dhamira, ujumbe, migogoro, mtazamo, na falsafa na kisha tutatalii kwa kina juu ya fani na vipengele vyake..
Dhamira, Katika riwaya hii ya Kufikirika mwandishi shaaban Robert ameonesha dhamira kuu ni ukombozi wa kiutamaduni. Kiujumla riwaya ya kufikirika inajdili harakati zinazofanywa na Utu Busara za kupambana na tamaduni zilizopitwa na wakati. Kupitia mhusika Utu Busara mwandishi anaonesha kuwa mila na tamaduni zilizopitwa na wakati hazina budi kutupiliwa mbali hasa katika kipindi hiki cha sayansi na teknolojia.
Licha ya dhamira kuu, pia mwandishi amejadili dhamira ndogondogo kupitia wahusika lukuki ambao amewatumia katika riwaya hii, Dhamira hizo ni kama zifuatazo:
Suala la uongozi, Mwandishi Shaban Robert hakupuuzia suala la uongozi katika riwaya hii, anaonesha kuwa viongozi wa nchi ni lazima wawe mstari wa mbele katika kuhakikisha maslahi ya nchi yanalindwa na wananchi wanaishi kwa amani. Mwandishi anabainisha suala hili kwa kumtumia mhusika mfalme (uk 1-2)
“Nimejaliwa kupata ufalme kuliko wafalme wengine walio majirani zangu. Binafsi yangu nimepigana vita nyingi kulinda nchi isitekwe adui. Ushindi wa kila vita umenipa utukufu wa namna ya peke yake. Milki yangu pana imeenea kaskazini, kusini, mashariki na magharibi.”
Suala la ugumba na utasa,mwandishi shaban robert hakusita kulielezea suala la ugumba na utasa katika riwaya hii ambalo ndio lilipelekea kuibua dhamira mbalimbali. Mwandishi anamtumia mhusika mfalme na malkia katika kuonesha tatizo hili. Mwandishi anaonesha kuwa licha ya ujasili, uzalendo na furaha yote aliyokua nayo mfalme na malkia lakini walijiona sio kitu kutokana na kukosa mtoto, ambaye angekuja kurithi madaraka mara baada ya kufa kwa mfalme.(uk 3)
“................jina lake litachorwa kwa majohari, wa watu hawa na pia nashukuru kwa kuwa bwana juu ya vitu vya faraja visivyokwisha, lakini nina sikitiko kubwa kwa kukosa mtoto. Maskini mwenye mtoto namuona kuwa bora kuliko mimi.............”
Kutokana na tatizo hili mfalme akatafuta kila njia ili aweze kupata mtoto. Hapa ndipo mfalme alipoamua kuweka bayana tatizo lake hili aweze kuaidiwa.
Suala la imani potofu, mwandishi anaonesha juu ya dhana potofu zilizojengeka katika vichwa vya watu wa kufikilika juu ya mtu mwerevu na mjinga. Wanaona kuwa mjinga na mwelevu hujulikana kutokana na kazi anayoifanya mtu, utu busara alionekana kama mtu mjinga kutokana na shughuli ya kilimo aliyokuwa anaifanya halikadhalika mfanyabiashara alionekana mwelevu kutokana na kazi yake (uk 39)
”............mtu wa kwanza alikuwa na umbo kuza. Kazi yake ilikuwa ni biashara mjini. Ajali ya kukamatwa ilikua amekaa kitako dukani pake. Yeye alihesabiwa kuwa ni mwerevu. Mtu wa pili alikua na umbo la wastani. Amali yake ilikuwa ni ukulima. Ajali ya kufanywa mahabusi wa kafara ilimkuta shambani pake analima. Huyu alidhaniwa kuwa ni mjinga........”
Kutokana na mtazamo huu, hatimaye mwelevu aliweza kujinasua na kifo hicho, hivyo mwandishi shaban robert anajaribu kutoa mwanga kwa jamii juu ya dhana potofu na kuitaka jamii kubadilika ili kuendana na wakati.
Halikadhalika imani potofu imekisili katika jamii ya watu wa kufikirika kwani wanaamini juu ya mambo ya jadi hasa uganga na kupuuzia huduma za kisasa kama vile hospitali. Hivyo mwandishi shaban robert kupitia mhusika wake Utubusara anaitaka jamii kuachana na mila na tamaduni zilizopitwa na wakati kwani huweza kusababisha hasara kubwa kwa jamii husika kama ilivyowapata watu wa kufikirika ambao walipoteza vitu vingi kwa ajili ya uganga (Uk 8-14)
Nafasi ya mwanamke, mwandishi shaaban robert hakupuuza nafasi ya mwanamke katika riwaya yake. Katika riwaya hii mwandishi amemchora mwanamke kama mtu muhimu katika jamii mwenye kutoa ushauri na ukakubalika. Mfalme analithibitisha hili katika ( uk 1) anasema
“.........alikuwa tayari kupokea msaada uliotolewa kwa hiyari na mwanamke lakini kulazimisha kutendewa msaada hakupenda. Aliona kazi na faraju zitendwazo na wanawake katika maisha zilitosha kuwa mzigo mzito juu yao.....”
Hivyo mwandishi anaonesha jinsi mwanamke anavyofanya mambo makubwa katika jamii, hivyo anapaswa kuheshimiwa na kuthaminiwa.
Pia mwanamke amechorwa kama mtu mvumilivu, mwandishi Shaaban Robert amemuonesha mwanamke kama mtu mwenye kuvumilia matatizo mbalimbali yanayomkabili. Malkia licha ya kukumbwa na tatizo la kukosa mtoto hakuvunjika moyo aliendeleza upendo wake kwa mfalme mpaka pale mungu alipowajalia kupata mtoto.
Dhamira nyingine ni dharau na majivuno, dhamira hii imejitokeza pale ambapo mhusika Mfanyabiashara alipokuwa gerezani alikuwa anamdharau utu busara. Kutokana na kazi aliyokuwanayo mfanyabiashara alijiona kuwa ni bora kuliko mkulima( uk 40)
.............Huwaje, wewe mvaa koja la ushanga shingoni kama mwanamke kupata njia! Una sifa zaidi ya ujinga. Nashangaa kwanini hawakutakiwa wajinga wawili kwa kafara hii! Ujinga ni ila ya kustahili upanga wa chakali.
Umuhimu wa elimu ni dhamira nyingine ambayo mwandishi Shaaban Robert ameijadili katika kazi yake. Mwandishi anaonesha kuwa watu wa Kufikirika walikuwa hawana elimu ya dunia walijiegemeza zaidi katika mambo ya uganga, hivyo utu busara alijaribu kuleta mabadiliko katika nchi ya kufikirika kwa kuwapatia elimu ya dunia ambayo baadae ilisaidia kuikomboa nchi ya kufikirika.
Pia dhamira nyingine ni matumizi mabaya ya mali, kutokana na mfalme kukosa mtoto, waganga walitumia sehemu kubwa ya mali ya nchi ya kufikirika hadi ikapelekea matatizo katika nchi ya kufikirika( uk 14)
Nchi ambayo zamani ilikuwa ya shibe, utajili, nguo, tafrija na neema zote sasa ilikuwa imegeuka nchi ya njaa, umaskini, uchi, uzito na uhitaji wa kila namna ulikuwa mbele ya watu.........
Kipengele kingine ni ujumbe. katika riwaya ya kufikirika kupitia dhamira mbalimbali zimeweza kutuibulia ujumbe ufuatao.
· Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Mfano wananchi wa kufikirika walikuwa na umoja katika kufanikisha ustawi wa nchi yao hali kadhalika watu wa kufikirika walikuwa na umoja na ushirikiano katika kufanikisha mfalme wao anapata mtoto.
· Kwenye upendo, umoja na ushirikiano hakuna vurugu na matatizo mbalimbali.ustawi wa nchi ya Kufikirika umetokana na umoja na ushirikiano waliokuwa nao.
· Jamii isijiegemeze katika imani za kimila na kitamaduni tu bali iangalie upande mwingine. Hii inatokana na ukweli kwamba wanakufikirika walikuwa hawaamini masuala ya hospitali badala yake walikuwa wanaamini mambo ya kimila na kitamaduni.
· Ujinga na werevu wa mtu hupimwa kwa matendo na sio kazi anayoifanya. Hii inatokana na watu wa kufikirika ambayo walikuwa wanapima werevu na ujinga wa mtu kutokana na kazi zao.
· Ujumbe mwingine ni kwamba viongozi lazima wadumishe sheria za nchi ili kuleta usawa na amani katika nchi.
Hivyo Shaaban Robert anaitaka jamii ibadilike kwa kuzingatia maonyo na maadili yapatikanayo katika riwaya ya kufikirika.
Kipengele kingine ni migogoro, mgogoro ni mvutano kati ya pande mbili au zaidi.mwandishi Shaaban Robert katika riwaya hii ya kufikirika ameonyesha migogoro mbalimbali kama vile mgogoro wa kiuchumi,kijamii,kisiasa,utamaduni na mgogoro wa nafsi.
Tukianza na mgogoro wa kiuchumi, Mwandishi ameonyesha jinsi nchi ya kufikirika ilvyoyumba kiuchumi kutokana na mali zote za nchi zilivyotumika katika kumtibu mfalme na malkia na mwishowe shughuli za nchi zilisimama.uk (8-12).
Pia kuna mgogoro wa kijamii, mwandishi ameonyesha mgogoro wa mfalme na malkia kwa kukosa mtoto,kwakua walijiona hawana umuhimu katika jamii ingawa walikua na mali nyingi. Uk(1-6).
Pia mgogoro mwingine wa kijamii ni kati ya mfalme na waganga kwamba makundi matano ya waganga waliokusudiwa kumtibu mfalme na malkia walishindwa kuwatibu.uk(8-13).
Mgogoro mwingine wa kijamii ni kati ya mfalme na waliotakiwa kutolewa kafara,kwamba katika nchi ya kufikirika suala la mtu kutolewa kafara ni suala ambalo haliendani na sheria za nchi ya kufikirika.
Vilevile kuna mgogoro wa nafsi uliojitokeza kwa mfalme,jinsi mfalme alivyokua akiumia juu ya kukosa mtoto kwa muda mrefu takribani miaka kumi baada kuoana na malkia.
Pia malkia alikua na mgogoro na nafsi yake juu ya kukosa mtoto kwa muda mrefu tangu kuoana kwao.
Hali kadhalika kuna mgogoro kati ya waziri mkuu na wajumbe juu ya kubadili mfumo wa uongozi.
Pia kuna mgogoro kati ya ukale na usasa,kwamba wananchi wa kufikirika waliamini sana mambo ya kishirikina wakati Utubusara alikua akijaribu kuwaelimisha juu ya mambo ya sayansi na teknolojia na waachane na mambo ya zamani.
Pia kuna mgogoro wa kisiasa, mwandishi ameonyesha jinsi mfalme alivyokua ameegemea kuongoza nchi yake kupitia mila na desturi, lakini tunaona jinsi Utubusara alivyokua akijaribu kuishauri jamii ya kufikirika kuepukana na mila zilizopitwa na wakati na waegemee katika sayansi na teknolojia ili waweze kuleta mabadiliko.
Falsafa, kiujumla falsafa ni mchujo wa welekeo wa mawazo muhimu yajitokezayo kila mara katika kazi mbalimbali za msanii ( Senkoro 2011). Katika kazi hii shabaan Robert anaonekana kutawaliwa na falsafa kuwa mila na tamaduni zilizopitwa na wakati hazina nafasi katika nkipindi hiki cha sayansi na teknolojia.
Msimamo, msimamo ndio uwezao kuwatofautisha wasanii wawili wanaotunga kazi za fasihi zilizo na kiini na chimbuko moja ( senkoro 2011). Katika kazi hii mwandishi shaaban Robert anaonekana kuwa na msimamo wa kiyakinifu. Kwa mujibu wa mwandishi anaona katika kipindi cha sayansi na teknolojia mila na tamaduni za zamani zisipewe nafasi.
Mtazamo, mwandishi shaaban robert anaonekana kuwa na mtazamo wa kimapinduzi, mwandishi anaona kuwa ili jamii isiangalie mila na tamaduni tu bali iangalie mambo ya sayansi na teknolojia.
Baada ya kuchambua vipengele vya maudhui sasa tugeukie vipengele vya kifani.kiujumla fani katika fasihi ni ule ufundi wa kisanaa anaotumia msanii katika kazi yake(Senkoro 2011). Katika kuchambua vipengele vya fani tutajikita katika muundo, mtindo, wahusika, mandhari na matumizi ya lugha.
Wahusika, hawa ni watu, ama viumbe, waliokusudiwa wawakilishe dhana, mawazo au tabia za watu, katika kazi za fasihi. Katika riwaya ya kufikirika mwandishi Shaaban Robert amepambanisha wahusika mbalimbali katika kuibua au kusindikiza dhamira zake. Baadhi ya wahusika aliowatumia ni kama wafuatao
Mfalme, huyu alikuwa ndiye kiongozi au mfalme wa nchi ya kufikirika ambaye aliongoza vema na alikuwa mtu mwenye huruma na upendo na watu wake. Hali kadhalika mfalme alikuwa ni jasiri na mzalendo aliyepigania haki za raia wake na kuzilinda sheria za nchi ya kufikirika. Licha ya mali na furaha yote aliyonayo mfalme lakini kwa kipindi kirefu cha maisha yake mfalme amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kukosa mtoto. Kupitia uhusika alioubeba mfalme ameibua dhamira mbalimbali kama vile suala la uongozi, ujasiri na uzalendo, umuhimu wa kuwajali wanawake na imani potofu.
Malkia, huyu alikuwa ni mke wa mfalme ambaye pia alikuwa anasumbuliwa na tatizo la utasa. Ni mwanamke mvumilivu na mwenye subira hivyo anafaa kuigwa na jamii. Mwandishi kwa kumtumia mhusika malkia ameibua dhana ya utasa na uvumilivu.
Utu busara ujinga hasara, ni mhusika aliyeibua dhamira nyingi katika riwaya hii ya kufikirika, alikuwa ni mtu makini na mwenye upeo mkubwa katika kufikiria mambo. Huyu ndiye aliyetabiri kuzaliwa kwa mtoto wa mfalme, baadae akawa mwalimu wa mtoto wa mfalme na baadae akajiingiza katika ukulima( uk 49). Hekima na uelewa aliokuwa nao ulikuwa ngao tosha iliyomsaidia kujikomboa kutoka katika vikwazo vyote alivyokumbana navyo, hakika ni mtu anayefaa kuigwa katika jamii.
Mwerevu, huyu alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alionekana ni mwerevu kutokana na kazi yake. Ama hakika ni mtu aliyajaa dharau na majivuno( uk 40) anasema,
.............Huwaje, wewe mvaa koja la ushanga shingoni kama mwanamke kupata njia! Una sifa zaidi ya ujinga. Nashangaa kwanini hawakutakiwa wajinga wawili kwa kafara hii! Ujinga ni ila ya kustahili upanga wa chakali.
Kwa hakika utu busara alileta mwanga katika nchi ya kufikirika juu ya imani na tamaduni zilizopitwa na wakati.
Waziri mkuu, huyu uwakilisha viongozi wanaopindisha sheria kwa manufaa ya watu wachache. Mwandishi anamchora mhusika huyu kama mtu ambaye aliyetumia vitisho na nguvu katika kushawishi wajumbe kukubaliana na ubadilishaji wa sheria. Hakika hafai kuigwa na jamii hasa katika kipindi hiki cha mabadiliko.
Muundo, Katika kazi ya fasihi muundo ni mpango na mtiririko wa kazi hiyo kwa upande wa visa na matukio( Senkoro 2011). Hivyo katika riwaya hii ya Kufikirika mwandishi Shaaban Robert ametumia muundo wa moja kwa moja ambapo amesimulia kitabu mwanzo hadi mwisho. Katika kuipamba kazi yake mwandishi Shaaban Robert ameigawa riwaya yake katika sehemu ndogondogo , Kila sura ina kichwa cha habari. Sura hizo ni kama vile Mfalme, Waganga, Matokeo ya utabiri, Mtoto wa mfalme na Kafara. Pia sura ya tano ameigawa katika sehemu kuu mbili na kuipa jina la Baraza na Gereza.
Mtindo, katika kazi ya fasihi ni ile nama mbayo msanii hutunga kazi hiyo na huipa sura ambayo kifani na kimaudhui huainisha kanuni au kawaida zilizofuatwa kama ni zilizopo( za kimapokeo) au ni za kipekee( senkoro 2011). Mwandishi shaaban Robert katika kazi yake hii ametumia mtindo wa masimulizi yaani amesimulia matukio yote katika mtiririko unaofaa.pia nafsi zote zimetumika, hali kadhalika katika kuipamba kazi yake mwandishi ametumia ushairi ( uk 18-19) anasema.
Jina lipewe wana
Kulikariri kwa moyo
Waelezewe maana
Wakuze wayatendayo
Kama milivyoona
Matendo ya mtu huyo
Katenda bora sana
Kwa tuzo apewayo
Pia katika riwaya hii, mwandishi ametumia mtindo wa kutoa maana ya meneno magumu mwishoni ili kufanya kazi yake ieleweke kwa urahisi.
Mandhari. Mandhari ni mahali au sehemu ambayo kazi ya fasihi inatendeka. Katika riwaya ya kufikirika mwandishi shabani robert ametumia mandhari ya Kufikirika, kwani hata nchi inayozungumziwa ni ya Kufikirika, pia nchi zilizopakana na nchi ya Kufikirika nazo ni za kufikirika. Pia mwandishi ametumia muktadha halisi kama vile Gerezani, Nyumbani kwa Mfalme, Bustanini ( uk 1) na Shambani. Kupitia mandhari hizi mwandishi Shabani Robert ameibua dhamira mbalimbali ambazo tumejadili hapo awali.
Matumizi ya lugha, hujumuisha jinsi mtunzi alivyotumia lugha katika kuwasilisha kazi yake. Matumizi ya lugha hujumuisha misemo, nahau, methali na tamathali za semi.
Methali, methali zilizotumika katika riwaya hii ni kama vile, nyumba ya mgumba haina matanga (uk 5),mwenye haya hazai (uk 6),
Misemo, katika riwaya ya kufikirika misemo iliyotumika ni kama ifuatayo. Dunia haifichi siri (uk 23), maisha ni kama kuwa katika bahari ( uk 24).
Tamathali za semi, haya ni maneno ambayo hutumiwa na wasanii wa fasihi ili kutia nguvu katika maana, mtindo na hata sauti katika maandishi au kusema. Pia tamathali za semi hutumika ili kupamba lugha au mazungumzo. Katika riwaya ya kufikirika mwandishi Shaaban Robert ametumia tamathali mbalimbali kama ifuatavyo:
Tashibiha, katika tamathali hii watu ama vitu viwili au zaidi hulinganishwa na watu ama vitu vingine kwa kutumia maneno kama mithili, kama, n.k, katika riwaya hii tahibiha zilizojitokeza ni kama vile kichwa chake kilishindiliwa kama gunia (uk 29),sauti ya waafrika ni kali kama ile ya radi ( uk 6)waliweza kunusa kama mbwa mwitu( uk 8), akili yake kali kama wembe ( uk 38), maswali aliyamimina kama maji ( uk 29), mtu mdogo kama mbilikimo (uk 41)
Tashihisi, katika aina hii vitu visivyo na sifa walizonazo watu hupewa sifa hizo. Katika riwaya hii mwandishi Shaaban Robert anabainisha tashihisi zifuatazo,sauti ya ndege waliokuwa wakiimba matawini kwa kuagana na mchana ilikuwa na simanzi masikioni (uk 1)
Sitiari, hii ni tamathali ambayo hulinganisha vitu bila kutumia viunganishi, mwandishi wa riwaya hii ametumia sitiari zifuatazo, mjinga ni mnyama ( uk 41), wanawake ni malaika( uk 40).
Mubalagha, ni tamathali ya semi ambayo hutia chumvi au hukuza jambo. Katika riwaya ya Kufikirika mwandishi ametumia mbinu hii katika( uk 11) siku hiyo kuni, mkaa, na mafuta yote yalikwisha kwa kuchoma hirizi hizo, moshi mwingi uliruka juu ukatanda katika hewa kama wingu kubwa la mvua.
Jinala kitabu, Jina lakitabu kufikirika linasadifu yaliyomo .Kwanza nchi yenyewe ya kufikirika ni nchi ambayo haipo,mwandishi anaonyesha kwamba hata mfalme mwenyewe haijui mipaka ya nchi yake.Hata nchi zinazopakana nazo ni nchi za kufikirika tu.Nchi kama Anasa,Majaribu,Bahari ya kufaulu na safu ya milima ya Jitihada vyote ni vya kufikirika tu.
Kwa upande wa maudhui, mambo ya kafara ni ya kufikirika tu,kwani mambo hayo katika jamii zetu hayapo.Matibabu mengi siku hizi hufanywa hospitalini,ambako kuna wataalamu waliosomea taaluma hii ya uganga na sio miti shamba kama wananchi wa kufikirika.
Kwa kuhitimisha tunaweza kusema kuwa mwandishi shaaban robert kwa kiasi kikubwa ameonesha matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii na kuyatolewa ufumbuzi.
Marejeo
Robert, S (1991) Kufikirika.Dar es salaam. Mkuki na nyota publishers.
Senkoro, F.E.M.K (2011) Fasihi. Dar es salaam. KAUTTU.

UHAKIKI WA RIWAYA YA KUSADIKIKA

UTANGULIZI
Katika kujadili vipengele mbalimbali vya Fani na maudhui vilivyotumiwa katika riwaya ya kusadikika iliyoandika na Shaaban Robert Washiriki hatukujikita zaidi katika kujadili maana ya riwaya za wataalamu mbalimbali bali tuliweza kujadili kazi hii kwa kuchambua vipengele vya fani na maudhui kutokana na masimulizi ya nchi ya Kusadikika.
Masimulizi ya kitabu kwa kifupi.
Riwaya ya kusadikika ni kitabu kinachoelezea masimulizi ya nchi ya kusadikika ambayo mwandishi ameanza kwa kusimulia tukio la kushitakiwa kwa Karama ambaye ndiye Mhusika mkuu kwa tuhuma za kuihujumu serikali ya Kusadikika. Kwa maelezo ya Waziri Majivuno aliwasilisha mashitaka haya mbele ya Mahakama eti kwa sababu Karama alikuwa akitoa elimu ya sheria ambayo kwa Mtazamo wa Waziri huyu alidai kuwa angewafanya raia wa kusadikika kuelewa haki zao ambako kungepelekea wananchi hao kutotii serikali au kwa namna nyingine kungekomesha unyanyasasaji, uonevu na uongozi mbaya wa watawala wa kusadikika na hivyo waziri Majivuno alijawa hofu kubwa sana.
Riwaya imeendelea kusimulia namna mshitakiwa Karama alivyowasilisha utetezi wake mbele ya Mahakama ya Kusadikika iliyoundwa na Mfalme na Madiwani. Karama aliwasilisha utetezi huo kwa kuthibitisha jinsi serikali ilivyoshindwa kuthamini michango mbalimbali ya wananchi wake kwa kuelezea historia wajumbe mbalimbali waliojitoa kwenda kufanya utafiti wa namna ya kuendeleleza nchi yao. Masimulizi yake yaliwataja hasa wajumbe 6 waliotumwa mipakani au pande zote 6 ambazo nchi ya kusadikika inapakana nayo. Pande hizo ni Kaskazini, Mashariki, Kusini, Magharibi, Mbinguni na Ardhini. Hatima ya wajumbe hawa ambao walikuwa wazalendo waliishia Kifungoni pindi waliporejea kutoka walikotumwa.
Mwisho wa riwaya hii mwandishi anaelezea hukumu ya Karama ambapo Mahakama iliyoongozwa na Mfalme ilivyomtoa hatia mtuhumiwa kwa kauli moja ya kuwa hana hatia na Mfalme kuagiza wajumbe wote waliokuwa wanatumikia kifungo kufunguliwa na kulipwa fidia kwa kunyanyaswa pamoja na jitihada zao.
Baada ya muhtasari wa masimulizi ya nchi ya kusadikika tuliweza kujadili vipengele vinavyounda Fani na Maudhui ya kazi ya riwaya ya kusadikika kama ifuatavyo;-
Fani ni ujuzi au Mbinu mbalimbali azitumiazo msanii kuwasilisha ujumbe au Fikra zake kwa hadhira aliyoikusudia. Fani inaundwa na vipengele vya Mandhari, Wahusika, muundo, Mtindo na Matumizi ya lugha.
Maudhui ni jumla ya mawazo yanayowasilishwa na msanii wa kazi ya kifasihi katika kazi yake. Maudhui huundwa na vipengele vya Dhamira, Ujumbe, Falsafa, Migogoro, Mtazamo na Msimamo.
Uchambuzi wa Vipengele mbalimbali alivyovitumia mwandishi wa riwaya hii ya Kusadikika ni:
Mandhari: ambayo humaanisha mahali au sehemu ambayo tukio linafananyika. Mwandishi ametumia mandhari ya Kufikirika ambayo haiwezi kujidhihirisha kwa macho ya kawaida (haionekani) kwani ni nchi inayoelea angani. Pia ametumia mji wa sadiki na mipaka au pande sita zinazopakana na nchi hii za Kaskazini, Mashariki, Kusini, Magharibi, Ardhini na Mbinguni.
Wahusika ni mtu au watu, wanyama, na mimea anaotumia mwandishi katika kuwasilisha kazi yake kwa hadhira iliyokusudiwa. Kwa kiasi kikubwa Mwandishi ametumia Wahusika ambao aliowapa majina yanayosawiri tabia zao na wahusika ambao hawabadiliki badiliki ;-
Karama, Huyu ni mhusika mkuu ambaye pia alikuwa Jasiri na Shujaa, Mwanasheria, Mzalendo mtetezi wa haki na Mshitakiwa. Vilevile mhusika huyu alichorwa mwema kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Majivuno, Waziri wa kusadikika, mwenye uchu wa madaraka, mwenye haiba, asiye na uzalendo, kiongozi anayelindwa na Mfalme na asiye na shukurani.
Mfalme, Kiongozi wa kusadikika, Katili, Mjinga, mwenye tama ya uongozi, mkuu wa baraza la Mahakama.
Madiwani, Wasaliti, wakuu wa mahakama, waonevu, wakatili, wenye dhuluma na sio wazalendo.
Mudir wa sheria, mwanasheria wa serikali, Mjinga, msaliti na asiye mzalendo.
Buruhani, Mjumbe wa kaskazini, Jasiri, Mzalendo mpenda haki, Mwanaharakati, Mfungwa na maskini. Msanii anasema “Hii ilikuwa safari ya ujasiri iliyotaka uthabiti na matumaini, mwenye heshima, hodari na mwaminifu alitakiwa ajitolee mwenyewe kwa safari hii” uk.12.
Fadhili, Mjumbe aliyetumwa mashariki, Jasiri, Mzalendo, mpenda haki, Mfungwa na maskini. “Mtu mwenye sifa njema alitakiwa kujitolea mwenyewe kwa ujumbe wa mashariki na mtu kama huyu alipatikana upesi sana kuliko ilivyokuwa ikitazamiwa” uk.16.
Kabuli, Mjumbe wa kusini, jasiri, Mzalendo, Mpenda haki, Maskini na mfungwa.
Auni, Mjumbe wa Magharibi, Jasiri, Mzalendo, Mpenda haki, Mwananchi wa kawaida na mfungwa.
Sapa na Salihi, walikuwa vipofu, wananchi wa magharibi, Sapa alikuwa mwenye tama na wivu, Sapa alikuwa mpole, Sapa aliomba upofu.
Radhaa, mjumbe wa mbinguni, Jasiri, mzalendo, mpenda haki, Mfungwa na Maskini.
Amini, mjumbe wa ardhini, Jasiri, mpenda haki, mzalendo na mfungwa.
Wahusika wengine ni wananchi, bwana Taadabuni, katibu wa serikali, bwana Komeni, Amiri jeshi, bwana fujo, mlinda hazina, bwana Baromini na wananchi wa pande zingine.
Muundo, ni namna au jinsi mwandishi anavyopangilia visa na matukio katika kazi yake ya kifasihi. Mwandishi ametumia muundo wa moja kwa moja ambapo katika mpangilio wa masimulizi ameanza mwanzo wa kisa kwa kuonesha jinsi mashitaka yalivyowasilishwa, kukafuatiwa na utetezi wa mshitakiwa au kile mwandishi alichokiita maombezi mbele ya Mfalme na Madiwani kwa kusimulia historia ya kusadikika kupitia wajumbe sita waliotumwa pande sita na kuishia kifungoni kama sehemu ya pili ya kisa na hatimaye alimalizia kwa kuelezea hukumu ya kesi ya Karama ambapo Mfalme na Madiwani walionesha kuwa mtuhuma hakuwa na hatia na kufunguliwa kwa wajumbe sita na kuachiwa huru huku Mfalme akiamuru walipwe fidia.
Mtindo. Ni namna mwandishi anavyoiumba kazi yake ya kifasihi. Mwandishi Shaaban Robert ametumia mitindo mbalimbali katika kazi hii ya riwaya ya kusadikika kama vile, ametumia maswali hasa katika sehemu ya mwisho ya kitabu, ametumia dayalojia kati ya Sapa na Salihi uk. 29, ametumia masimulizi kwa kiasi kikubwa katika kazi hii ambayo kwake ndio mbinu kuu pamoja na matumizi ya nafsi ya pili na tatu umoja na nafsi ya tatu wingi sehemu kubwa ya riwaya.
Lugha. Mwandishi ametumia lugha ngumu ambayo si rahisi kueleweka kwa msomaji kutokana na kutumia misamiati isiyoeleweka. Hali hii ya kutumia lugha ngumu ililengwa kukwepa makucha ya wakoloni. Mfano wa misamiati hiyo ni sudusi, takirifu, kafaungo, hutasawari, akapatilizwa, ali, kujikagajuu, Kuyabisika, kujikaga, Kadura n.k. Pia mwandishi ametumia vipengele vya Tamathali za semi ambazo ni ;-
Methali. Kitanda usichokilalia hujui Kunguni wake.
Msiba wa kujitakia hauna kilio. Lila na fila hawatangamani.
Misemo.
Kumtosa mshitakiwa katika bahari ya maangamizi.
Tashibiha.
Umri wake mkubwa ulizofanya nywele zake za kichwani kuwa nyeupe kama fedha.
Uso wa kipofu wa kwanza ulikuwa na furaha kama bwana harusi.
Alikuwa na tabia ya kuficha siri kama kaburi lifunikalo maiti.
Anamaneno kama kitabu
Tashihisi.
Giza limezalo nuru na ufupisho uoni wa macho.
Wakati una mabawa kama ndege uk. 11.
Jina la Kitabu (KUSADIKIKA). Jina la kitabu linasawiri yaliyomo katika riwaya hii kwani limetokana na neno “sadiki” likimaanisha “Amini” hivyo linaweza kusemwa kuwa ni kuaminika. Mwandishi anatuonesha kuwa Wasadikika ni wajinga kwani hawakujihusisha na uchambuzi wa masuala yake waliishia kuamini na kukubali kila jambo mwandishi anasema “Imani ya Kusadikika ni nguzo imara ya majengo ya utawala wa Wasadikika” wakati mataifa mengine yalipojifananisha kwa mambo kama vile enzi, uwezo na fahari nyingine taifa la kusadikika lilijivuna kwa sababu ya kusadiki mambo yaliyotoka vinywani mwa watu wake” uk. 4-5.
Kwa washiriki wa uchambuzi huu wanakiri kuwa kwa kiasi kikubwa tumefanikiwa kuchambua haya katika vipengele vya fani na maudhui alivyotumia msanii Shaabani Robert katika riwaya ya Kusadikika ingawa si vyote vilivyotumika katika vipengele hivi tumeweza kuviainisha. (rejea masimulizi ya kitabu)
KIPENGELE CHA MAUDHUI.
Maudhui ni jumla ya mawazo aliyonayo msanii katika kazi yake ya kifasihi, Kipengele cha maudhui kinaundwa na ujumla, dhamira, migogoro, falsafa, Msimamo/Mtazamo.
Dhamira mbalimbali
Dhamira kuu ni Ukombozi: Dhamira hii ndio kuu katika riwaya ya kusadikika iliojikita kwenye ukombozi wa kifikra na ukombozi wa kisiasa. Mwandishi amemtumia mhusika karama aliyeanzisha elimu ya sheria yenye lengo la kuwezesha wananchi ili wawezekushiriki katika mambo mbalimbali ya nchi.
Ukombozi wa kisiasa unarejelea harakati zilizoongozwa na Karama na wajumbe sita zenye lengo la kuleta mabadiliko katika nchi ya kusadikika kuhusu haki na uongozi (viongozi). Msanii anasema “Kwa nini wanasiasa wa kusadikika hawakuwaacha kama Karama kujishughulisha na mambo yaliyowapita vimo vyao”
Matabaka. Hali ya wahusika kuwa na hadhi au makundi au madaraja tofauti tofauti. Katika riwaya ya kusadikika ameonesha matabaka ya namna mbalimbali kama;-
Tabaka la viongozi na wananchi, matajiri na wasomi na wasio wasomi na wenye haki na wasio na haki. Katika kudhihirisha matabaka haya mwandishi ameeleza kwa mifano baadhi ya maeneo haya anasema “Sheria za wasadikika zilikuwa hazimuamuru mshitakiwa kujitetea juu ya ushahidi wa mshitaki. Aghalabu mashitaka mengi yalikubaliwa bila ya swali wala kiapo kama mashitaka yaliletwa mbele ya baraza na wafalme, watoto wao, matajiri au watu wengine maarufu nguvu ya desturi hii ilifanywa maradufu. Hapana shaka salama ya watu wadogo ilikuwa kidogo sana katika nchi ya kusadikika” uk.7.
Uongozi Mbaya. Mwandishi amedhihirisha hili kwa kuwatumia wahusika waziri Majivuno, Wafalme, Madiwani na matajiri ambao ndio waliochorwa kwa taswira ya kuwa Wanahaki zaidi kuliko wananchi wa kawaida. Tunapozungumzia uongozi mbaya ni hali ya utawala kutowajali kwa kuwasaidia wananchi wa kawaida kisiasa, uchumi, na kijamii.
“Aghalabu Mashitaka mengi yalikubaliwa bila ya swali wala kiapo kama mashitaka yaliletwa mbele ya baraza na wafalme, watoto wao, matajiri au watu wengine maarufu nguvu ya desturi hii ilifanywa maradufu” uk.7.
Uzalendo na ujasiri. Uzalendo ni hali ya mtu kuipenda nchi yake na kujitoa kuipigania katika mambo mbalimbali yanayokwamisha maendeleo. Mwandishi anasema “pigano la kufa na kupona lilikuwa mbele yake” uk.8. “alikuwa hana silaha nyingine za kuokolea maisha ila zana hizi” uk.9. “Msema kweli hukimbiwa na marafiki zake, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa Kitambo nikajinyima ushirika wa milele unaotazamiwa kutokea baada ya kushindwa kwa uongo”uk.9.
Mwandishi amewatumia wahusika Karama, Buruhani, Fadhili, Kabuli, Auni, Radhaa, Amini kuonesha ujasiri na uzalendo walijitoa na kufanyakazi katika masahibu mengi tena bila ya kukata tama huku baadhi wakiishia kifungoni. Hatimaye waliweza kushinda. Mwandishi anasema “kwa kazi zake bora na uaminifu mwingi hakushukuriwa bali kuvunjiwa kadiri, aliaibishwa kuwa alileta uzushi ulikuwa hauna faida katika nchi zaidi ya hayo alitumbukizwa katika kifungo cha maisha”
Ujinga. Hali ya watu kutoelewa mambo mbalimbali ya msingi kijamii kisiasa, kiutamaduni na kiuchumi. Mfano haki sheria na uongozi nakadhalika. Shaaban Robert amethibitisha uwepo wa ujinga katika nchi ya kusadikika kupitia viongozi na wananchi waliosadiki mambo yao na kuyakana ya nje. Pia mwandishi amewatumia wananchi waliohudhuria mahakamani siku ya kwanza ya mashitaka. Msanii anasema “Baadhi ya watu wachache waliokuja barazani kusikiliza kesi hii walimsikitikia mshitakiwa wengi walikuwa wakinong’onezana kuwa msiba wa kujitakia hauna kilio” uk 7. “ujinga wao haukuyazuia maendeleo tu lakini hasa ulirudisha nchi nyuma vilevile” uk. 14. “Twaona kuwa mshitakiwa hana hatia ila alikuwa akitafuta jinsi ya kuisaidia sheria ya kusadikika kwa njia ngeni” Maelezo haya ni matokeo ya ufumbuzi wa ujinga uliokuwa umekithiri kwa viongozi wa kusadikika na wananchi wake.
Uonevu na Ukandamizaji (kukosekana kwa haki). Hali ya kutothaminiwa, kupewa haki na kuhukumiwa bila ya kufanya kosa lolote, na wakati mwingine kutopewa nafasi ya umuhimu katika tabaka fulani la watu “sheria za kusadikika zilikuwa hazimuamuru mtu yeyote kujitetea juu ya ushahidi wa mshitaki” uk.7. Buruhani, Fadhili, Kabuli, Auni, Radhaa, Amini walifungwa tena kwa kunyanyaswa Mwandishi anasema “Natoa amri watu sita waliotajwa wafunguliwe mara moja, inasikitisha sana kwa dhuluma juu ya watu hawa hazikutengenezwa mpaka leo. Gereza ni makao ya wahalifu na watu hawa si wahalifu” Mhusika mkuu karama pia alishitakiwa na Waziri majivuno kwa hulka tu za ukandamizaji.
Umaskini. Ni hali ya kutomudu kujipatia mahitaji mbalimbali ya kila siku kwa kiwango kinachoridhisha (cha kutosha) Mwandishi anasema “kwa kukosekana kwa Madaraja mito inafanya shida juu ya watu walio ng’ambo moja kukutana na Ng’ambo nyingine, maradhi hayajapata uuguzaji, vifo vya mapema hapa katika mwaka mmoja jumla yake yatisha kuliko ile ya vifo vitokeavyo katika nchi nyingine katika karne moja” Uk. 25. Pia “Aghalabu Mashitaka mengi yalikubaliwa bila ya swali wala kiapo kama mashitaka yaliletwa mbele ya baraza na wafalme, watoto wao, matajiri au watu wengine maarufu nguvu ya desturi hii ilifanywa maradufu. Hapana shaka salama ya watu wadogo ilikuwa kidogo sana katika nchi ya kusadikika” uk. 7. Maelezo haya yanaonesha uwezekano mkubwa wa uwepo wa kundi kubwa la watu masikini ambao ndio walioguswa na sheria za kusadikika.
Dhamira nyingine ndogondogo zilizomo katika riwaya hii ni tamaa iliyooneshwa kupitia Salihi na Majivuno, Unafiki na woga wa wananchi wa kusadikika, utengano na kukosekana kwa umoja.
Migogoro. Hali ya kutoelewa au kuridhishwa na jambo fulani na kupelekea kutoelewana kwa makundi au pande mbili za watu. Katika riwaya hii kuna migogoro ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.
Migogoro ya kijamii. Mfano wa migogoro ya kijamii ni mgogoro wa Sapa na Salihi uliotokea baada ya Sapa kuomba upofu kutokana na tama ya Salihi kutamani vitu vya Sapa, Mwandishi anasema “kwa sababu hii tuliafikiana kushirikiana kila kitu atakachoomba tukaandikiana hati mbele ya Kadhi. Palepale mwenzangu aliinua mikono yake juu akaomba upofu” uk.30
Mgogoro nafsia: ni hali ya mtu kuhofia jambo fulani na kupelekea mtu huyo kuwa namsongo wa mawazo, Mwandishi amemtumia waziri Majivuno aliyekuwa na hofu ya kupoteza madaraka na kukomeshwa kwa ukandamizaji endapo wananchi wataelewa sheria mbalimbali za kusadikika waliokuwa wakielimishwa na Karama. Hatimaye aliamua kumshitaki katika baraza msanii anasema “Upelelezi huo ulidhihirisha bila ya shaka yoyote kuwa mshitkiwa akiwafunza watu sio kuomba msamaha na huruma katika baraza tu lakini hata kuzibatilisha hukumu za baraza la kusadikika kwa njia zote hii inaonesha kuwa mgogoro mkubwa utakuwako kati ya sheria za nchi na watu wake” uk 2.
Migogoro ya Kiuchumi. Mgogoro wa walionacho/matajiri ambao ndio waliopewa haki na upendeleo na Maskini walionyimwa haki hata mbele ya sheria na mahakaka.Katika nchi ya kusadikika watu hawa hawakuweza kabisa kushirikiana.Mwandishi anasema “Aghalabu Mashitaka mengi yalikubaliwa bila ya swali wala kiapo kama mashitaka yaliletwa mbele ya baraza na wafalme, watoto wao, matajiri au watu wengine maarufu nguvu ya desturi hii ilifanywa maradufu. Hapana shaka salama ya watu wadogo ilikuwa kidogo sana katika nchi ya kusadikika” uk. 7.
Migogoro wa Kisiasa. Huu ni mgogoro unaowahusisha wanaharakati wazalendo walioongozwa na karama dhibi ya serikali na viongozi wan chi ya kusadikika. Wanaharakati hao walihitaji mabadiliko na walichoshwa na uonevu wa viongozi wao, mgogoro huu ndio uliopelekea wananchi kuishia kifungoni pindi walipojitolea kudai mabadiliko.
Ujumbe. Uongozi mbaya unachangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha maendeleo ya wananchi. Kuwepo kwa hali ya uzalendo katika nchi ni chachu ya maendeleo na mafanikio katika jamii. Suala la uelimishaji (elimu) ni muhimu katika utambuzi wa wananchi katika shughuli mbalimbali za kijamii.Tamaa na viongozi kujali maslahi kunapelekea hali duni ya wananchi walio wengi. Viongozi wanapaswa kuthamini haki za wananchi wanaowatumikia.
Msimamo wa Mwandishi. Msimamo wa mwandishi katika riwaya hii ni wa kimapinduzi kwani anaonesha jinsi jamii ilivyopaswa kujituma tena kwa ujasiri, kupigania haki na mabadiliko ya wananchi wote.
Mtazamo wa Mwandishi. Mtazamo wa mwandishi wa riwaya hii ni wa Kiyakinifu kwani kwa kiasi kikubwa umeakisi mambo ambayo yanaweza kufuatwa katika kufanikisha maendeleo ya jamiii yeyote kama vile mgongano wa mawazo uzalendo na ujasiri, uelewa na mambo mengine. Aidha yapo baadhi ya maeneo yanagusia mtazamo wa kidhanifu kama vile kusadiki kila kinachosemwa na watawala.
Falsafa ya mwandishi. Falsafa ya mwandishi ni ya wema hushinda ubaya, amedhihirisha hili kupitia mhusika Karama aliyechorwa kama mtu mwema dhidi ya Majivuno aliyechorwa kama mtu mbaya. Kwa taswira hii Karama amewakilisha wema wote katika jamii ya wasadikika na Majivuno anawakilisha wabaya wote katika jamii hiyohiyo.




UCHAMBUA WA KITABU CHA MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI-MWANDISHI: SHAABAN ROBERT
UTANGULIZI
Kitabu cha Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini ni riwaya iliyoandikwa na Shaaban Robert (1936-1946) yenye insha na mashairi yanayoelezea mambo aliyoyafanya kuanzia umri wa ujana mpaka uzee wake, pamoja na mafanikio mbalimbali aliyoyafikia, changamoto alizokumbana nazo na namna alivyozitatua.
DHAMIRI YA MTUNZI
Kwa mujibu ya kamusi ya Karne ya 21(2011) inafafanua kwamba, dhamiri ni ile azma, kusudio au nia ya kufanya jambo. Katika muktadha wa kifasihi tunaweza kusema dhamiri ni lile lengo au kusudi la mtunzi katika kuitunga kazi yake. Na hii inatuthihirishia kwamba, kila mtunzi husukumwa na jambo fulani (ama zito ama jepesi) katika utunzi wake. Hakuna mtunzi anayetunga kazi yake katika ombwe. Mwandishi yoyote yule hata kama anaandika tungo za kubuni, kwa kawaida huwa amesukumwa na jambo au mambo fulani aliyowahi kusikia, kushuhudia katika fikra zake au katika hali halisi maishani; na fikra hizo hujengwa na mambo fulani ya tajiriba halisi katika maisha halisi.
Hivyo Shaaban Robert katika kitabu chake cha “Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini” suala la msingi lililomsukuma mpaka kuandika kitabu hiki ni kutaka kuweka kumbukumbu nzuri juu ya maisha yake kwa yale yote ambayo aliyafanya akiwa kama mwandishi maarufu wa Afrika Mashariki na Kati, hususani kwa vizazi vijavyo ambavyo havikupata bahati ya kumwona mwandishi huyu, kwa hiyo kwa kupitia kazi yake hii waweze kujifunza mengi na kupata mafanikio katika maisha.
NADHARIA YA UHALISIA
Kwa mujibu wa Ntarangwi (2004) anasema nadharia hii katika upana wake, humaanisha uwakilishi wa uhalisi wa mambo katika fasihi. Nadharia hii ilizuka katika karne ya kumi na tisa hususani kwa lengo la kupinga mkondo wa ulimbwende. Mhalisia huamini katika matokeo ya mambo na ukweli anaouzingatia ni ule unaoweza kuonekana na kuthibitishwa kwa tajirba. Vile vile, wanauhalisia huiamini demokrasia kama hali ya maisha, na malighafi ya kuelezea maisha ya kawaida, ya kadiri na ya kila siku. Hivyo basi uhalisia hujikita katika mambo yaliyopo, tukio mahsusi na matokeo yanayoweza kuthibitika.
Imani ya mhalisia ni kwamba kazi ya fasihi yapaswa kuwaweka wanajamii husika katika ulimwengu wao wa kawaida, wa kweli, na halisi. Hivyo basi hata picha za ulimwengu atakazoumba msanii, zapaswa kudhihirisha hali hiyo.
Mhakiki anayezingatia nadharia hii ya uhalisia, hupembua namna mtunzi alivyodhihirisha uhalisi wa mambo kupitia maudhui aliyoyazingatia na wahusika aliowasawiri. Hivyo basi, mhakiki hutizama jinsi ukweli ulivyodhihirishwa katika juhudi za mtunzi za kuchora hali halisi ya mambo katika wakati maalum. Kwa muhtasari basi msanii anatarajiwa kusawiri wahusika, matukio na mandhari yanayokubalika na kuaminika katika jamii ya wakati wake. Ufahamu wa mazingira na maisha anayoyalenga mtunzi ni nguzo muhimu kwa mhakiki wa kihalisia. Shida inayoletwa na nadharia hii ni kuchukulia kwamba uhalisi na maana yake hauna utata wowote katika jamii yoyote, ni kwamba unachukulia kuwa watu wote katika jamii hiyo wanaona uhalisi mmoja na kuwa na fasili sawa kuhusu maisha yao.
Haki na uaminifu; Shaaban Robert anaona kuwa uaminifu na kutenda haki ni nuru ya maisha bora kwa mwanadamu hapo baadaye. Dhamira hii inajidhihirisha katika insha yake ya Umri uk.2 anasema, “Milango ya nyuma ya kuifikia bahati ilikuwa mingi lakini haikunishawishi hata kidogo”. Suala hili linahusisha hata katika jamii zetu za leo, kwani watu wengi hutumia milango ya nyuma katika kufikia mafanikio. Kwa mfano; kwa kutoa rushwa, ufisadi nk.
Dhuluma na uonevu; Shaaban Robert anaeleza kuwa dhuluma na uonevu vimekuwa ni vipingamizi vikubwa katika mafanikio ya mtu ya kila siku, kwa mfano kama vile kunyimwa jambo fulani au kukandamizwa kwa sababu fulani ni ukuta katika maendeleo binafsi na ya jamii kwa ujumla. Jambo hili linajibainisha katika uk.1 “Mara kwa mara niliposimama wima kuiendea niliteleza nikaanguka chini. Nilipotaka kunyoosha mkono kuishika yalitokea mazuio ambayo sikuyatazamia au nilifungiwa milango ya mbele nisionane nayo”.
Vilevile katika insha ya Mwandishi S. Robert ameonesha ni kwa namna gani alivyodhulumiwa katika uchapaji wa kazi zake. Kwa mfano, uk.78 anasema; “Kwa kazi yangu iliyoweza kuleta sh.25000/- kwa vitabu 5000/- katika mwaka 1954 sikupewa hata pesa moja ya shaba kwa muda wa miaka kadhaa…sikupata kitu kwa kazi yangu iliyoleta karibu sh.15000/- kwa vitabu 5000/- katika mwaka 1958”. Pia anaonesha ni kwa namna gani alivyozidi kudhulumiwa na hata wale ambao walichukua madaraka baadaye. Mfano; uk.79 “Nilikuwa mtumishi wa bure na mtu wa chini kuliko pembe nyeusi yoyote iliyopata kuwako katika ulimwengu huu. Kwa nani? Kwa wale waliofadhiliwa na waliotajirishwa na waliotumikiwa na waliofunzwa na kazi zangu”
Katika jamii yetu ya leo hususani Tanzania tunaona mambo haya yamekithiri sana. Hivyo basi, ili jamii iweze kuondokana na hali hii ni lazima iungane pamoja na kupinga dhuluma na uonevu. Pia kwa kuzingatia haki ya mwandishi S. Robert anasema; uk.80 “Mwandishi si mtu wa ajabu awezae kuishi kwa kula hewa na kunywa ukungu. Ni mtu wa desturi ambaye kama watu wengine wa desturi, hafarijiwi na hasara”.
Ugumu wa soko la vitabu; Mwandishi ameonesha ugumu wa suala hili pale alipofungua duka la vitabu lakini watu hawakuhamasika kununua vitabu hivyo, hali hii ilitokana watu wengi kutokujua kusoma na kutokana na utamaduni wa jamii hiyo katika suala zima la usomaji wa vitabu kwani hawakujua thamani yake, kama asemavyo; uk.110 “Walikuwa katika tarehe ya ujinga wa kujua kuwa mazoea ya kusoma yalikamilisha utu wetu katika dunia. Hawakufahamu kwamba katika vitabu ndimo ghala za utamaduni wa elimu zilimopatikana”. Hali hii inahalisika sana katika jamii ya leo kwani watu wengi wanajua kusoma lakini hawana utamaduni wa kusoma hivyo husababisha soko la vitabu kuwa gumu.
Uzalendo; Suala hili limeoneshwa na S. Robert jinsi gani alivyokuwa mzalendo kwa nchi yake (Tanganyika) katika kupinga mifumo yote ya kiutawala wa kikoloni ambaye ilimdharau mwafrika hususani katika kipengele hiki cha kisiasa, kuwa mwafrika hawezi kufanya chochote. Mfano uk.75 “Mwafrika aliweza kufanya nini? Alikuwa mtu gani mbele ya watu?” hali hii ilimfanya Shaaban Robert kujitoa muhanga katika kushiriki misafara mbalimbali ya kisiasa ili kuhamasisha maendeleo ya mwafrika, japokuwa gharama zote za safari hiyo zilikuwa juu yake. Na hii ilitokana na hali ya uzalendo iliyojaa kifuani mwake, kama asemavyo katika uk.74“Sikuwa na kago juu ya ari hii. Alivyokuwa kila mtu ndivyo nilivyokuwa mimi vilevile. Nilitekwa na uzalendo kama alivyotekwa mtu yoyote mwingine. Sikupenda kuwa mgeni katika nchi ya asili na uzazi wangu”.
Hivyo basi suala hili la uzalendo linahalisika katika jamii ya sasa, kwani watu mbalimbali huingia katika siasa na kutetea maslahi ya haki zao ili kujipatia maendeleo hivyo mwandishi anaitaka jamii ya sasa kujitoa muhanga katika kupingana na utawala mbovu uliojaa dharau kwa wale wanaowaongoza.
Kifo na maisha; Haya ni mambo yaliyomo ndani ya jamii, kama binadamu tunapaswa kuyapokea, kuyakubali na pia kuangalia ni kwa namna gani tutakabiliana nayo. Shaaban Robert anaeleza ugumu wa maisha ya upweke na ukiwa na jinsi alivyoyakabili baada ya kufiwa na mkewe Amina. Uk.4 “…mauti yake ya mapema yalikuwa ni msiba na hasara kubwa kwangu.” Lakini Shaaban Robert anatuonesha kwamba pamoja na matatizo hayo jamii inapaswa kuwa na moyo wa uvumilivu kwani upo wakati mwingine mzuri ujao.
Mapenzi ya dhati; Shaaban Robert anaonesha mapenzi ya dhati aliyokuwa nayo kwa mkewe baada ya kifo. Mfano katika uk.3 anasema, “…tokeo hili lilikuwa pigo kubwa sana kwangu na msiba katika nyumba nzima. Marehemu huyu alikuwa johari ya maisha yangu, tegemeo na mshauri mwema”.
Vilevile alionesha mapenzi ya dhati kwa kuwajali wanae ambao nao walikuwa na upweke wa kumkosa mama yao, alionesha upendo mkubwa kwao kwa kutoacha mwanya wa kujisikia wakiwa. Mfano aliwapatia elimu; uk.5 anasema, “…niliwapenda kwa mapenzi sawa kama baba na mama, nikawatunza kama mboni za macho yangu”. Shaaban Robert anaiasa jamii kuwa suala la kulea watoto baada ya kifo cha mzazi mmoja si la mama tu, bali hata baba kama mzazi anapaswa kuwalea watoto walioachwa tena kwa mapenzi yote ya baba na mama, hivyo si budi jamii kubadilika katika hili.
Nafasi ya mwanamke; Mwandishi Shaaban Robert anamuona mwanamke kama kiungo muhimu sana katika safari hii ya maisha, anamchukulia katika nafasi mbalimbali kama ifuatavyo:
· Mwanamke kama tegemeo na mshauri mwema. Mfano; uk.3 “…marehemu huyu alikuwa jahari ya maisha yangu, tegemeo na mshauri mwema”.
· Pia anamuona mwanamke kama mtu mwenye ushirikiano na asiye mvivu. Mfano; uk.3 “…alinisaidia katika mambo mengi wakati wa maisha yetu pamoja ambayo yangalinishinda kuyatenda mimi peke yangu”. Pia hata katika isha ya Idara ya Utawala Shaaban Robert anaeleza uhodari na uchapakazi wa mke wa Mudir. Mfano; uk. 61 “bibi huyu alikuwa hodari na mcheshi sana”
· Vilevile anaona mwanamke kama mlezi muhimu sana. Kwa mfano; uk.5 “…nilisikitishwa mno kwa ukosefu wa malezi ya mama yao lakini nilikuwa sina uwezo wa kumwita arudi duniani tena”.
· Shaaban Robert anamuona mwanamke kama pambo na faraja katika maisha ya ndoa. Anasema katika uk.3 “Sura yake ilikuwa jamali kwa kimo cha kadirio, uso wake ulikuwa mviringo wa yai, nywele nyeusi za kushuka, paji pana, nyusi za upinde, macho mazuri yaliyokuwa na tazamo juu ya kila kitu, kope za kitana, masikio ya kindo yasiyopitwa na sauti ndogo, meno ya mwanya…”
· Mwanamke pia ameoneshwa…