Mtangazaji maarufu wa kituo cha redio cha Clouds FM, Gardner G Habash (50) amefariki dunia leo Jumamosi April 20, 2024 saa 11 alfajiri.

Msemaji wa Kampuni ya Clouds Media Group, Emilian Mallya amethibitisha kifo cha mtangazaji huyo.


Gadner maarufu kama ‘Captain’ aliejizolea Umaarufu Mkubwa kupitia Kipindi cha Jahazi, alikua amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es Salaam kutokana na kusumbuliwa na Pressure (Shinikizo la Damu)